Mbinu 7 Za Kukumbuka Unachosoma Katika Vitabu Bila KUSAHAU TENA...
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Kakaa/Dadaa Yangu...
Unasoma kitabu leo…
Kesho haukumbuki hata ukurasa wa kwanza.
Ukiulizwa ulichojifunza, unazubaa kama umepigwa na butwaa.
Unajikuta unasoma tu ilimradi umalize, si kwa sababu unaelewa au utakumbuka.
Yani unatumia muda wako kusoma…
Unaweka akiba ya maneno kichwani…
Halafu akili inafuta kila kitu kama flash drive yenye virus!
Unasoma vitabu vingi, ila akili haina ushahidi wowote.
Inapoteza kumbukumbu kama ex wako aliyesahau yote mliyowahi kupitia.
Lakini mbona kuna wengine wakisoma, wanakumbuka hadi mistari ya mwisho?
Hii ndo pointi ya kukasirikia!
Sio kwamba Huna Akili.
Sio kwamba huna uwezo.
Ni mbinu tu unazotumia ndizo za kizamani.
Zile za kukariri bila kuelewa, au kusoma harakaharaka kama unakimbizana na deadline ya NECTA.
Zisahau. Hapa nakuletea mbinu mpya, za kisasa, na za uhakika.
Zikikupita, utabaki na kichwa kizito kisicho na content.
Twende sasa… Hizi ndizo MBINU 7 ZA KUKUMBUKA UNACHOSOMA:
MBINU YA KWANZA:
Soma kwa Sauti
Usione aibu, jifunze kuongea na kitabu chako.
Ukisoma kimya kimya, akili inaweza kuwa inasafiri.
Soma kwa sauti hata sauti ya chini.
Itakusaidia kusikia, kuelewa, na kukumbuka.
Ni kama kuongea na rafiki, unaelewa zaidi.
MBINU YA PILI:
Fanya Summary kwa Maneno Yako
Ukimaliza sehemu fulani, simama.
Jisomee upya, lakini kwa maneno yako mwenyewe.
Hii inasaidia ubongo kushughulika kuchuja kilicho muhimu.
Na utakumbuka kwa muda mrefu zaidi.
MBINU YA TATU:
Fundisha Mtu Mwingine.
Ukisoma na ukaweza kumfundisha mwingine, basi umekielewa kweli.
Mchukue kaka, dada, rafiki au hata mpenzi wako…
Mwambie ulichosoma kama vile wewe ndiye mwandishi.
Trust me utakumbuka hadi footnote!
MBINU YA NNE:
Chora au Andika Pointi Muhimu.
Ubongo unakumbuka picha kuliko mistari.
Tengeneza ramani ya akili (mindmap), chora mistari, andika kwa rangi tofauti.
Hii inaleta rangi kwenye kumbukumbu zako na inazishikilia vizuri.
MBINU YA TANO: Tumia Hisia.
Gusa hisia zako unapokutana na pointi kali.
Kama inakugusa moyo, simama.
Jiulize: “Hii inamaanisha nini kwangu?”
Unapohusisha hisia na kusoma, kumbukumbu hujikita kwenye moyo.
Na moyo hausahau kirahisi.
MBINU YA SITA:
Rudia Mara kwa Mara.
Usisome mara moja tu halafu usubiri miujiza?
Hapana, bro!
Rudia tena na tena.
Kila ukirudia, unakumbuka zaidi.
Repetition is the mother of mastery.
MBINU YA SABA:
Tumia Wakati Bora wa Ubongo.
Asubuhi au usiku kabla ya kulala…
Ubongo unakuwa fresh na tulivu.
Usisome ukiwa na njaa au umechoka—hakuna kitakachokaa kichwani.
Tafuta muda ambapo akili yako iko active.
Hapo ndipo uweke content ya nguvu.
Kuna dogo mmoja anaitwa Musa.
Alikuwa ana penda sana kusoma vitabu.
Lakini alikuwa na tabu moja hakumbuki chochote.
Alisoma kitabu cha “NGUVU YA VITABU”
Wiki moja baadaye, hakuwa anakumbuka hata jina la kitabu.
Nilimfundisha hizi mbinu saba…
Baada ya mwezi mmoja, aliweza kunielezea vitabu vitatu alivyomaliza.
Mistari, funzo, mfano, hadi methali alizikumbuka kama ni mistari ya nyimbo.
Leo anaitwa “Mwalimu Musa” mtaani kwake.
Na kazi yake ni kufundisha wengine kusoma na kukumbuka.
Sasa ni zamu yako.
Usiendelee kupoteza muda kusoma bila faida.
Tumia mbinu hizi.
Zimejaribiwa, zimeaminika.
Zinakufanya usome kwa raha, na kukumbuka kama kompyuta yenye RAM kubwa.
Kama umefika hapa…
Basi moyo wako una kiu ya mabadiliko.
Na hakika, huo ndio mwanzo wa akili mpya.
Uko tayari kukikumbuka kila kitabu utakachosoma?
Sema: “Leo ndo mwisho wa kusoma bila kuelewa!”
Kama Bado Hujajiunga na Group La Usomaji Wa Vitabu,
Piga Simu 0750376891.
Karibu.
Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni