Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya vitabu vya mabadiliko

Siri Za Hadithi Za Mauzo...

 *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Rafiki Yangu, Wauzaji wengi wanahangaika kuandika matangazo yanayouza. Wanaandika, lakini hakuna anayeona, hakuna anayeuliza, hakuna anaye nunua. Ni maumivu makali kuona mtu mwingine anauza bidhaa kama yako, Lakini wewe unabaki unalalamika *soko ni gumu.* Kitabu *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Kinakuonyesha namna ya kuandika hadithi zinazogusa mioyo, zinazoeleza, zinasisimua, na hatimaye zinauza. Utajifunza kuandika maandiko yanayovutia macho, yanayobeba hisia, na yanayobadilisha wasomaji kuwa wanunuzi. Pata nakala yako leo. Kwa kuwasiliana na 0755376891. PS; Anza kuandika hadithi zinazouza badala ya maneno yasiyoleta matokeo.

‎🔥 Nilikuwa Sina Dira... Mpaka Kitabu Kimoja Kilivyonibadilisha...

  ‎ ‎Siku zote nilikuwa mtu wa kawaida tu. ‎Ninaamka asubuhi, nakwenda kazini, narudi jioni nikiwa nimechoka. ‎ ‎Mishahara ni ileile, ndoto zipo tu kichwani lakini hakuna kinachoenda mbele. ‎ ‎Nilihisi maisha hayaendi… lakini pia sikuamini sana mambo ya vitabu. ‎ ‎Nikajipa moyo: “Hivi kweli mtu anaweza kufanikiwa kwa kusoma tu?” ‎ ‎Siku moja nikiwa kwenye daladala, nikasikia kijana mmoja akimwambia mwenzake: ‎ ‎"Mimi sikuchaguliwa chuoni, lakini kitabu kimoja kilinifunulia njia. ‎ ‎Sasa nauza online na nimefungua biashara yangu." ‎ ‎Maneno yale yalinigusa kama mshale. ‎ ‎Je, nami naweza kubadilika kupitia kusoma? ‎ ‎Nilijitetea: ‎"Aah! Mbona wengi wanasoma hawafanikiwi? Wengine wanamaliza PhD lakini bado ni masikini." ‎ ‎Nikajifariji kwa kisingizio cha muda na pesa. ‎Lakini moyoni nilihisi sauti ikiniambia: "Jaribu. Hata kama ni mara moja." ‎ ‎ ‎Nikamfuata rafiki yangu mmoja, ambaye nilimjua ana maendeleo m...

Kwanini Wanaosoma Vitabu Huonekana Wasomi Zaidi? Siri Ambayo Wengi Hawajui! ‎

Hii Ndio Sababu Halisi Wengi Hawaijui! ‎ ‎Rafiki Yangu, ‎ ‎Unakutana na mtu hajavaa suti. Hana lafudhi ya kizungu. ‎Lakini ukiongea naye, anakuvutia. Anakuonesha dunia kwa maneno. ‎ ‎Unajiuliza, “Huyu kazitoa wapi hizi akili?” ‎Jibu ni rahisi anasoma vitabu. ‎ ‎Vitabu sio tu karatasi na maneno. Ni bunduki ya akili. ‎Ukivisoma, unajifunza kuongea kama mtaalam. ‎Unajua kuandika vizuri, kufikiri kwa undani, na kuelewa haraka mambo ambayo wengine bado wanashangaa. ‎ ‎Sasa angalia watu ambao hawasomi. ‎Wanaongea kama watu wa mitandaoni. ‎Wanaishi kwa maneno ya "nilisikia", "walisema", na "inavyoonekana". ‎ ‎Hawana msimamo. ‎Hawajui kwa nini wanafanya wanachofanya. ‎Wanadanganywa kirahisi. ‎ ‎Kila kitu kwao ni “trend”, si truth. ‎Na ukikaa nao, unahisi unarudi nyuma kimaendeleo. ‎ ‎Unadhani kusoma ni kazi ya shule? ‎Ama ni kwa watu waliopata division one? ‎ ‎Umeambiwa uache vitabu usije ukaonekana "unaringa"? ‎Huo ni uongo mkubwa kuliko ahadi za wanasi...