‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

Hupendi Kusoma Vitabu? Hii Ndiyo Njia Rahisi Ya Kuanza Kusoma Na Kufanikiwa Maishani!


Jinsi Ya Kuanza Kusoma Vitabu Hata Kama Hupendi Kusoma.

‎Rafiki Yangu Mpendwa,

‎Kuna Jamaa mmoja aliwahi kuniambia kitu kilichonifanya nisahau hata njaa.

‎Akasema:

‎Mimi sihitaji kusoma vitabu. Si vipo YouTube na TikTok?

‎Mwaka mmoja baadaye...

‎Simu yake haikuwa na kifurushi.

‎Alichoka kuomba miamala ya 200 kwa mama wa kiosk.

‎Na maisha yake yalikuwa pale pale.

‎Mwishowe akanitext:

‎Bwana, tafadhali nipe jina la kile kitabu ulichonitumia. Naona sasa nahitaji kusoma…

‎Katika makala hii, utakutana na njia rahisi kabisa ya kuanza kusoma vitabu hata kama huwa hupendi kabisa kusoma.

‎Sitakuambia usome kurasa 100 kwa siku, hapana.

‎Nitakufundisha njia ya kuanza polepole, kwa ustadi, bila kuumiza kichwa.

‎Na zaidi ya yote, nitakueleza kwanini watu waliokuwa kama wewe sasa ni mamilionea.

‎Hebu vuta picha hii:

‎Unaamka asubuhi ukiwa na hamasa ya maisha.

‎Umejaa maarifa.

‎Umejua jinsi ya kutengeneza pesa.

‎Unajua kuzungumza vizuri mbele ya watu.

‎Unapendwa na watu kwa sababu ya hekima zako.

‎Na yote haya, si kwa sababu ulienda chuo .

‎Bali kwa sababu ya vitabu vitatu ulivyomaliza mwaka huu.

‎Mmoja ya vijana waliokuwa hawapendi kusoma, leo ni mmiliki wa biashara 3.

‎Alianza kwa kusoma kurasa 2 tu kwa siku.

‎Leo ananukuliwa kwenye redio, anafundisha wengine.

‎Mwingine alianza kusoma akiwa anauza chips.

‎Leo anamiliki duka la vitabu.

‎Na mshangao?

‎Wote walichukia kusoma mwanzoni… kama wewe.

‎Sasa, ngoja nikuonyeshe njia rahisi ya kuanza kusoma vitabu bila kuboreka:

‎✅ Usianze na vitabu vigumu.

‎Anza na kitabu ambacho kina hadithi. Kinachoburudisha. Kinachoeleweka haraka.

‎✅ Soma dakika 5 tu kwa siku.

‎Usijiambie *lazima nimalize sura.* Weka muda sio malengo ya kurasa.

‎✅ Soma mahali tulivu.

‎Usisome ukiwa kwenye foleni ya daladala au ukiangalia TV.

‎✅ Andika maneno matatu muhimu uliyojifunza.

‎Hii hukufanya kukumbuka zaidi na kuona thamani ya ulichosoma.

‎✅ Pata rafiki wa kusoma nae.

‎Mchangie alichojifunza. Jifunze kutoka kwake pia.

‎Ukweli ni huu:

‎Ukisubiri hadi siku utapenda kusoma haitafika.

‎Mafanikio hayaji kwa kubahatisha.

‎Yanaanza kwa maamuzi madogo.

‎Na uamuzi mmoja muhimu zaidi leo ni kuanza kusoma hata kurasa mbili.

‎Chukua kitabu kimoja leo.

‎Anza leo.

‎Sio kesho.

‎Sio wiki ijayo.

‎Leo.

‎Ukiendelea kukwepa vitabu, utabaki ukisubiria mafanikio ya watu wengine.

‎Lakini ukikubali kusoma, hata kidogo, utarusha maisha yako kiwango kingine.

‎Chagua leo:

‎Soma au endelea kusota.

‎Uamuzi ni wako.

‎Lakini kumbuka: kusoma ni njia fupi ya kufika mbali.

‎Anyway, Kama unataka vitabu vizuri,

‎Tuwasiliane Kwa Namba 0750376891.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali.

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?