🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥
Kakaa/Dadaa Yangu....
Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen?
Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?*
Basi sikia hii...
Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia.
Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion.
Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea.
Lakini...
Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku.
Unaitwa: Hero’s Journey.
Ni mfumo wa hadithi ya shujaa.
Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda.
Kama Simba kwenye Lion King.
Kama Neo kwenye Matrix.
Kama wewe kwenye maisha yako.
Sasa tatizo ni hili...
Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia.
Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni.
Wanakosa story.
Na bila story,hakuna connection.
Unasema bidhaa yako ni bora? So what?
Wateja wanataka kujihisi wao ni mashujaa kwenye maisha yao.
Na kama hujawafanyia hivyo…
Utakula rejection mpaka uanze kujishuku.
Usijidanganye kuwa unahitaji maneno mengi, au Kiingereza cha kuvunja shingo.
Hii siyo habari ya vocabulary.
Ni habari ya mfumo.
Na huu mfumo ni silaha ya mawasiliano yenye uzito.
Hero’s Journey inatoka kwa Joseph Campbell.
Ni chombo kilichotumika kuunda filamu karibu zote kubwa duniani.
Wengine wanajaribu kuuza kwa ‘features na benefits.’
Lakini watu hawanunui features.
Wanunua safari ya kihisia.
Sasa, chukua karatasi na kalamu.
Andika hadithi ya mteja wako kama shujaa.
Hii ndiyo ramani ya Hero’s Journey (kwa lugha ya mtaa):
1. 👉 Anayeanza safari (Mteja wa kawaida, ana shida)
2. 👉 Anaona ishara (Anasikia kuhusu suluhisho lako)
3. 👉 Anasita (Anaogopa kujaribu, haelewi kama itawezekana)
4. 👉 Anakutana na kocha/mshauri (Wewe)
5. 👉 Anaamua kujaribu (Ananunua, anaanza kutumia)
6. 👉 Anapambana na vikwazo
7. 👉 Anakaribia kushindwa
8. 👉 Anasimama tena
9. 👉 Anashinda vita
10. 👉 Anarudi kama shujaa mpya (Amebadilika. Ana furaha. Ana matokeo.)
Ukijua kutumia hii formula unaweza kuuza kitu chochote.
Ngoja nikupe mfano halisi.
Kuna kijana mmoja anaitwa John.
Alikuwa hana chochote.
Maskini wa kutupa.
Alikuwa anaishi kwa bibi yake, hana ajira, hana kipato.
Lakini alianza kusoma kitabu cha Nguvu Ya Buku.
Alianza kuweka buku tu kila siku.
Alianza na mtaji wa elfu tano tu kuuza maandazi.
Alipambana. Alikataliwa. Alichekwa.
Lakini hakuacha.
Akasoma tena. Akarekebisha. Akakutana na changamoto, lakini hakuacha.
Leo hii, ana duka lake. Ana wasaidizi. Ana amani kichwani.
Kwa sababu ya hatua ya shujaa aliyochukua.
Yaani mtu wa kawaida, amegeuka kuwa shujaa wa familia yake.
Hadithi zinauza kwa sababu watu wanajiona ndani yake.
Wanaona maumivu yao.
Wanaona tumaini.
Wanaona matokeo.
Ukijua kutumia Hero’s Journey, utaandika matangazo yanayogusa roho.
Utaandika post ambazo zina comments “Bro umeandika kuhusu mimi kabisa!”
Utaandika hadithi ambazo zinawasha moto wa kununua.
🔥 Basi ni muda wako sasa kuwa mwandishi wa hadithi za mashujaa.
👉 Wauzie watu safari, si bidhaa.
👉 Waonyeshe kuwa wewe ni mwongoza safari, si muuza tu.
Na ukitaka kujifunza jinsi ya kutumia Hero’s Journey kwenye biashara yako,
Meseji moja tu inatosha!
Tuma Neno *Hadithi* Kwenda 0750376891.
Karibu.
Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,
Mkufunzi Ramadhan Amir.
0750376891.
Maoni
Chapisha Maoni