Kwanini Watu Wengi Hawapendi Kusoma Na Suluhisho Rahisi La Kukusaidia.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Kakaa/Dadaa Yangu...
Kuna tatizo moja kubwa sana…
Watu wengi hawapendi kabisa kusoma vitabu.
Wanaona vitabu ni mzigo.
Ni kama kuambiwa uanze kufua na mikono wakati kuna mashine ya kufulia.
Hawana muda.
Hawana hamasa.
Na wengine, hawajui hata wapi pa kuanzia.
Lakini sasa ngoja nikuulize wewe:
Ulishawahi kununua kitabu, ukakisoma kurasa mbili, ukakitelekeza juu ya meza hadi ukakisahau?
Ama ulikuwa na ndoto ya kujifunza mambo fulani, ukasema “acha nitafute kitabu”
Lakini hadi leo unatafuta tu sababu ya kuanza?
Kama ni ndiyo… Haupo Pekee Yako.
Lakini hiyo tabia… inatuumiza sana.
Unajua kwanini?
Sababu maisha hayaendi kwa kubahatisha.
Tunahitaji maarifa.
Tunahitaji kuelewa pesa.
Mahusiano.
Biashara.
Uongozi.
Maisha yenyewe.
Lakini kama husomi…
Utaendelea kuuliza maswali yale yale.
Kuteseka kwa mambo ambayo wengine walishayashinda miaka mingi iliyopita kwa kusoma tu.
Na mbaya zaidi…
Ukizoea kutojifunza, akili inazoea uvivu.
Inaanza kuchoka mapema.
Inakataa kubeba ndoto zako kubwa.
Wewe una ndoto za kuwa milionea, lakini akili yako bado iko kwenye maelfu kwa sababu haipati mazoezi.
Kuna watu hudhani hawapendi kusoma kwa sababu “vitabu vinachosha.”
Au “hawana muda.”
Wengine husema, “mimi si mtu wa vitabu.”
Akisoma tu kichwa Cha habari tayari wanapata usingizi.
Lakini ukweli ni huu:
Sio wewe unayechoka kusoma.
Ni mfumo wa kusoma ndio mbaya.
Vitabu vingi vimeandikwa kwa lugha ngumu.
Kama vile vililengwa kwa maprofesa.
Vingine vinaboa.
Havikugusi. Havina stori. Havina vichekesho. Havina maisha halisi.
Halafu hakuna mtu aliyekuonyesha namna rahisi ya kusoma bila pressure.
Kwa hiyo, kila ukijaribu una-drop.
Sio kosa lako.
Ni mfumo tu mbovu.
Lakini sasa, hii hapa dawa rahisi kabisa:
Soma vitabu vilivyoandikwa kwa lugha rahisi.
Lugha ya mtaani.
Stori nzuri.
Meseji kali.
Somo moja moja linakuingia bila hata kuumia.
Kuna vitabu vinafundisha kama vile marafiki wawili wameketi kijiweni.
Vinafurahisha.
Vinakugusa.
Vinakuelimisha.
Unavikuta asubuhi, kabla hujamaliza chai tayari umekishambulia nusu.
Pia, badala ya kulazimisha kusoma kwa saa nzima anza na dakika tano tu kila siku.
Wewe soma ukurasa mmoja kila asubuhi.
Kesho ukurasa mwingine.
Baada ya wiki, akili yako itaanza kuomba vitabu yenyewe.
Utaingia kwenye lami ya watu wachache sana… wale wanaojifunza kila siku.
Bado nakumbuka vizuri…
Nilipokuwa chuoni, nilikuwa na chumba kilichojaa vitabu.
Lakini vitabu hivyo vilikaa tu kwenye shelf, vikikaa kimya kama sanamu.
Sikuwa nasoma hata kimoja.
Niliona kama ni mapambo tu.
Mpaka siku moja, rafiki yangu alinipa kijikitabu kidogo kilichoandikwa kwa lugha ya mtaani.
Kilitumia stori za mitaani, changamoto za maisha halisi, na suluhisho kali.
Nilikisoma hadi mwisho, bila hata kushika simu.
Nikagundua kumbe kumbe… tatizo langu halikuwa “sikupenda kusoma”.
Tatizo ni kwamba nilikuwa nasoma vitabu visivyofaa.
Tangu siku hiyo, maisha yangu yamebadilika.
Sasa nasoma kila siku.
Najifunza kila siku.
Na najua…
Maisha yangu ya kesho yatatokana na maarifa ninayoyapanda leo.
Kama na wewe umekuwa hujisomei…
Usijichukie.
Usijilaumu.
Chukua tu hatua moja rahisi:
Tafuta vitabu vinavyoeleweka kirahisi.
Vya lugha ya mtaani.
Vyenye stori kali.
Vyenye kukufundisha bila kukuchosha.
Halafu, anza kidogo.
Ukurasa mmoja kwa siku.
Ndani ya miezi michache, utakuwa mtu mwingine kabisa.
Ukitaka mojawapo ya vitabu kama hivyo niambie.
Kwa Namba 0750376891.
Nitakushauri vizuri.
Usikubali maisha yakupite tu ilhali suluhisho lipo mezani.
Karibu.
Mkufunzi Ramadhan Amir.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni