‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

‎Angalia Nguvu Ya Haya Maneno Matano (5) Yenye Kulevya – Maneno Yanayovutia Haraka Machoni.....



‎Rafiki Yangu Mpendwa,

‎Unajua shida kubwa ya wengi?

‎Wanaandika maneno ya kawaida mno.

‎Maneno yaliyokufa.

‎Hayana ladha. Hayagusi hisia.

‎Yanapitwa tu kama upepo.

‎Alafu wanashangaa...

‎Mbona hakuna anayesimama kusoma?

‎Mbona hakuna anayebonyeza?

‎Sasa leo nakuonyesha kitu kinono.

‎Maneno matano tu.

‎Lakini ni hatari.

‎Yana nguvu ya kuvuta macho ya mtu hata akiwa bize aje asome tu.

‎Hebu fikiria…

‎Umeweka post kali sana.

‎Unajua kabisa kuna madini.

‎Lakini hakuna mtu anaye-comment.

‎Hakuna likes. Hakuna saves.

‎Unakata tamaa.

‎Unaanza kufuta post zako.

‎Unaamini labda huwezi.

‎Unajua kwanini?

‎Ni kwa sababu kichwa cha habari yako kinapwaya.

‎Hakina mvuto.

‎Hakina “punch.”

‎Hakina kulevya.

‎Sikiliza kaka, dada...

‎Hili neno “karibu” ni zuri.

‎Lakini halina nguvu kama “karibu ujionee.”

‎Hili neno “soma” ni zuri.

‎Lakini halivutii kama “soma haraka kabla haijatolewa.”

‎Unashika pointi?

‎Lugha ya kuuza lazima iwe na mchele wa maneno ya moto.

‎Maneno ya kishindo.

‎Maneno yanayochoma kama pilipili nyekundu.

‎Kama unataka kuvuta macho ya mtazamaji…

‎Maneno haya ni silaha zako tano:

‎✅ “ANGALIA” – linaamsha macho. Linapiga stop.

‎✅ “SIRI” – linaficha lakini linavuta. Mtu anatamani kujua.

‎✅ “HARAKA” – linaongeza presha. Hali ya dharura.

‎✅ “SOMA HAPA” – linaelekeza. Linaita. Kama alarm.

‎✅ “USIPITE HAPA” – linakataza kwa njia inayovutia zaidi.

‎Haya ni maneno ya kutia chumvi kwenye kichwa cha habari.

‎Yakiwa kwenye sentensi, yanavuta macho kama sumaku.

‎Yanavuta vidole vya mtu vilivyo bize.

‎Anaswipe hadi asome.

‎Bado namkumbuka...

‎Dogo Wa Kinondoni Alivyogeuza Post Za Kupitwa Kuwa Za Kuchafua Notification

‎Kuna dogo anaitwa Jemo.

‎Anafanya biashara ya mashati ya kitenge Instagram.

‎Post zake zilikuwa kama hewa.

‎Anapost, lakini hakuna anayejali.

‎Nikamwambia:

‎“Bro, usianze na ‘karibu’ au ‘hello guys’… weka moto kichwani!”

‎Akaanza kutumia maneno haya matano.

‎Kichwa cha post kikawa kama:

‎“ANGALIA MASHATI HAYA YA KUPASUA MIOYO – USIPITE HAPA!”

‎Matokeo?

‎Within wiki moja…

‎Post moja ilifanya orders 74.

‎DM zikawa zinabana hadi akaweka WhatsApp link.

‎Leo hii, Jemo ni mmoja wa vijana wanaosumbua mtaani.

‎Kwa nini?

‎Kwa sababu aligundua nguvu ya maneno yenye kulevya.

‎Ujumbe Wa Mwisho Kwako...

‎Usiwe tu mtu wa kupost.

‎Kuwa msanii wa maneno.

‎Maneno matano tu…

‎Yanaweza kuwasimamisha watu kama muziki wa Diamond.

‎Anza kuandika kwa hisia.

‎Maneno ya moto.

‎Maneno ya kuvuta.

‎Maneno ya kulevya.

‎Ukitaka list ndefu ya maneno kama haya ya “kulevya macho”… niambie tu.

‎Nitakutumia kama zawadi ya copywriter. 😎🔥

‎Tuma meseji nataka kuwa "COPYWRITER"

‎Kwenda 0750376891.

‎Karibu.

‎Hii Imetoka Kwa Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?