Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya maarifa ya maisha

Siri Za Hadithi Za Mauzo...

 *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Rafiki Yangu, Wauzaji wengi wanahangaika kuandika matangazo yanayouza. Wanaandika, lakini hakuna anayeona, hakuna anayeuliza, hakuna anaye nunua. Ni maumivu makali kuona mtu mwingine anauza bidhaa kama yako, Lakini wewe unabaki unalalamika *soko ni gumu.* Kitabu *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Kinakuonyesha namna ya kuandika hadithi zinazogusa mioyo, zinazoeleza, zinasisimua, na hatimaye zinauza. Utajifunza kuandika maandiko yanayovutia macho, yanayobeba hisia, na yanayobadilisha wasomaji kuwa wanunuzi. Pata nakala yako leo. Kwa kuwasiliana na 0755376891. PS; Anza kuandika hadithi zinazouza badala ya maneno yasiyoleta matokeo.

‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

Kwanini Wanaosoma Vitabu Huonekana Wasomi Zaidi? Siri Ambayo Wengi Hawajui! ‎

Hii Ndio Sababu Halisi Wengi Hawaijui! ‎ ‎Rafiki Yangu, ‎ ‎Unakutana na mtu hajavaa suti. Hana lafudhi ya kizungu. ‎Lakini ukiongea naye, anakuvutia. Anakuonesha dunia kwa maneno. ‎ ‎Unajiuliza, “Huyu kazitoa wapi hizi akili?” ‎Jibu ni rahisi anasoma vitabu. ‎ ‎Vitabu sio tu karatasi na maneno. Ni bunduki ya akili. ‎Ukivisoma, unajifunza kuongea kama mtaalam. ‎Unajua kuandika vizuri, kufikiri kwa undani, na kuelewa haraka mambo ambayo wengine bado wanashangaa. ‎ ‎Sasa angalia watu ambao hawasomi. ‎Wanaongea kama watu wa mitandaoni. ‎Wanaishi kwa maneno ya "nilisikia", "walisema", na "inavyoonekana". ‎ ‎Hawana msimamo. ‎Hawajui kwa nini wanafanya wanachofanya. ‎Wanadanganywa kirahisi. ‎ ‎Kila kitu kwao ni “trend”, si truth. ‎Na ukikaa nao, unahisi unarudi nyuma kimaendeleo. ‎ ‎Unadhani kusoma ni kazi ya shule? ‎Ama ni kwa watu waliopata division one? ‎ ‎Umeambiwa uache vitabu usije ukaonekana "unaringa"? ‎Huo ni uongo mkubwa kuliko ahadi za wanasi...