Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya kuvunja umasikini

‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

‎Soma Dakika 15 Kila Siku: Njia Rahisi Ya Kuvunja Umasikini Na Kujenga Utajiri...

 ‎Rafiki Yangu... ‎ ‎Unalala na simu mkononi. ‎Unamka na WhatsApp, Insta, na bet. ‎Hujawahi kukaa chini usome dakika 15 hata siku moja. ‎ ‎Na bado unajiuliza, “Mbona maisha hayaendi?” ‎Sasa sikia… ‎ ‎Watu wengi wanadhani utajiri unatokana na bahati. ‎Au kuwa na baba tajiri. ‎Au kufungua biashara kubwa ghafla. ‎ ‎Hawajui siri moja ya ajabu: ‎Dakika 15 tu za kusoma kila siku zinaweza kubadili kila kitu. ‎ ‎Sio lazima usome vitabu vigumu kama vya sayansi. ‎La hasha. ‎Unaweza kusoma kuhusu pesa, biashara, akili, au tabia za mafanikio. ‎ ‎Ni kama kuchoma mafuta polepole lakini mwisho gari linafika mbali sana. ‎ ‎Lakini unajua kinachoumiza zaidi? ‎Watu wanaosema “mimi sibadiliki kwa kusoma!” ‎Wanasema hivyo wakiwa broke. ‎Wakiwa wamechoka na maisha. ‎Wakilia usiku, wakicheka mchana. ‎ ‎Wanataka pesa, heshima, uhuru… ‎Lakini hawako tayari kusoma hata ukurasa mmoja kwa siku. ‎ ‎Wanakataa kusoma lakini wanakubali kuumia. ‎Wanachoka kusubiri neema ya ghafla, wakati wenyewe wamekata neema ya ...