Siri Za Hadithi Za Mauzo...

 *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Rafiki Yangu, Wauzaji wengi wanahangaika kuandika matangazo yanayouza. Wanaandika, lakini hakuna anayeona, hakuna anayeuliza, hakuna anaye nunua. Ni maumivu makali kuona mtu mwingine anauza bidhaa kama yako, Lakini wewe unabaki unalalamika *soko ni gumu.* Kitabu *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Kinakuonyesha namna ya kuandika hadithi zinazogusa mioyo, zinazoeleza, zinasisimua, na hatimaye zinauza. Utajifunza kuandika maandiko yanayovutia macho, yanayobeba hisia, na yanayobadilisha wasomaji kuwa wanunuzi. Pata nakala yako leo. Kwa kuwasiliana na 0755376891. PS; Anza kuandika hadithi zinazouza badala ya maneno yasiyoleta matokeo.

Acha Kuomba Anza Kuitwa….




Rafiki Yangu,


Miaka mitatu (3) iliyopita,


Nilikutana na kijana mmoja ambaye aliniambia, 


“Kaka, mimi huandika inbox 50 kwa siku hakuna anayejibu. 


Wengine hata huniblock.” Nilimtazama kwa upole nikamwambia, 


“Labda tatizo si watu ni wewe kuomba badala ya kuvutia.” 


Siku hizi biashara si ya kuomba omba huruma, ni ya kujijenga kiasi kwamba watu wenyewe wanakuja kukuomba uwauzie. 


Uliposikia kuhusu kampuni kama Apple, walikuita au uliwakimbilia? 


Ndiyo maana leo tunasema: acha kuomba anza kuitwa.


Somo hili utajifunza.


Jinsi ya kuacha kuomba wateja bila mafanikio,


Njia za kujijenga ili wateja wakutafute wenyewe,


Mbinu za kuvutia badala ya kusumbua,Mitazamo mipya ya kibiashara inayokufanya uonekane wa thamani kubwa.


Fikiria ukiamka asubuhi na unakuta ujumbe:


"Habari, nimesikia kuhusu huduma yako, naomba unisaidie…


"Watu wanaku-tag mitandaoni, wanakutumia referrals, wanakutafuta wenyewe. 


Umeacha kusukuma watu sasa unavutia kwa nguvu. 


Unapumua kwa raha, biashara inatiririka kama maji. 


Ndoto ya kila mfanyabiashara ni kuitwa na hiyo ndoto inaweza kuwa kweli, kuanzia leo.


Mimi mwenyewe nilianza kama muombaji. 


Nilikuwa naandika hadi watu wananiita “msumbufu.


” Lakini nilipogundua kuwa mvuto huzalishwa kwa njia ya thamani, nilibadilika. 


Nilianza kutoa elimu ya bure, kushiriki uzoefu wangu, kusikiliza shida za watu. 


Miezi mitatu baadaye, inbox yangu ilianza kubadilika. 


Watu walikuwa wakiniambia, “Nimekuwa nikikufuatilia muda mrefu naomba unisaidie.


” Ndiyo nguvu ya kuitwa.


Njia 5 Za Kuhakikisha Wateja Wanaanza Kukuita…


1. Jenga Thamani Inayoonekana:


Toa elimu. Andika, ongea, rekodi video. 


Watu wanavutwa na watu wanaowasaidia hata kabla hawajawalipa. 


Kama huoneshi unachojua, usitarajie waje kukuuliza.


2. Kuwa Suluhisho, Siyo Muuzaji:


Badala ya kusema “nauza sabuni,” sema “nasaidia akina mama kuondoa madoa bila sumu.” 


Hii inaweka akili ya mteja kwenye suluhisho, si bei.


3. Jenga Mvuto Wa Kitaaluma (Professional Pull):


Fanya kazi kwa ubora hata kama ni kwa mteja mmoja. 


Akitoka akisema “huyu mtu ni wa tofauti,” atakuletea wengine bila kusema.


4. Shirikiana Na Watu Wenye Jamii (Collaboration):


Jifunze kushirikiana badala ya kushindana. 


Tafuta mtu mwenye jamii tayari (mtu wa mitandao, mwalimu, mshauri) mshirikiane na tafuta nafasi ya kujitambulisha bila kuuza moja kwa moja.


5. Kuwa Hai Kwenye Maeneo Ambayo Wateja Wapo:


Kama wateja wako wako WhatsApp, jenga broadcast list. 


Kama wako Telegram, fungua group. Kama wako TikTok, toa elimu fupi. 


Usiogope kuonekana mara kwa mara uvutano hutokea kupitia “exposure.


”Leo, simama kwenye ukweli: kuomba ni mzigo. 


Kuvutia ni mteremko. Anza kujenga mvuto wako:


Chagua jukwaa moja la kuonyesha thamani yako kila siku,


Tengeneza mfumo wa kukusanya ushuhuda wa wateja,


Na kama Bado leo, anza kuitengeneza.


Anyway, kama bado hujapata kitabu kipya Cha NDOANO YA KISASA,


Na kile cha NGUVU YA KITABU,


Unajipunja.


Piga simu sasahivi, Kwenda 0755376891.


Kisha utapewa.


Kutoka Kwa Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,


Ramadhani Amir,


Mwandishi| |Copywriter| Mkufunzi| Kocha.

0755376891


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Mbinu 7 Za Kukumbuka Unachosoma Katika Vitabu Bila KUSAHAU TENA... ‎

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection