‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

‎Mbinu 3 Rahisi Zitakazokusaidia Na Kufanya Wateja Wakupende Bila Kujipendekeza…

 ‎

‎Kakaa/Dadaa....

‎Unajua shida kubwa ya wauzaji wengi ni nini?

‎Wanahangaika kuwafanya wateja wawapende…

‎Wanawafuata wateja kila kona…

‎Wanaomba omba mapenzi kama wahitaji…

‎Lakini bado…

‎Wateja hawawaoni!

‎Wateja hawawakumbuki!

‎Wateja hawasikii hata huruma!

‎Mbaya zaidi, kuna jamaa mwingine hajawahi hata kujitambulisha sana…

‎Lakini kila mteja anamuita, anamfuata, anamwamini!

‎Unajiuliza… *Kwa nini sio mimi?*

‎Kwa nini mimi ndo napigwa chenga kila siku?

‎Ngoja nikuambie kitu cha ukweli…

‎Wateja hawapendi mtu anayeomba sana.

‎Wanapenda mtu anayewaonyesha thamani… kimya kimya.

‎Na ndo maana leo nakupa hizi mbinu 3.

‎Mbinu za mtaa.

‎Rahisi sana… lakini zenye uzito wa almasi.

‎MBINU #1: Usijiuze, Jionyeshe

‎Acha kulalamika eti watu hawakunotisi…

‎Wewe jionyeshe tu kwa vitendo.

‎Jibu comment zao.

‎Watumie ujumbe unaosaidia bila kutegemea chochote.

‎Toa msaada mdogo mdogo kwenye status zako.

‎Wacha maneno mengi.

‎Tenda.

‎Waonyeshe kuwa upo… bila kuomba.

‎Wateja hupenda watu wanaojituma kimya kimya.

‎MBINU #2: Wasaidie Bila Hata Kuombwa.

‎Siku hizi watu wamechoka na wauzaji wanaoshika shika mabega.

‎Wanataka mtu anayejua shida zao kabla hawajasema.

‎Ukiona mtu analalamika hana wateja…

‎Mtumie voice note moja ya sekunde 15 ya motisha.

‎Ukiona mtu anahangaika na bei…

‎Mtumie tips 3 za kuongeza faida bila kuongeza bei.

‎Unajua nini?

‎Atasave jina lako.

‎Atakutafuta mwenyewe.

‎Kwa sababu ulimgusa… bila kuomba.

‎MBINU #3: Jenga Hadithi Yako Kwenye Maisha Yao

‎Watu wanapenda mtu anayejua walikotoka.

‎Mtu anayewakumbusha maisha yao.

‎Mtu anayewaelewa bila hukumu.

‎Ukitangaza bidhaa, weka kisa.

‎Kisa cha mtu aliyewahi kuwa na tabu… lakini bidhaa yako ikambadilisha.

‎Kisa ambacho wao wanaweza sema, “Dah, huu ni mimi kabisa!”

‎Ukifanya hivi…

‎Utakua si muuzaji tena…

‎Utakua rafiki yao.

‎Na marafiki wanapendwa bila kuomba!

‎SASA SKIZA HII HADITHI FUPI (Real Story)

‎Kuna kijana mmoja anaitwa Musa.

‎Alikua anauza sabuni za mikono.

‎Kila siku alikua anapost, *Beba yako leo…!*

‎Hakuna aliyecomment.

‎Hakuna aliyejibu.

‎Siku moja, akabadili mbinu…

‎Aliandika hivi:

‎“Dada yangu alinipigia simu akilia, mikono yake imejaa mipasuko kwa kutumia sabuni za kawaida. Nikamtumia hii sabuni yangu… ndani ya wiki 1, akaniambia: *Musa, mikono yangu imekuwa kama ya mtoto.*

‎Ndo hapo nikajua… watu hawauzi bidhaa, watu huuza matokeo.

‎Baada ya post hiyo…

‎Watu 57 walimuinbox.

‎28 walinunua siku hiyo hiyo.

‎Leo hii Musa hana muda wa kusaka wateja.

‎Wateja wanamsaka yeye.

‎Kwa nini?

‎Kwasababu....

‎Aliwafanya wampende… bila kuomba.

‎Sasa ni zamu yako.

‎Acha kuomba.

‎Acha kukimbizana.

‎Fanya haya matatu…

‎Na utaona maajabu.

‎Ukihitaji msaada, Piga au Tuma Meseji NAMBA Ni 0750376891.

‎Lakini ukitekeleza hizi mbinu 3…

‎Wateja watapiga hodi kwenye inbox yako kila siku!

‎Karibu.

‎0750376891.

‎Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?