‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

Mbona Unataka Kunilazimisha KUSOMA? Hii Ndio Siri Ya Kusoma Bila Kujiumiza!

 

‎Kakaa/Dadaa Yangu...

‎Kuna Watu Hupenda Kusoma Sana.
‎Wakiamka wanasoma.
‎Wakikula wanasoma.
‎Wakipanda gari wanasoma.

‎Lakini wewe?
‎Ukisikia neno “soma” unaona stress inakuja kama mawingu meusi.

‎Lakini sio kosa lako.
‎Uliwahi kulazimishwa kusoma.
‎Ulikaa darasani ukiangalia saa isogee.
‎Ukasoma ili ufaulu, si kwa sababu unataka.

‎Unajua Tatizo Liko Wapi?
‎Watu wanakudanganya eti:
‎*Tengeneza ratiba ya kusoma.*

‎Hawakuambii namna ya kuitengeneza ambayo haiwezi kukutesa.
‎Wewe si robot.

‎Wewe ni binadamu mwenye moods, pressure, akili na miguno.

‎Hebu Acha Hizi Ratiba Zenye Vifungo Kama Magereza.

‎Soma saa mbili hadi saa nne kila siku?
‎Saa tano asubuhi uanze na kitabu kizito?
‎Hapana.
‎Sio kila mtu anaweza hivyo.

‎Sasa Hebu Tujifunze Tofauti.
‎Kwanza, angalia maisha yako.
‎Wewe huamka saa ngapi?

‎Unakaa kwenye foleni?
‎Una muda wa kuscroll TikTok?

‎Hapo ndo panaitwa nafasi.
‎Usibadili maisha kwa ajili ya kusoma.
‎Badili ratiba ya kusoma ili iingie kwenye maisha yako.

‎Soma Ukiwa Upo Free.
‎Sio lazima iwe muda mrefu.
‎Hata dakika 3 zinatosha.
‎Ukurasa 1 tu kwa siku unaweza kukutoa mbali kuliko yule anayeanza na kurasa 50 siku ya kwanza, kisha anakata tamaa.

‎Ngoja Nikupe Story Ya Kaka Amani.

‎Jamaa alikuwa mvivu kupindukia.
‎Alisema vitabu ni vya watu wenye pesa.
‎Lakini alikua na ndoto ya kubadilika.

‎Akaanza na dakika 5 kila siku.
‎Sio kwa lazima.
‎Alisoma akiwa chooni.
‎Mara nyingine kwenye daladala.

‎Baada ya wiki 3...
‎Akaanza kubadilika.
‎Maneno yake yakaanza kubadilika.
‎Mtazamo wake ukabadilika.

‎Leo hii Amani anauza vitabu online.
‎Na watu wanamsikiliza kama vile google.

‎Sio kwa sababu alikuwa na akili nyingi.
‎Ni kwa sababu alijifunza kusoma bila kulazimishwa.

‎Na Wewe Unaweza.
‎Ukianza kwa dakika 3 tu kwa siku.
‎Ukurasa 1 tu kwa siku.

‎Mahali ulipo, kwa muda uliopo.
‎Hakuna pressure. Hakuna stress.
‎Hakuna ratiba za maumivu.

‎Nimekuandalia Mwongozo Special.
‎Utakusaidia kuanza kusoma kwa raha.
‎Bila force.
‎Bila mikono kukataa kushika kitabu.

‎Bila usingizi kukufuata baada ya sentensi ya pili.

‎Mwongozo huu utakuonesha jinsi ya...
‎✅ Kutengeneza ratiba isiyo na stress
‎✅ Kusoma bila kung’ang’ania
‎✅ Kuongeza maarifa bila kujilazimisha


‎Unausubiri nini?
‎👉 Kupata Mwongozo Kamili.

‎Tuma MWONGOZO,

‎Kwenda 0750376891.

‎Kumbuka, hakuna mtu aliwahi kufanikiwa kwa kulazimishwa.

‎Lakini wengi wamefanikiwa walipojifunza kusoma kwa raha.

‎Anza leo, kwa style yako.

‎Imetoka Kwa Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana.

‎Mkufunzi Ramadhan Amir

‎0750376891.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?