‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

‎Hupendi Kusoma Vitabu? Hizi Njia 5 Zitakubadilisha Bila Kujua!.... ‎

 ‎Hebu niambie kaka/dada…

‎Ukitaja vitabu unahisi usingizi unakukamata?

‎Unajikuta unasema,

‎“Aaah mi si mtu wa vitabu bana, sina muda wala mood!”

‎Sawa.

‎Lakini je… umewahi kujiuliza,

‎Hii tabia ya kukwepa vitabu inakuumiza wapi?

‎Leo, nitaongea na moyo wako.

‎Sio kwa kukuhukumu.

‎Bali kwa kukupa mwanga wa kubadili maisha… bila stress.

‎Tatizo si wewe.

‎Tatizo ni mfumo ulivyokufundisha kusoma kama adhabu.

‎Ulipokuwa shule,

‎uliambiwa usome ili ufaulu mitihani.

‎Sio ili ufanikiwe kwenye maisha.

‎Hakuna aliyekuambia,

‎*Soma ili ujue namna ya kujiongezea kipato.*

‎*Soma ili ujue kujitetea kisheria.*

‎*Soma ili usilaghaiwe.*

‎Ndio maana sasa huoni maana ya kusoma.

‎Unahisi ni mambo ya watoto wa chuo tu.

‎Lakini ukweli ni huu:

‎Watu wote waliofanikiwa wanapata maarifa kupitia vitabu.

‎Ukitaka kujifunza siri ya pesa ipo kwenye kitabu.

‎Ukitaka kubadilisha mindset ipo kwenye kitabu.

‎Ukitaka kujua mbinu za biashara – ipo kwenye kitabu.

‎Na wewe bado unasema:

‎“Siwezi kusoma bana!”

‎Wakati huo huo, maisha yanakusukuma kila kona.

‎Umechoka na hali uliyonayo…

‎Lakini suluhisho linakutazama ukurasa wa kwanza tu.

‎Ukipita, unapata nuru.

‎Sasa sikiliza vizuri…

‎Sio lazima uwe msomi kuanza kusoma.

‎Sio lazima uanze na vitabu vikubwa kama Biblia.

‎Na wala huhitaji saa nzima.

‎Dakika 10 tu kwa siku zinatosha.

‎Na kama bado huna muda —

‎Una muda wa WhatsApp, TikTok, na Instagram.

‎Kwa hiyo muda upo, ni mindset tu haijawa tayari.

‎Halafu usianze na vitabu vya kuchosha.

‎Anza na kitu unachokipenda:

‎Biashara, mapenzi, mafanikio, pesa au hata stori.

‎Hebu chukua hizi njia 5 rahisi za kuanza kusoma hata kama huipendi:

‎1. Chagua vitabu vinavyokuhusu.

‎Usianze na “Thinking Fast and Slow.”

‎Anza na “Nguvu Ya Buku” au “Hadithi Za Mafanikio.”

‎2. Weka lengo dogo sana.

‎Usiseme "nitamaliza sura moja."

‎Sema, “Nitasoma paragraph moja tu leo.”

‎Ukianza hutaacha!

‎3. Soma muda ule ambao una amani.

‎Asubuhi kabla ya WhatsApp au usiku kabla ya kulala.

‎4. Tumia audiobook.

‎Unaweza kusikiliza vitabu ukiwa jikoni, gym au kwenye basi.

‎5. Shirikiana na mtu.

‎Pata mtu wa kukukumbusha au kusoma pamoja.

‎Hata mjadala wa mistari mitatu unaweza kukubadilisha.

‎Nakumbuka jamaa mmoja maeneo ya Temeke anaitwa Juma.

‎Alikuwa anasema:

‎“Mi sijawahi kupenda kitabu hata kidogo.”

‎Siku moja alikuta kazini kwao wanasoma kitabu fulani “Nguvu Ya Vitabu.”

‎Akajitahidi kusoma ukurasa wa kwanza.

‎Akashangaa kumbe kuna stori za mtaani mle ndani.

‎Akajikuta anamaliza sura tatu kwa siku moja!

‎Leo hii, Juma ana duka lake mwenyewe.

‎Anaandika bei na matangazo ya biashara yake kwa maneno ya kuvutia.

‎Na anasema:

‎“Kusoma kulinipa akili ya pesa ambayo shule haikunipa!”

‎Mwisho Kabisa?

‎Kama Juma aliweza, na wewe unaweza.

‎Anza kidogo, rudia mara nyingi,

‎Utaingia kwenye sayari mpya ya maarifa na mafanikio.

‎Usisubiri mpaka maisha yakulazimishe usome.

‎Anza leo, hata na mstari mmoja tu.

‎Anyway, kama unataka vitabu vizuri,

‎Piga Simu Kwenda 0750376891.

‎Karibu.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

‎0750376891

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?