‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

‎Faida 7 Za Kipekee Za Kusoma VITABU Kila Siku Hata Kama Ni DAKIKA 10 TU!

 ‎


‎Kakaa/Dadaa Yangu...

‎Watu wengi wanalalamika hawafanikiwi.

‎Wanajitahidi sana lakini hakuna hatua zozote wanazopiga.

‎Wengine kila siku wako online lakini akili zao ziko offline.

‎Kila mtu anatafuta "shortcut ya mafanikio", lakini wanakosa kitu kimoja cha msingi...

‎Kusoma vitabu.

‎Ndiyo, hata kama ni dakika 10 tu kwa siku, inaweza kubadilisha kila kitu.

‎Hebu fikiria…

‎Miaka mitano ijayo, utakuwa mtu yule yule tu, isipokuwa tu kwa vitu viwili:

‎Vitabu ulivyosoma, na watu ulioambatana nao.

‎Sasa kama kila siku unasoma status, memes na story za watu…

‎Lakini huwezi kusoma hata ukurasa mmoja wa kitabu, unajidhulumu mwenyewe.

‎Mafanikio hayaji kwa kuomba omba—yanakuja kwa maarifa.

‎Na maarifa yapo vitabuni.

‎Ukikwepa kusoma leo, utajikuta unakumbana na matatizo yale yale kesho.

‎Kuna watu wanasema, “Mimi siwezi kusoma vitabu.”

‎“Nachoka haraka.”

‎"Usomaji sio vitu vyangu."

‎Wanajikosea sana.

‎Hakuna mtu yeyote aliyezaliwa akijua kusoma.

‎Lakini kila mtu anaweza kujifunza kupenda kusoma.

‎Na usidanganywe…

‎Huwezi pata mafanikio ya kweli kwa kusikiliza tu motivational videos.

‎Au kwa kubrowse quotes kila siku.

‎Vitabu vinakupa undani.

‎Vitabu vinakuza akili.

‎Vitabu vinakufungua kichwa.

‎Dakika 10 tu kwa siku, zinaweza kukuokoa na miaka 10 ya mateso.

‎Sasa hebu niambie, unawezaje kufaidika na kusoma vitabu kila siku?

‎Hii hapa orodha ya faida 7 zinazokukodolea macho:

‎1. Unakua Mwerevu Zaidi.

‎Unajua mambo mengi kuliko watu wa kawaida.

‎Unakuwa na hoja nzito. Unatisha kimawazo.

‎2. Unajiamini Sana.

‎Unapokuwa na maarifa, huogopi kusema.

‎Huogopi changamoto. Unasimama imara.

‎3. Mawazo Yako Yanakuwa Safi.

‎Vitabu vinasaidia akili yako kuwa tulivu.

‎Vinapunguza stress na msongamano wa mawazo.

‎4. Unaongeza Kumbukumbu na Umakini.

‎Kusoma ni kama kuufanyisha mazoezi ubongo.

‎Kadri unavyosoma, ndivyo unavyoimarika kiakili.

‎5. Unapata Mawazo Mapya Ya Biashara, Maisha na Mafanikio.

‎Kuna watu walifaulu kabla yako.

‎Waliandika walichojifunza.

‎Unapovisoma vitabu vyao unafupisha njia.

‎6. Lugha Yako Inaimarika.

‎Unaanza kuongea vizuri.

‎Kuandika vizuri. 

‎Kujieleza kwa ufasaha.

‎7. Unajitambua Zaidi.

‎Vitabu vinaangaza ndani yako.

‎Vinakufundisha kuhusu wewe mwenyewe.

‎Namkumbuka kaka mmoja mtaa wa Keko – anaitwa Ally.

‎Huyu jamaa aliwahi kuwa mchoma chips.

‎Lakini leo hii ni mtaalamu wa mitandao na ana biashara yake.

‎Niliuliza siri yake, akaniambia kitu kimoja:

‎“Niliamua kusoma kitabu kimoja kila mwezi. Hata kama ni ukurasa mmoja kwa siku.”

‎Kila kitu kilianza kubadilika.

‎Akili yake ikafunguka.

‎Akaanza kufikiri tofauti.

‎Leo hii, anawashauri wafanyabiashara wakubwa.

‎Si kwa sababu ya pesa aliyokuwa nayo bali maarifa aliyoyachota kwenye vitabu.

‎Sasa ni zamu yako.

‎Usisubiri kuwa na muda mwingi.

‎Anza na dakika 10 tu kwa siku.

‎Soma kabla ya kulala.

‎Soma ukiwa kwenye daladala.

‎Soma wakati wengine wanabishana kwenye comments.

‎Kumbuka:

‎Kila ukurasa unaosoma ni hatua moja karibu na ndoto zako.

‎Kama unahitaji vitabu bora vya kuanzia, niambie nitakushauri vizuri.

‎Andika Meseji *NATAKA VITABU*

‎Kwenda 0750376891.

‎Usikubali maisha yakutese kwa sababu hujachukua dakika 10 ya kujisomea.

‎Weka comment yako hapo chini…

‎ Umesoma kitabu gani mwezi huu?

‎Twende kazi!

‎Karibu.

‎0750376891.

‎Mkufunzi Ramadhan Amir

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?