Jinsi Ya Kuwashinda Washindani Bila Kuwataja Bila Vita, Bila Kelele.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
*Wanazidi Kujitangaza, Wewe Watangulie Kimya Kimya*
Kakaa/Dadaa Yangu....
Unajua shida kubwa ya watu wengi?
Ni kufikiria ushindani ni vita.
Kila mtu anataka kupiga kelele, kutaja majina, kushusha wengine ili aonekane juu.
Lakini ukweli ni huu...
Watu hawapendi kelele.
Wanapenda thamani. Wanapenda kuaminika.
Na mtaa hausahau ukitoa kitu cha maana, kimya kimya.
Unataka ushinde sokoni?
Usipige kelele.
Toa tofauti.
Lakini sasa ona...
Wao kila siku wanapost.
Wanapiga picha na wateja.
Wanapiga video za “success.”
Wanasema wao ndio namba moja.
Na wewe unaanza kuwaza:
"Nikikaa kimya, nani atanijua?"
"Wateja watawafuata wao, si mimi?"
Mbaya zaidi, wengine wanaanza kukudharau.
Wanakuuliza, “We bado upo?”
Inaumaaa…
Sasa sikiliza kaka/dada...
Kelele hazijengi heshima.
Kelele hazijengi chapa.
Na kelele hazileti pesa ya kweli.
Ukweli ni huu:
Mteja hataki kujua nani mkubwa zaidi.
Anataka kujua ni nani atamsaidia haraka na kwa uhakika.
Soko lina akili.
Wateja wanaona.
Ukiwa mnyoofu, mwenye thamani watafuata.
Bila kushindana. Bila kutaja yeyote.
Hii ndo njia ya kweli ya kuwashinda washindani bila kuwataja:
Weka nguvu kwenye bidhaa yako.
Weka roho kwenye huduma yako.
Weka moyo kwenye mawasiliano yako.
Toa thamani kiasi kwamba wateja wao waanze kuwaambia:
*Mbona yule mwingine yuko tofauti?*
Usihubiri.
Usisingizie.
Toa kitu hadi washindani waanze kujiuliza:
*Huyu anafanya nini hadi watu wamfuate hivi kimya?*
Namkumbuka jamaa mmoja Mbagala.
Alikuwa na duka la nguo.
Kila mtu mtaani alikuwa anampita.
Maana hakupiga promo, hakusema chochote online.
Lakini jamaa alikuwa na staili yake:
Kila mteja aliyekuja, alihudumiwa kama mfalme.
Alipendezesha duka lake kimya kimya.
Akajua jina la kila mteja wake.
Akajua nguo gani zinampendezea nani.
Leo hii...
Washindani wake wanampost.
Wanamsema bila kumtaja.
Maana wateja wao wanawaacha na kukimbilia kwake.
Siri yake ni moja:
Alijua kupika ladha isiyohitaji mbwembwe.
Chukua Hili Kama Funzo:
Wanaopiga kelele, huisha kelele zikiisha.
Wanaotoa thamani, hubaki mioyoni.
Toa kitu mpaka kimya chako kiishike mitaa.
Shinda bila kubishana.
Washinde kwa kazi, sio kwa mdomo.
Anyway, kama unataka huduma ya usimamizi wa karibu,
Tuma meseji *NATAKA HUDUMA YA UKOCHA*
Kwenda 0750376891.
Imetoka kwa Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,
Mkufunzi Ramadhan Amir.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni