Rich Dad vs Poor Dad: Je, Baba Maskini Anaweza Kukufundisha Siri za Utajiri?
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Rafiki Yangu....
Nilivyokuwa mdogo, nilijua pesa huja kwa bidii.
Lazima uamke mapema, ufanye kazi kwa juhudi, utii maagizo ya bosi wako, na usikose kazini hata siku moja.
Niliona wazazi wangu wakitoka alfajiri, wakirudi jioni wakiwa wamechoka, lakini wakiwa maskini vilevile.
Nikajua labda maisha ndivyo yalivyo.
Mpaka nilipokutana na Rich Dad Poor Dad.
Ndiyo siku maisha yangu yalibadilika.
Katika makala hii, nitakuonyesha:
Jinsi kitabu cha Rich Dad Poor Dad kinavyochambua siri za pesa.
Ni kwa nini watu wengi wanapambana maisha yao yote lakini hawajawahi kujua *kanuni ya utajiri.*
Na kwa nini kusoma kitabu hiki ni hatua ya kwanza kuelekea uhuru wa kifedha.
Fikiria maisha bila presha ya bili kila mwisho wa mwezi.
Fikiria kuwa na uhuru wa kuchagua unachotaka kufanya si kwa sababu ya mshahara, bali kwa sababu unapenda.
Kuwa na biashara zako, uwekezaji unaoleta pesa hata ukiwa umelala.
Kuwa na muda na familia yako, kwenda likizo unapotaka, si unapopewa ruhusa.
Ndiyo maisha Rich Dad alifundisha.
Na unaweza kuyapata.
Robert Kiyosaki mwenyewe alikulia katika familia ya kawaida.
Aliona baba yake mzazi (Poor Dad) akifundisha, akijituma, lakini akibaki maskini.
Lakini alipopata mentor (Rich Dad), mwenye mtazamo tofauti kuhusu pesa ndipo akaanza kuelewa tofauti ya watu matajiri na watu maskini:
Si bidii ya kazi tu, bali ni aina ya elimu unayoipata kuhusu pesa.
Leo hii, mamilioni ya watu duniani wamesoma kitabu hiki, wamebadilisha fikra zao, na maisha yao pia yakabadilika.
Kitabu hiki kinakuonyesha mambo manne ya msingi:
1. Maskini hufanya kazi kwa pesa. Matajiri hufanya pesa iwafanyie kazi.
2. Maskini huamini elimu ya darasani tu. Matajiri huwekeza kwenye elimu ya kifedha.
3. Maskini hununua mali zinazowapotezea pesa. Matajiri hununua mali zinazowaingizia pesa.
4. Maskini huwa waoga kujaribu. Matajiri hujifunza kwa kufanya makosa.
Kitabu hiki hakikufundishi kupenda pesa, kinakufundisha kuielewa.
Kujua mtiririko wake.
Kujua njia zake.
Na jinsi ya kuitumia kukujengea uhuru.
Kama unaendelea kufanya kazi tu bila kuelewa pesa, utaitumikia maisha yako yote.
Kama hutabadili fikra zako kuhusu pesa, maisha hayatabadilika.
Lakini habari njema ni hii:
Unaweza kuanza leo.
Kwa kusoma kitabu cha Rich Dad Poor Dad.
Hiki si kitabu cha kawaida ni ramani ya kutoka kwenye mtego wa maisha ya mkopo, madeni, na mshahara wa mwezi.
Watu wanaofanikiwa si wa kipekee wana maarifa tofauti tu.
Usiishi maisha yote ukiwa umefungwa na fikra za *Baba Maskini.*
Wekeza kwenye akili yako leo.
Pata nakala yako ya Rich Dad Poor Dad.
Kwa kupiga simu Kwenda 0750376891.
Kisome. Kielewe. Kitumie.
Halafu kaa pembeni, uangalie jinsi maisha yako yanavyoanza kubadilika kidogo kidogo, hadi uwe huru kabisa.
Kosa si kuwa maskini kosa ni kubaki hivyo baada ya kupata maarifa.”
Na maarifa yako hapa mkononi.
Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,
Mkufunzi Ramadhan Amir.
0750376891.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni