‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

‎Jinsi Kusoma Vitabu Kunavyobadilisha Ubongo Wako....

 

‎Rafiki Yangu,

‎Miaka michache iliyopita, nilikuwa mtu wa kawaida sana.
‎Nilikuwa na ndoto kubwa… lakini akili iliyochoka.
‎Kichwa kilijaa mazungumzo ya watu, si ndoto zangu.
‎Nilikuwa nikiamka asubuhi nikijiuliza, “Hivi akili yangu inafanya kazi kwa asilimia ngapi tu?”

‎Sikujua kuwa kitu kimoja kidogo kingeweza kubadilisha kabisa maisha yangu.

‎Siku moja, nikiwa napitia changamoto za maisha, nilikutana na kitabu kidogo cha kurasa 120.
‎Jina lake lilikuwa ni "Change Your Thinking Change Your Life”

‎Kwa dharau nikasema, “Kitabu gani hiki? Kitatofautisha nini?”
‎Lakini kuna sauti ndani yangu ilisema:
‎“Jaribu. Una nini cha kupoteza?”

‎Nilikubali… Nikaanza kusoma.

‎Mwanzo kilikuwa kigumu. Ubongo wangu ulitaka kuachana nacho.
‎Nilikuwa nimezoea starehe, sio maarifa.
‎Nilikuwa mwepesi wa kuangalia video, sio kusoma kurasa.

‎Lakini kwa namna ya ajabu  kila ukurasa niliomaliza, akili yangu iliongezeka nguvu.
‎Nilianza kuona vitu nilivyokuwa sivioni.
‎Nilianza kufikiri kwa undani, kuelewa kwa haraka, na kuhoji kwa busara.

‎Baada ya vitabu 10, nilikuwa tofauti kabisa.
‎Nilielewa jinsi ubongo wangu unavyofanya kazi.
‎Nilijua kwa nini nilikuwa nikichelewa kufanya maamuzi.
‎Nilijua kwa nini nilikuwa nikiahirisha mambo muhimu.

‎Vitabu ni kama “chakula cha akili” kila ukurasa ulijenga misuli ya kufikiri.
‎Uwezo wangu wa kuelewa, kupambanua mambo, na kutatua matatizo uliongezeka mara mbili… mara tatu!

‎Leo hii, mimi ndiye watu wanamgeukia kushauriwa.
‎Mimi ndiye ninaleta suluhisho mezani.
‎Mimi ndiye ninayeandika, ninayeongoza, ninayefikiri kwa kina.

‎Na nilichogundua ni hiki:
‎👉 “Ubongo wako ni kama misuli. Ukiusomesha, unakuwa shujaa.”
‎👉 “Kitabu ni kama kocha wa ndani. Kinazungumza na akili yako kimya kimya lakini kwa sauti yenye nguvu isiyofutika.”

‎Kama unahisi una uwezo mkubwa lakini haueleweki…
‎Kama kila siku unahisi unajichanganya, unakosa dira, au unafanya maamuzi mabaya…
‎Basi usisubiri hadi maisha yakufundishe kwa maumivu.

‎🧠 Anza leo.
‎Chukua kitabu.
‎Soma kila siku hata kurasa mbili.
‎Ubongo wako utakushukuru kwa miaka kumi ijayo.

‎💡 Kwa sababu: “Tofauti kati ya kichwa kinachojua na kisichojua…
‎ni kurasa chache tu zilizosomewa kwa makini.”

‎📘 Safari ya ubongo wako inaanza kwa kitabu kimoja tu.
‎Je, uko tayari kuwa shujaa wa akili yako?

‎Anyway, Kama Unataka Kupata Vitabu Vizuri, Piga Simu 0750376891,

‎Karibu.
‎Imetoka Kwa Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,
‎Mkufunzi Ramadhan.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?