Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya vitabu vs audiobook

‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

Kuna Tofauti Gani Kati ya Kusoma Vitabu Halisi na Audiobooks?

 ‎📘 Sauti Iliongea Nami… Ndipo Nikagundua Nguvu Halisi ya Kusoma ‎ ‎Mimi nilikuwa msomaji wa kawaida sana. ‎Nilipenda vitabu… lakini muda wa kusoma? Hakuna! ‎ ‎Kazi nyingi, kichwa kiliniuma jioni, mara simu, mara familia. ‎Vitabu vinanivutia lakini kuvisoma ni kama kujilazimisha. ‎Nikaanza kujisikia kama nimechoka kuwa na ndoto zisizoendelezwa. ‎ ‎Siku moja rafiki yangu akaniambia: ‎"Kama kusoma kunakuchosha, kwanini usijaribu audiobook?" ‎Nilicheka tu. ‎ ‎"Kusikiliza si sawa na kusoma!" Nikasema kwa kejeli. ‎ ‎Nilihisi kama nikisikiliza kitabu, nitakuwa mvivu. ‎"Hakuna mtu aliyefanikiwa kwa kusikiliza tu... ni kama kudesa!" ‎Niliendelea kung’ang’ania vitabu vya karatasi, lakini vingi vikasalia na vumbi kabatini. ‎ ‎Siku moja nikiwa YouTube, nikamuona mtu mashuhuri akisema: ‎"Audiobooks zimenisaidia kusoma zaidi ya vitabu 50 kwa mwaka." ‎ ‎Nikaguswa. Nikasema: ‎"Subiri kidogo… Huyu amefanikiwa, na anasikiliza vitabu? Labda kuna jambo hapa....