‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

Utajiri Unaanza Na Dakika 15 Tu Kila Siku Na Hakuna Atakayekuanbia HILI!


‎‎Aliwahi kuwa maskini sana. Hakuwahi kumaliza hata kitabu kimoja maishani mwake.

‎Lakini siku moja, alijilazimisha kusoma dakika 15 tu kabla ya kulala.

‎Mwaka mmoja baadaye, alikuwa na biashara tatu, kipato cha kila siku, na uhuru aliokuwa akiuota.

‎Ni ajabu eeh?

‎Ndiyo.

‎Lakini si uchawi. Ni nguvu ya maarifa madogo kila siku.

‎Katika makala hii, nitakuonyesha jinsi dakika 15 tu za kusoma kila siku zinavyoweza kukutoa kwenye maisha ya kukopa hadi maisha ya kutajirika.

‎Nitakufundisha:

‎Nini cha kusoma

‎Jinsi ya kuanza

‎Na kwanini dakika 15 ni zaidi ya kutosha.

‎Fikiria maisha yako baada ya miezi 6:

‎Unaongea kwa ujasiri.

‎Unajua wapi pa kuwekeza.

‎Una wazo la biashara.

‎Unajua kutunza fedha zako.

‎Unajiamini zaidi.

‎Watu wanaanza kukuona tofauti.

‎Kila siku unakaribia mafanikio.

‎Na yote yalianza na kurasa chache tu kila jioni.

‎Watu maarufu kama Warren Buffett, Elon Musk, na Oprah Winfrey wamesema wazi “kusoma kila siku ndicho kilichowatengeneza.”

‎Buffett husoma kurasa 500 kila siku.

‎Lakini hakuanza hivyo.

‎Alianza kwa dakika chache.

‎Ndiyo maana leo anaendesha mabilioni ya dola.

‎Hata hapa nyumbani ,kuna vijana waliokuwa wamekata tamaa, lakini baada ya kuanza kusoma vitabu vya fedha, biashara na maendeleo binafsi maisha yao yalibadilika kama usiku na mchana.

‎Sasa hivi unaweza kusema: “Sina muda.”

‎Lakini ukweli ni huu: kila mtu ana dakika 15.

‎Badala ya kuperuzi mitandao bila mpango, geuza dakika hizo kuwa uwekezaji kwenye ubongo wako.

‎👉 Chagua kitabu kimoja tu kwa mwezi mfano: Nguvu Ya vitabu, Mwanafunzi wa Pesa, Rich Dad Poor Dad, au Think and Grow Rich.

‎👉 Soma kurasa 5 tu kila siku hata ukiwa umechoka.

‎👉 Chukua dondoo moja na uiweke kazini kesho.

‎Hakuna sharti umalize haraka muhimu ni kufanya kila siku.

‎Usiseme “Nitaanza kesho.”

‎Kesho huja na visingizio vipya.

‎Anza leo. Dakika 15 tu hakuna anayekuzuia isipokuwa wewe mwenyewe.

‎Chukua kitabu.

‎Soma kurasa chache.

‎Kesho rudia.

‎Mwezi ujao utaona tofauti.

‎Mwaka mmoja ujao utamshukuru sana “Wewe” wa leo.

‎Usitafute miujiza wewe ndiye muujiza.

‎Dakika 15 tu kila siku zinaweza kubadili jina lako kwenye orodha ya walalahoi hadi kwenye orodha ya wenye mafanikio.

‎Usikubali maisha yakupite bila wewe kuyatawala.

‎Dakika 15 Huo ndio mwanzo wa utajiri wako.

‎Anza leo.

‎Anyway, kama unataka vitabu vizuri basi piga simu 0750376891.

‎Karibu.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?