‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

Kwanini Wengi Hawamalizi VITABU? Na Suluhisho Rahisi Kabisa La Kulishinda Hilo!




‎Kakaa/Dadaa...
‎Watu wengi wananunua vitabu kwa hamasa kubwa.
‎Wanapiga picha na kuweka Instagram.
‎Na kuandika "nimekivuta hiki!”
‎Lakini baada ya kurasa tano... wameishia hapo.
‎Wiki mbili baadaye, kitabu kiko kabatini, kinakusanya vumbi.
‎Wewe mwenyewe umewahi kuanza kusoma kitabu ukakimaliza kweli?
‎Usijidai. Tuseme ukweli.
‎Na kama umewahi, je ni vitabu vingapi?
‎Watu hawamalizi vitabu. 
‎Wengi Sana.
‎Hata wale wanaojifanya "book lovers" mitandaoni.
‎Unajua shida ni nini....
‎Unakosa maarifa muhimu.
‎Unajinyima fursa ya kubadilika.
‎Uko pale pale kimaisha.
‎Wenzako wanaendelea, wanachukua hatua kwa sababu wamesoma na wakatekeleza.
‎Wewe bado uko kwenye ukurasa wa 7, unajishawishi, “nitamalizia weekend.”
‎Weekend ikifika? 
‎Unapiga mfululizo wa series 8 kwa siku moja.
‎Na bado unaendelea kujifariji na kusema huna muda wa kusoma!
‎Sasa ngoja nikutobolee siri…
‎Tatizo si wewe.
‎Tatizo si kwamba huna nidhamu.
‎Tatizo si kwamba huna muda.
‎Tatizo ni mfumo wa usomaji unaoutumia.
‎Unajilazimisha usome kila ukurasa kama unasoma mtihani.
‎Unadhani lazima usome kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
‎Unadhani kusoma ni kama kula ugali wa jioni mpaka uumalize.
‎Wrong kabisa.
‎Hivyo ndivyo watu wengi wanavyoamini na wanabaki kushindwa.
‎Sasa hivi, hii hapa ndiyo dawa ya huu ugonjwa.
‎Badilisha mtazamo wako wa kusoma vitabu.
‎Soma kama vile unatafuta dhahabu kwenye mchanga.
‎Usilazimishe kusoma kila ukurasa.
‎Chukua kilicho cha muhimu.
‎Ruka sehemu zisizokusaidia sasa hivi.
‎Anza katikati kama huko ndiko kuna jawabu lako.
‎Soma kwa dakika 10 tu kila siku.
‎Dakika 10 tu bwana!
‎Na kama kitabu ni kizito sikiliza audiobook ukiwa safarini.
‎Usiwe na presha ya kumaliza, kuwa na njaa ya kuelewa.
‎Hapo sasa, utaanza kuona mabadiliko.
‎Kuna mdada mmoja anaitwa Jamila.
‎Alikuwa ananunua vitabu kwa hamu.
‎Akaweka shelf kali kabisa sebuleni.
‎Lakini hakuna hata kimoja alichomaliza.
‎Mpaka siku moja nikamfundisha njia hii ya "kusoma kama mtafuta dhahabu."
‎Akaanza kuchukua vipande muhimu, kuandika notes, kurudia sehemu alizopenda.
‎Leo hii, ananiambia:
‎“Bro, nimetoka mbali. Kitabu kimoja sasa kinanibadilisha maisha.”
‎Na unajua nini?
‎Jamila sasa anaandika kitabu chake.
‎Yaani yule yule aliyekuwa hawezi kumaliza sura ya pili!
‎Sio lazima umalize kila kitabu.
‎Lakini ni lazima uchukue maarifa ndani yake.
‎Badilika.
‎Soma kwa akili, si kwa mazoea.
‎Elimu haitoki kwenye kurasa 300 inatoka kwenye mstari mmoja tu, unaobadilisha maisha yako.
‎Ukishamaliza kusoma haya, usiweke tu moyoni. 
‎Chukua hatua.
‎Rudi kabatini, vuta kile kitabu ulichokiacha. 
‎Tafuta dhahabu ndani yake.
‎Usisome ili kumaliza soma ili kubadilika.
‎Kama Bado Hujajiunga Na Wenzako Kwenye Kundi La Usomaji Wa Vitabu.
‎Tuma Meseji *NATAKA KUNDI LA VITABU*
‎Kwenda 0750376891.
‎Karibu.
‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?