Siri Ya Kusoma Vitabu Vingi Bila Kuvisahau.....
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Kakaa/Dadaa Yangu...
Unasoma kitabu leo... kesho umesahau kila kitu.
Ushaona hiyo kitu? Inachosha. Inakatisha tamaa.
Unajikuta unasoma tu, lakini hamna unachobeba.
Kama umewahi kujisikia hivyo… karibu kwenye club yetu.
Lakini leo nataka nikuambie kitu cha maana sana.
Siri ambayo wengi hawajui.
Siri ya kusoma vitabu vingi bila kuvisahau.
Na kuvitumia kukuinua maishani.
Unasoma, unasahau. Unasoma, unasahau.
Kama vile ubongo wako unazima mara tu ukifunga kitabu.
Unajikuta unarejea kwenye maisha ya zamani.
Unasema “Aaah, kile kitabu kilikuwa kizuri sana…”
Lakini ukuliza ulijifunza nini? Unashindwa kusema.
Inaumiza. Sana.
Ni kama unakula chakula kizuri, lakini mwili wako haukipokei.
Hakuna nguvu. Hakuna mabadiliko. Hakuna matokeo.
Lakini tatizo si wewe.
Tatizo ni mbinu unayotumia.
Watu wengi husoma vitabu kama vile wanasoma gazeti.
Wanakimbia. Wanamaliza haraka.
Wanataka kumaliza kurasa nyingi bila kutafuna kilichoandikwa.
Halafu wanashangaa kwa nini hawabadiliki.
Ndio maana hata baada ya kusoma vitabu 10…
Maisha yao bado hayajabadilika.
Kipato bado ni kilekile.
Tabia zilezile.
Na ndoto bado hazijaguswa.
Hebu nikufundishe siri moja kali sana.
Kama kweli unataka kusoma bila kusahau…
Fanya hivi:
1. Soma kwa sauti. Ndiyo, usione haya. Sauti inasaidia ubongo kukumbuka.
2. Andika mistari inayokugusa. Si kusoma tu tafuna. Tafakari. Tafsiri.
3. Tumia kile unachosoma. Usisubiri. Jaribu. Ongea nacho. Fundisha wengine.
4. Rudia mara kwa mara. Ndiyo maana kuna repeat kwenye muziki na kwenye vitabu pia!
Na kama unataka kwenda level nyingine…
Kuna kitabu kipya kimetoka.
Kali kinoma kinachobeba haya yote kwa undani.
Kinaitwa “NGUVU YA VITABU”
Hiki sio kitabu cha kukutisha kwa misamiati.
Ni kama vile unazungumza na rafiki yako wa karibu.
Kinakufundisha:
Jinsi ya kuchagua vitabu sahihi
Mbinu za kusoma haraka lakini kwa kina
Njia ya kubadili usomaji kuwa matokeo
Na jinsi ya kuvigeuza vitabu kuwa pesa!
Na ngoja nikuambie hadithi moja fupi.
Jamaa mmoja alikuwa anapenda sana kusoma… lakini alikata tamaa.
Kila kitabu anakisoma, anakisahau.
Mpaka alipopata kitabu cha “NGUVU YA VITABU” kwa bahati.
Akabadilika.
Leo hii anafanya kazi kubwa sana…
Anafundisha wengine…
Na anasema hivi:
“Sikujua kuwa tatizo halikuwa mimi bali mbinu zangu.”
Na wewe pia unaweza kubadilika.
Usiachwe nyuma.
Chukua nakala yako ya NGUVU YA VITABU leo.
Usome kama mwelevu, ukumbuke kama bingwa.
Maisha yako hayawezi kuwa vilevile tena.
Kama Upo Tayari Andika Ujumbe "NATAKA NGUVU YA VITABU"
Kwenda 0750376891.
Karibu.
Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan Amir.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni