Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Kakaa/Dadaa...
Vinaweza Kubadilisha Yako Pia.
Ndiyo Leo.
Miaka kadhaa nyuma... nilikuwa na akili lakini maisha yalikuwa hayanisikii.
Nilikuwa najua mambo mengi, ila siyo yanayoweza kulipa bili.
Nilikuwa naenda kusoma vitabu vya shule tu, vitabu vyenye mistari mingi isiyoeleweka.
Vyenye theory nyingi lakini maisha yangu halisi hayabadiliki.
Unajua uchungu wa kujua sana lakini huna kitu?
Kila mtu anakuita mwerevu ila huna ata buku mfukoni?
Kila mtu anakusifia una akili ila huwezi kumsaidia hata mama yako elfu tano?
Ni kama una cheti cha kuogelea lakini unaishi jangwa.
Unajua kuelea, lakini hakuna maji!
Hapo ndo nilijua, kuna kitu kimekosewa.
Nilivyokaa chini nikagundua kitu kimoja.
Sio vitabu vyote vina uwezo wa kubadilisha maisha.
Kusoma tu hakutoshi—swali ni: unasoma nini?
Unapiga msuli wa vitabu vya lecture, wakati watu waliofanikiwa wanasoma vitabu vya pesa, mindset, ujasiriamali.
Vitabu vya kawaida vinakupa daraja la kupita kwenye mitihani.
Vitabu sahihi vinakupa daraja la kupita kwenye maisha.
Nilipoanza kusoma vitabu vya akina Robert Kiyosaki (Rich Dad Poor Dad),
Brian Tracy (No Excuses!), Napoleon Hill (Think and Grow Rich),
Jordan Belfort (Way of the Wolf)...
Maisha yalianza kubadilika.
Niliwaza tofauti.
Nikaongea tofauti.
Nikaanza kuona fursa zilikuwa karibu na mimi kila siku.
Zilikuwa zikinipita kwa sababu akili yangu haikuwa trained kuziona.
Nikajua kuwa pesa kwanza hupatikana kichwani kabla haijashikwa mkononi.
Nakumbuka usiku mmoja nililala njaa huku nimeshikilia kitabu cha Rich Dad Poor Dad mkononi.
Nilikuwa nimetoka kumtembelea rafiki yangu ambaye alinitamkia, "Bro, acha hizo ndoto zako za kuwa tajiri, haziwezekani hapa bongo!"
Nilicheka kimoyomoyo.
Siku hiyo hiyo nilijifunza kuhusu assets vs liabilities...
Nikaanza kuandika ndoto zangu chini.
Miezi sita baadaye nilianzisha biashara ya mtandaoni.
Sasa hivi watu wananishangaa.
Wengine wanadhani ni miujiza.
Lakini ukweli ni kwamba nilianza kusoma vitabu sahihi.
Vile ambavyo havikuniambia niingoje serikali,
...bali nianze na nilicho nacho.
Ndiyo Leo...
Kama una hasira na hali yako ya sasa.
Kama una uchungu kuona unahangaika miaka nenda miaka rudi bila mabadiliko…
Jibu halipo kwenye kulalamika.
Lipo kwenye kuchagua kusoma vitu sahihi.
Chukua kitabu kimoja tu leo.
Kisome kwa moyo.
Kitabadilisha maisha yako. Kama kilivyobadilisha yangu.
Kama unataka, naweza kukupa listi ya vitabu hivyo na ni kwa nini kila kimoja kilinibadilisha.
Na vimetafsiriwa kwa lugha ya kiswahili Kizuri,
Kama unavitaka bonyeza h
apa 👇 nitakupatia,
Ni hapa 👉*https://wa.link/dk8lxg*
Karibu.
Mkufunzi Ramadhan
0750376891.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni