Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya lugha ya kuuza

Siri Za Hadithi Za Mauzo...

 *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Rafiki Yangu, Wauzaji wengi wanahangaika kuandika matangazo yanayouza. Wanaandika, lakini hakuna anayeona, hakuna anayeuliza, hakuna anaye nunua. Ni maumivu makali kuona mtu mwingine anauza bidhaa kama yako, Lakini wewe unabaki unalalamika *soko ni gumu.* Kitabu *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Kinakuonyesha namna ya kuandika hadithi zinazogusa mioyo, zinazoeleza, zinasisimua, na hatimaye zinauza. Utajifunza kuandika maandiko yanayovutia macho, yanayobeba hisia, na yanayobadilisha wasomaji kuwa wanunuzi. Pata nakala yako leo. Kwa kuwasiliana na 0755376891. PS; Anza kuandika hadithi zinazouza badala ya maneno yasiyoleta matokeo.

‎ ‎🧨 Maneno Ya Kuuza vs Maneno Ya Kawaida Jifunze LUGHA YA MAUZO.

 ‎ Rafiki Yangu, ‎ ‎🛑 Acha tuanze na swali moja rahisi: ‎ ‎Ungependa mtu akusikie... ‎au akusikie na achukue hatua? ‎ ‎Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuongea tu, na kuongea hadi mtu avue viatu akimbie kununua kitu chako. ‎ ‎Karibu kwenye darasa la mtaa hapa unajifunza maneno ya kuuza, si maneno ya kupoteza muda. ‎ ‎🔥 1. Watu Wengi Wanakosea Hapa Hawajui Kuzungumza  LUGHA YA MTEJA ‎ ‎Wanauza kama wanaelezea. ‎Wanashawishi kama wanahubiri. ‎Wanatumia maneno ya kawaida kwenye kazi ya kuuza. ‎ ‎Mfano: ‎ ‎“Hii ni bidhaa bora sana.” ‎ ‎“Tuna huduma nzuri.” ‎ ‎“Karibu tukuhudumie.” ‎ ‎ ‎Yaani mtu anasikia, lakini hashtuki. Hakuna msisimko. Hakuna kichwa kumruka. ‎Matokeo yake? Wanapitwa tu na wanaojua kuchagua maneno sahihi. ‎ ‎ ‎💣 2. INAKERA! Unajua Kitu Chako Ni Kizuri, Lakini Watu HAWANUNUI! ‎ ‎Unajituma. ‎Unajua bidhaa yako ni ya maana. ‎Lakini ukiweka tangazo, ni kama umeandika barua ya maombi. ‎ ‎Ni kama vile unawaomba wanunue, badala ya kuwafanya watamani hadi wasilale. ‎ ...

‎Angalia Nguvu Ya Haya Maneno Matano (5) Yenye Kulevya – Maneno Yanayovutia Haraka Machoni.....

‎Rafiki Yangu Mpendwa, ‎ ‎Unajua shida kubwa ya wengi? ‎Wanaandika maneno ya kawaida mno. ‎Maneno yaliyokufa. ‎Hayana ladha. Hayagusi hisia. ‎Yanapitwa tu kama upepo. ‎ ‎Alafu wanashangaa... ‎Mbona hakuna anayesimama kusoma? ‎Mbona hakuna anayebonyeza? ‎ ‎Sasa leo nakuonyesha kitu kinono. ‎Maneno matano tu. ‎Lakini ni hatari. ‎Yana nguvu ya kuvuta macho ya mtu hata akiwa bize aje asome tu. ‎ ‎Hebu fikiria… ‎Umeweka post kali sana. ‎Unajua kabisa kuna madini. ‎Lakini hakuna mtu anaye-comment. ‎Hakuna likes. Hakuna saves. ‎ ‎Unakata tamaa. ‎Unaanza kufuta post zako. ‎Unaamini labda huwezi. ‎ ‎Unajua kwanini? ‎Ni kwa sababu kichwa cha habari yako kinapwaya. ‎ ‎Hakina mvuto. ‎Hakina “punch.” ‎Hakina kulevya. ‎ ‎Sikiliza kaka, dada... ‎Hili neno “karibu” ni zuri. ‎Lakini halina nguvu kama “karibu ujionee.” ‎Hili neno “soma” ni zuri. ‎ ‎Lakini halivutii kama “soma haraka kabla haijatolewa.” ‎ ‎Unashika pointi? ‎Lugha ya kuuza lazima iwe na mchele wa maneno ya moto. ‎Maneno ya kishindo. ‎Mane...