‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?

 ‎



Kakaa/Dadaa...


Vinaweza Kubadilisha Yako Pia.

‎Ndiyo Leo.

‎Miaka kadhaa nyuma... nilikuwa na akili lakini maisha yalikuwa hayanisikii.

‎Nilikuwa najua mambo mengi, ila siyo yanayoweza kulipa bili.

‎Nilikuwa naenda kusoma vitabu vya shule tu, vitabu vyenye mistari mingi isiyoeleweka.

‎Vyenye theory nyingi lakini maisha yangu halisi hayabadiliki.

‎Unajua uchungu wa kujua sana lakini huna kitu?

‎Kila mtu anakuita mwerevu ila huna ata buku mfukoni?

‎Kila mtu anakusifia una akili ila huwezi kumsaidia hata mama yako elfu tano?

‎Ni kama una cheti cha kuogelea lakini unaishi jangwa.

‎Unajua kuelea, lakini hakuna maji!

‎Hapo ndo nilijua, kuna kitu kimekosewa.

‎Nilivyokaa chini nikagundua kitu kimoja.

‎Sio vitabu vyote vina uwezo wa kubadilisha maisha.

‎Kusoma tu hakutoshi—swali ni: unasoma nini?

‎Unapiga msuli wa vitabu vya lecture, wakati watu waliofanikiwa wanasoma vitabu vya pesa, mindset, ujasiriamali.

‎Vitabu vya kawaida vinakupa daraja la kupita kwenye mitihani.

‎Vitabu sahihi vinakupa daraja la kupita kwenye maisha.

‎Nilipoanza kusoma vitabu vya akina Robert Kiyosaki (Rich Dad Poor Dad),

‎ Brian Tracy (No Excuses!), Napoleon Hill (Think and Grow Rich), 

‎Jordan Belfort (Way of the Wolf)...

‎Maisha yalianza kubadilika.

‎Niliwaza tofauti.

‎Nikaongea tofauti.

‎Nikaanza kuona fursa zilikuwa karibu na mimi kila siku.

‎Zilikuwa zikinipita kwa sababu akili yangu haikuwa trained kuziona.

‎Nikajua kuwa pesa kwanza hupatikana kichwani kabla haijashikwa mkononi.

‎Nakumbuka usiku mmoja nililala njaa huku nimeshikilia kitabu cha Rich Dad Poor Dad mkononi.

‎Nilikuwa nimetoka kumtembelea rafiki yangu ambaye alinitamkia, "Bro, acha hizo ndoto zako za kuwa tajiri, haziwezekani hapa bongo!"

‎Nilicheka kimoyomoyo.

‎Siku hiyo hiyo nilijifunza kuhusu assets vs liabilities...

‎Nikaanza kuandika ndoto zangu chini.

‎Miezi sita baadaye nilianzisha biashara ya mtandaoni.

‎Sasa hivi watu wananishangaa.

‎Wengine wanadhani ni miujiza.

‎Lakini ukweli ni kwamba nilianza kusoma vitabu sahihi.

‎Vile ambavyo havikuniambia niingoje serikali,

‎...bali nianze na nilicho nacho.

‎Ndiyo Leo...

‎Kama una hasira na hali yako ya sasa.

‎Kama una uchungu kuona unahangaika miaka nenda miaka rudi bila mabadiliko…

‎Jibu halipo kwenye kulalamika.

‎Lipo kwenye kuchagua kusoma vitu sahihi.

‎Chukua kitabu kimoja tu leo. 

‎Kisome kwa moyo. 

‎Kitabadilisha maisha yako. Kama kilivyobadilisha yangu.

‎Kama unataka, naweza kukupa listi ya vitabu hivyo na ni kwa nini kila kimoja kilinibadilisha. 

‎Na vimetafsiriwa kwa lugha ya kiswahili Kizuri,

‎Kama unavitaka bonyeza h

apa 👇 nitakupatia,

‎Ni hapa 👉*https://wa.link/dk8lxg*

‎Karibu.

‎Mkufunzi Ramadhan

‎0750376891.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection