Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya mabadiliko ya maisha

Siri Za Hadithi Za Mauzo...

 *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Rafiki Yangu, Wauzaji wengi wanahangaika kuandika matangazo yanayouza. Wanaandika, lakini hakuna anayeona, hakuna anayeuliza, hakuna anaye nunua. Ni maumivu makali kuona mtu mwingine anauza bidhaa kama yako, Lakini wewe unabaki unalalamika *soko ni gumu.* Kitabu *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Kinakuonyesha namna ya kuandika hadithi zinazogusa mioyo, zinazoeleza, zinasisimua, na hatimaye zinauza. Utajifunza kuandika maandiko yanayovutia macho, yanayobeba hisia, na yanayobadilisha wasomaji kuwa wanunuzi. Pata nakala yako leo. Kwa kuwasiliana na 0755376891. PS; Anza kuandika hadithi zinazouza badala ya maneno yasiyoleta matokeo.

Mtoto Wa Mchuuzi Aliyejijengea Ujasiri Kwa Kurasa...

 ‎Kijiji cha Msaranga kilijulikana kwa soko lake dogo lenye kelele nyingi na vumbi la kila asubuhi.  ‎ ‎Hapo ndipo alipokulia Amani, kijana mdogo, mtoto wa mchuuzi wa viazi. ‎ ‎Maisha yalikuwa magumu.  ‎ ‎Kila siku ilianza kwa sauti ya mama yake akimwamsha mapema: ‎ ‎“Amani, chukua ndoo, twende sokoni.” ‎ ‎Amani alikuwa mpole, mwenye aibu na asiyejiamini.  ‎ ‎Kila alipokuwa karibu na watu wengi, sauti yake ilikuwa ndogo kama ya kupiga dua moyoni.  ‎ ‎Alipoitwa darasani ajibu swali, alitetemeka. Watu walimcheka. Alijiona dhaifu. Akijisemea moyoni, ‎ ‎"Mimi siwezi kuwa kama wale watoto wanaoongea mbele za watu. Mimi si kitu." ‎ ‎Siku moja, akiwa anafagia meza sokoni, aliona karatasi la gazeti limefungiwa samaki.  ‎ ‎Katika lile karatasi, kulikuwa na maneno yaliomvutia: ‎ ‎ “Vitabu vinawafanya watu kuwa huru.” ‎ ‎Alishangaa. Akajiuliza, “Inawezekanaje kurasa tu zabadili maisha ya mtu?”  ‎ ‎Hapo ndipo moyo wake mdogo ukapata hamu ya kujua zaidi. ‎ ‎Lakini ...

‎Unakufa Taratibu… Bila Hata Kujua Sababu? HUJISOMEI!

  ‎‎Unajua nini kaka/dada…  Kuna maumivu huwa hayapigi kelele. ‎Hayaleti presha. Hayajulikani fasta. ‎Yanakuja polepole… kimyakimya… mpaka siku moja unajikuta umepotea kabisa. ‎ ‎Na moja ya maumivu hayo ni… ‎Maisha Bila Kusoma Vitabu. ‎ ‎Soma hapa sasa: ‎Watu wengi wanaishi kama vile kusoma ni kwa ajili ya shule tu. ‎Au ni kitu cha wasomi. ‎Au ni “luxury” ya watu wanaotafuta PhD. ‎ ‎Lakini ukweli ni huu: ‎Maisha Bila Kusoma ni kama gari bila mafuta. ‎Unalipenda. Unalipiga mswaki kila asubuhi. ‎Lakini halisogei. ‎Linasimama pale pale, siku baada ya siku. ‎ ‎Umeshajiuliza kwanini maisha yako yamekuwa magumu hivi? ‎Kwanini kila mwaka una malengo… lakini hakuna kinachobadilika? ‎ ‎Kwanini wengine wanakimbia… na wewe unatembea? ‎Au hata kutambaa ni kazi? ‎ ‎Ni kama dunia inasonga mbele… lakini wewe umesahaulika. ‎Unajituma. Unahangaika. ‎Lakini bado maisha hayakusikilizi. ‎ ‎Na wakati wewe unapiga miayo ukiangalia TikTok… ‎wengine wanasoma makala, vitabu, kozi, wanajifunza skills… ...