‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

‎Vitabu 3 Vilivyomtoa Huyu Kwenye Umaskini Kabisa Mpaka Kuwa Milionea


‎Bro!

‎Yani kuna kipindi alikuwa hana hata buku ya vocha.

‎Hana biashara.

‎Hana network.

‎Hana tumaini.

‎Alikuwa anapambana na maisha bila silaha.

‎Mtaa unamjua kama yule jamaa wa "bado tu".

‎Lakini sasa hivi?

‎Anaeza kukodi ndege.

‎Na anadai, vitabu vitatu tu ndiyo vilimtoa huko alikokuwa.

‎Watu wengi wako hoi.

‎Kazi ni kutafuta hela.

‎Hela yenyewe haikai.

‎Kila siku ni mipango, lakini hakuna kinachotoka.

‎Na tatizo kubwa ni hili:

‎Hawajui wanachokosa ni maarifa.

‎Unasikia mtu anasema:

‎"Hela ipo, mimi sina tu connection."

‎Au

‎"Sisi huku hatujapangiwa kuwa matajiri."

‎Aisee, hiyo ni uongo.

‎Kama hujui kutengeneza hela.

‎Na hujui kuitunza.

‎Halafu bado unaidai dunia ikutendee haki?

‎Kuna mtu mmoja alisema:

‎"Ukiwa maskini na bado hujifunzi, unajitakia."

‎Inaumiza lakini ni ukweli.

‎Maisha hayaoni huruma.

‎Ni ya wale wanaojua.

‎Wanaojifunza.

‎Wanaojichukua serious.

‎Sasa wengine wanasoma vitabu vingi,

‎Lakini maisha yao ni yale yale.

‎Kwa nini?

‎Wanasoma bila kuelewa nini wanatafuta.

‎Vitabu vinakuwa burudani tu.

‎Sio silaha ya mapambano.

‎Ili uvuke, usome vitabu vya kubadilisha mindset, si hadithi za mapenzi.

‎Sasa huyu jamaa alichukua hatua.

‎Akanunua vitabu vitatu tu.

‎1. “Rich Dad Poor Dad” –Cha Robert Kiyosaki

‎Hiki kimemfundisha tofauti kati ya kutumia hela na kuitengeneza.

‎Asset vs Liability.

‎Hela ya rent siyo yako. Jenga chanzo cha mapato ya uhakika.

‎2. “The Richest Man in Babylon” – George Clason

‎Hiki kimemfundisha nidhamu ya pesa.

‎Kujiwekea asilimia 10 kila hela anayopata.

‎Na kuitumia kwa busara.

‎3. “Think and Grow Rich” – Napoleon Hill

‎Hiki kimemfundisha nguvu ya akili.

‎Kwamba unachokiamini, unaweza kukifikia.

‎Aliandika ndoto yake. Akaifanya mission. Na maisha yakageuka.

‎Bro alikuwa anauza chips mitaani.

‎Jioni anarudi nyumbani na 5,000.

‎Siku moja akaona duka la vitabu.

‎Akanunua "Rich Dad Poor Dad" — kwa bahati tu.

‎Akakaa kusoma usiku kucha.

‎Aliamka akiwa mtu tofauti kichwani.

‎Akaanza kuweka akiba.

‎Akaanza kuuza bidhaa online.

‎Akaanza kusoma kila siku.

‎Leo hii ana biashara tatu.

‎Ana maduka.

‎Ana wafanyakazi.

‎Ana familia inayomtegemea.

‎Na anasema:

‎"Kama si vile vitabu vitatu, bado ningekuwa naomba vocha."

‎Unaonaje?

‎Unaweza kubadilika kwa kusoma tu?

‎Ndio kabisa.

‎Ila usome vitabu sahihi.

‎Usome kwa nia sahihi.

‎Na uanze kutenda.

‎NB: Kuna watu hawana pesa, sio kwa sababu hawana kazi… bali kwa sababu hawana maarifa.

‎Na maarifa yako kwenye kurasa.

‎Kupata tafsiri ya hivi vitabu vitatu (3),

‎Tuma ujumbe "NATAKA TAFSIRI YA VITABU VITATU"

‎Kwenda 0750376891.

‎Karibu.

‎0750376891.

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?