‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

‎Kwa Nini Unaacha Kusoma Kitabu Kwenye Ukurasa wa 17? Hii Ndio Sababu Halisi (Na Inashangaza!)

Kwa Nini Ni Vigumu Kusoma Vitabu Mpaka Mwisho?

‎Kuna jamaa mmoja...

‎Anaitwa Musa Mfalme.

‎Sio mfalme kweli, lakini akili zake zilikuwa na hazina ya kifalme.

‎Alikuwa na ndoto kubwa sana.

‎Alitaka kuwa tajiri.

‎Mwenye maarifa.

‎Awe mtu wa tofauti.

‎Siku moja akapata kitabu.

‎Kikubwa.

‎Kimeandikwa kwa rangi ya dhahabu.

‎Juu yake kimeandikwa,

‎“Nguvu Ya Maarifa: Jinsi Ya Kujenga Maisha Yako Kuanzia Sasa.”

‎Akasema,

‎"Hili ndilo lililokuwa linanikimbia. Leo naanza, mpaka mwisho!"

‎Akasoma ukurasa wa kwanza.

‎Ukurasa wa pili.

‎Wa tatu...

‎Kichwa kinamwambia, “Bora uangalie TikTok kidogo tu…”

‎Akachukua simu.

‎Dakika mbili.

‎Zikawa saa moja.

‎Akasema,

‎"Kesho nitaendelea kusoma."

‎Hakurudi tena kwenye kile kitabu.

‎Mpaka leo.

‎Lakini Kwa Nini? Kwa Nini Tunashindwa Kumaliza Vitabu?

‎Hii hapa safari ya ukweli...

‎Safari ambayo Musa Mfalme alipitia na labda na wewe pia.

‎1. Vitabu Vinataka Nguvu Ya Ndani

‎Kusoma si kama kuangalia movie.

‎Hakuna kelele. Hakuna mwanga.

‎Ni wewe na kurasa.

‎Na mara nyingi, akili yako inasema:

‎"Hii kazi ni nzito. Hebu tupumzike kidogo."

‎2. Dunia Inapiga Kelele Sana

‎Simu inaita.

‎Meseji zinagonga.

‎Meme zimejaa.

‎Unapokaa kusoma, unashindana na kelele za dunia.

‎Unashindwa.

‎3. Hakuna Muundo Wako

‎Unakaa tu.

‎Bila ratiba.

‎Bila mfumo.

‎Bila hata lengo.

‎Kusoma bila direction ni kama kuendesha gari bila destination.

‎4. Unataka Haraka Sana

‎Unataka usome leo, ufanikiwe kesho.

‎Ukikuta ukurasa wa kwanza hauna “motisha,” unachoka.

‎Hujui kuwa maarifa yanachimbwa taratibu kama dhahabu.

‎5. Ulikosea Kitabu

‎Unasoma kile ambacho hakikuhusu.

‎Kitabu cha “Accounting for Engineers”

‎Na wewe hata calculator huna.

‎Lakini Musa Mfalme Alibadilika...

‎Siku moja alipokutana na mimi.

‎Nikamwambia,

‎"Soma kurasa mbili tu kila siku. Si zaidi. Si chini. Ila kila siku."

‎Musa akaanza.

‎Siku ya kwanza: kurasa mbili.

‎Siku ya pili: mbili.

‎Wiki moja: anasoma tano kwa siku.

‎Mwezi mmoja: amemaliza kitabu chake cha kwanza.

‎Hiyo ilibadilisha kila kitu.

‎Somo la Leo: Si Lazima Usome Saa Mbili… Anza Na Dakika Kumi Tu.

‎Hakikisha una ratiba.

‎Chagua vitabu vinavyogusa maisha yako.

‎Zima usumbufu wote kabla ya kusoma.

‎Na kumbuka: Ukianza na kurasa mbili kila siku, ndani ya mwaka utakuwa na kichwa kama cha Profesa.

‎Kama uliwahi kuanza kusoma kitabu ukakishia ukurasa wa 17...

‎Uko peke yako?

‎Hapana.

‎Karibu kwenye kundi la Musa Mfalme.

‎Lakini sasa, unaweza kutoka humo.

‎Anza leo. Kurasa mbili tu.

‎Usijidanganye tena.

‎Vitabu ni silaha. Ukizitumia, unashinda vita ya maisha.

‎Je, Wewe Ni Kama Musa Mfalme?

‎Niandikie kwenye comment.

‎Ama share hii makala na rafiki ambaye kila mara anasema:

‎"Mwaka huu nasoma vitabu kumi!"

‎Halafu hata kimoja hajamaliza.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

‎0750376891.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?