Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Pesa Umasikini Mafanikio Elimu ya fedha Biashara Ramadhan Amir Hadithi ya kweli Motisha

‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

Kwa Nini Watu Wanakosa Pesa Ingawa Wanajituma?

‎Kakaa/Dadaa… ‎ ‎Umeshawahi kulala ukiwa umechoka sana, ‎ ‎Lakini bado huna hata shilingi mfukoni? ‎ ‎Umeamka mapema, ‎ ‎Ukapambana jua hadi linazama, ‎ ‎Ukavumilia kelele za mabosi, ‎Ukavumilia njaa kwa matumaini. ‎ ‎Lakini mwisho wa mwezi, ‎unahesabu senti. ‎ ‎Unaambiwa: *Jitume zaidi.* ‎Lakini unaumia moyoni, ‎kwa sababu umeshajituma mpaka unaungua ndani. ‎ ‎Kama hii ni hali yako, ‎najua uchungu unaoupitia. ‎ ‎Ni kama mbio zisizo na mwisho. ‎ ‎Unakimbia, lakini huoni mbele. ‎ ‎Unapiga hatua, lakini ni kama umerudi nyuma. ‎ ‎Wengine wanakucheka. ‎Wanasema huna akili ya pesa. ‎Lakini hawajui mateso yako. ‎ ‎Sasa sikiliza kwa makini... ‎ ‎Kazi ngumu pekee haitoshi. ‎Inauma kusema, lakini ni kweli. ‎ ‎Watu wengi wanaishia kuishi maisha ya mateso, ‎si kwa sababu hawajitumi, ‎bali kwa sababu hawajui cha kufanya na wanachopata. ‎ ‎Wanatumia kila walichonacho. ‎Hakuna mpango. ‎Hakuna akiba. ‎Hakuna uwekezaji. ‎Hakuna ndoto inayoelekea kutimia. ‎ ‎Na hapo ndipo ndoto nyingi hufia. ‎Ndipo ndo...