Unakufa Taratibu… Bila Hata Kujua Sababu? HUJISOMEI!
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Unajua nini kaka/dada…
Kuna maumivu huwa hayapigi kelele.
Hayaleti presha. Hayajulikani fasta.
Yanakuja polepole… kimyakimya… mpaka siku moja unajikuta umepotea kabisa.
Na moja ya maumivu hayo ni…
Maisha Bila Kusoma Vitabu.
Soma hapa sasa:
Watu wengi wanaishi kama vile kusoma ni kwa ajili ya shule tu.
Au ni kitu cha wasomi.
Au ni “luxury” ya watu wanaotafuta PhD.
Lakini ukweli ni huu:
Maisha Bila Kusoma ni kama gari bila mafuta.
Unalipenda. Unalipiga mswaki kila asubuhi.
Lakini halisogei.
Linasimama pale pale, siku baada ya siku.
Umeshajiuliza kwanini maisha yako yamekuwa magumu hivi?
Kwanini kila mwaka una malengo… lakini hakuna kinachobadilika?
Kwanini wengine wanakimbia… na wewe unatembea?
Au hata kutambaa ni kazi?
Ni kama dunia inasonga mbele… lakini wewe umesahaulika.
Unajituma. Unahangaika.
Lakini bado maisha hayakusikilizi.
Na wakati wewe unapiga miayo ukiangalia TikTok…
wengine wanasoma makala, vitabu, kozi, wanajifunza skills…
na wanachukua fursa zako. Ndiyo!
Wanachukua FURSA Zako LIVE!
Wengi hudhani pesa hupatikana kwa kuwa tu mchapakazi.
Eti ukiamka mapema na kulala late… utapiga hela.
Mbona mlinzi wa duka analala saa nane za usiku?
Mbona mama ntilie anachemsha maharage saa kumi alfajiri?
Sio kazi tu kaka…
Ni akili.
Ni maarifa.
Ni mbinu.
Ni kusoma.
Kusoma kunakupa miwani ya kuona pesa mahali wengine hawaioni.
Kusoma kunakufungua akili, kinoma.
Kusoma kunakuonyesha shortcut halali.
Unataka kuanza kuona mabadiliko ya kweli?
Unataka pesa ianze kukuona?
Unataka kutoka kule kubaya uliko?
Jisomee.
Na siyo lazima usome vitabu vigumu kama sheria.
Anza na makala kama hii.
Anza na kurasa moja kwa siku.
Anza na kitu kinachohusu maisha yako moja kwa moja, pesa, mahusiano, biashara, mawasiliano, akili ya mtu mzima.
Kila ukurasa unakosoma… unakukomboa.
Mimi mwenyewe nilikuwa sina time na kusoma.
Nilidhani *mimi ni mwerevu tu wa kuzaliwa.*
Eti akili inatosha.
Nilikuwa na kiburi ya kijinga.
Mpaka siku moja nilikosa kazi… sababu tu niliulizwa swali la kawaida kwenye interview ,nikashindwa.
Swali lilikuwa kwenye kitabu nilichowahi kukiona… nikapuuza.
Nikaanza kusoma… polepole.
Leo hii, nimeandika makala hii, na unaisoma.
Najua kuandika kwa kuvuta hisia.
Najua kuuza kwa maneno.
Najua kuishi kwa akili, si jasho tu.
Yote… kwa sababu nilianza kusoma vitabu.
Maisha ni kama mtihani usio na tarehe ya kuanza.
Kama hutasoma… utaendelea kufeli.
Usikubali maisha yakupite tu.
Chukua hatua leo.
Jisomee.
Jifunze.
Jikomboe.
Maana kama hutajifunza leo…
Kesho itakugharimu zaidi.
Kama Unataka Kushirikiana Na Wenzako Kwenye Safari Hii Ya Usomaji Wa Vitabu,
Basi Tuma Ujumbe,
*NATAKA KUSOMA VITABU*
Kwenda 0750376891.
Kutoka Kwa Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,
Mkufunzi Ramadhan Amir.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni