Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya tabia ya kusoma

‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

‎Kwa Nini Unaacha Kusoma Kitabu Kwenye Ukurasa wa 17? Hii Ndio Sababu Halisi (Na Inashangaza!)

Kwa Nini Ni Vigumu Kusoma Vitabu Mpaka Mwisho? ‎ ‎Kuna jamaa mmoja... ‎Anaitwa Musa Mfalme. ‎ ‎Sio mfalme kweli, lakini akili zake zilikuwa na hazina ya kifalme. ‎Alikuwa na ndoto kubwa sana. ‎Alitaka kuwa tajiri. ‎Mwenye maarifa. ‎Awe mtu wa tofauti. ‎ ‎Siku moja akapata kitabu. ‎Kikubwa. ‎Kimeandikwa kwa rangi ya dhahabu. ‎Juu yake kimeandikwa, ‎“Nguvu Ya Maarifa: Jinsi Ya Kujenga Maisha Yako Kuanzia Sasa.” ‎ ‎Akasema, ‎"Hili ndilo lililokuwa linanikimbia. Leo naanza, mpaka mwisho!" ‎ ‎Akasoma ukurasa wa kwanza. ‎Ukurasa wa pili. ‎Wa tatu... ‎Kichwa kinamwambia, “Bora uangalie TikTok kidogo tu…” ‎ ‎Akachukua simu. ‎Dakika mbili. ‎Zikawa saa moja. ‎Akasema, ‎"Kesho nitaendelea kusoma." ‎ ‎Hakurudi tena kwenye kile kitabu. ‎Mpaka leo. ‎ ‎Lakini Kwa Nini? Kwa Nini Tunashindwa Kumaliza Vitabu? ‎ ‎Hii hapa safari ya ukweli... ‎Safari ambayo Musa Mfalme alipitia na labda na wewe pia. ‎ ‎1. Vitabu Vinataka Nguvu Ya Ndani ‎ ‎Kusoma si kama kuangalia movie. ‎Hakuna kelele....

‎Jinsi Kusoma Vitabu Kunavyobadilisha Ubongo Wako....

  ‎Rafiki Yangu, ‎ ‎Miaka michache iliyopita, nilikuwa mtu wa kawaida sana. ‎Nilikuwa na ndoto kubwa… lakini akili iliyochoka. ‎Kichwa kilijaa mazungumzo ya watu, si ndoto zangu. ‎Nilikuwa nikiamka asubuhi nikijiuliza, “Hivi akili yangu inafanya kazi kwa asilimia ngapi tu?” ‎ ‎Sikujua kuwa kitu kimoja kidogo kingeweza kubadilisha kabisa maisha yangu. ‎ ‎Siku moja, nikiwa napitia changamoto za maisha, nilikutana na kitabu kidogo cha kurasa 120. ‎Jina lake lilikuwa ni "Change Your Thinking Change Your Life” ‎ ‎Kwa dharau nikasema, “Kitabu gani hiki? Kitatofautisha nini?” ‎Lakini kuna sauti ndani yangu ilisema: ‎“Jaribu. Una nini cha kupoteza?” ‎ ‎Nilikubali… Nikaanza kusoma. ‎ ‎Mwanzo kilikuwa kigumu. Ubongo wangu ulitaka kuachana nacho. ‎Nilikuwa nimezoea starehe, sio maarifa. ‎Nilikuwa mwepesi wa kuangalia video, sio kusoma kurasa. ‎ ‎Lakini kwa namna ya ajabu  kila ukurasa niliomaliza, akili yangu iliongezeka nguvu. ‎Nilianza kuona vitu nilivyokuwa sivi...