Sanaa Ya Kuandika Kichwa Cha Habari Cha Kutosha Kuusimamisha MOYO Wa MTEJA
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
“Ukishika hii, unaweza kuuza barafu jangwa la Sahara”
Kakaa/Dadaa Yangu....
Unajua shida kubwa ya waandishi wengi wa matangazo?
Wanahangaika kuandika miandiko mizuri sana…
Lakini "kichwa cha habari chao ni cha kawaida sana".
Halafu wanashangaa kwa nini hakuna anaye-click.
Wanasema watu hawasomi.
Hapana.
Watu wanasoma
Wanasoma vichwa vya habari tu.
Kama kichwa hakishiki moyo…
Kama hakimshtui mteja…
Kama hakimfanyi asimame hata kama alikuwa anaenda chooni…
Hutauza kitu.
Unajua inakera kiasi gani kuandika post kali, halafu hakuna mtu ana-comment?
Halafu mtu mwingine anaandika tu:
"Siku zote pesa ziko mitaani."
Anapiga emoji 3 za moto.
Anapata likes 400.
Inakuchoma roho.
Unajisikia umechemka.
Unajiuliza, “Kwani shida iko wapi?”
Shida iko kwenye kichwa cha habari.
Hicho ndo mtego.
Na mtego ukikosa chambo, samaki hawezi kung’ang’ania.
Sasa sikia kaka/dada...
Kichwa cha habari siyo tu sentensi ya mwanzo.
Ni mlango.
Ni ngumi ya kwanza.
Ni busu la kwanza kwenye story.
Ni densi ya kwanza kwenye harusi.
Ukiboa hapo game imeisha.
Na hapa wengi wanaboi.
Wanatumia vichwa vilivyojaa maneno ya “kitaalamu”, “kawaida”, au “yasiyoamsha hisia”.
Hata chura wa bwawa hawezi kushtuka navyo.
Mfano mbaya:
“Jinsi ya kupata wateja wengi”
Huo ni mfu. Hauchochei hamu.
Sasa sikia kichwa kinachopiga kelele:
“Wateja Wako Hawakimbii Wewe Ndio Unawafukuza Bila Kujua
(Soma Hii Kabla Hawajakutoka Kabisa!)”
Kichwa kama hicho?
Kinasimamisha moyo.
Suluhisho ni hili:
Andika kichwa kama mtu anayeandika SMS ya kuokoa mapenzi.
Kama mtu anayepiga kelele ya moto kwenye nyumba.
Kama mtu aliyepoteza wallet yenye mshahara wake wote.
Kichwa lazima kiwe na:
Shida.
Shtuko.
Siri.
Sababu ya mtu kusimama na kusoma.
Na unahitaji fomula kali.
Mojawapo ni hii hapa:
“(Ahadi Kubwa + Muda Mfupi + Hatari Ikikosewa)
Mfano:
“Jinsi Ya Kuandika Kichwa Kimoja Tu Kinachoweza Kukuletea Wateja 10 Bila Kulipia Tangazo Ukikosea Hii, Unaweza Kupoteza Fursa Za Mwaka Mzima!”
Ngoja nikupe story ya kweli.
Kuna jamaa mmoja aitwaye Kedi.
Anauza vifaa vya simu Instagram.
Alikuwa anapost picha tu.
Caption: “Zimefika mpya.”
Zero comments. Zero sales.
Nikampa kichwa hiki cha habari:
“Ukivaa Earbuds Mbovu, Unaweza Kukosana na Boss Bila Kujua, Angalia Hii Set Niliyokuwekea”
Broo!
Order 17 ndani ya siku 3.
DM zikawa nyingi kuliko likes.
Jamaa alinipigia usiku wa manane.
Akasema: “Nimeamini, kichwa cha habari ndio roho ya biashara.”
Sasa na wewe?
Usicheze na kichwa.
Ukikosa kichwa kizuri, maandiko yako hayana miguu.
Hayatembei.
Yanakufa.
Tumia muda mwingi kutunga kichwa—kuliko hata content.
Kwa sababu kichwa kikikamata moyo…
Hata maandiko yako ya kawaida yataonekana moto.
Na ukitaka nikusaidie kutunga vichwa vya habari vinavyosimamisha moyo kama betri mpya ya Tesla, niambie.
Mimi ni copywriter wako wa mtaa.
Na sipigi tu kelele nina rekodi ya kusababisha sales zisizotarajiwa.
Tuandike kichwa chako kesho?
Ama uendelee kupost “Zimefika mpya”?
Chaguo ni lako.
Kama Unataka Nikushike Mkono Andika "NATAKA KUWA COPYWRITER"
Kwenda 0750376891.
Karibu.
Ni Mimi Rafiki Yako Ninayekujali Sana.
Mkufunzi Ramadhan Amir.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni