‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

Ukweli Wa Kushangaza: Mara Ya Pili Nilipokisoma… Ndipo Nilipokisoma Kwa Mara Ya Kwanza.....

‎Je, unapaswa kusoma kitabu mara moja au mara nyingi? 

‎Hadithi hii itakupa jibu la moyo....

‎Nilikuwa na orodha ndefu ya vitabu.

‎Niliamini mafanikio yangu yanategemea idadi ya vitabu nilivyomaliza.

‎Nikawa najisifu: “Nimesoma vitabu 12 mwaka huu!”

‎Lakini cha kushangaza, sikumbuki hata sura ya kwanza ya vitabu vitano.

‎Nilikuwa msomaji mwenye kasi, lakini si mwenye mabadiliko.

‎Siku moja nikakutana na nukuu:

‎Don’t just read more books.

‎ Reread the right ones.

‎Nukuu hiyo ilinichoma kama sindano ya kweli.

‎Nikajiuliza: “Ina maana nasoma sana lakini bado nipo palepale?”

‎Nilijitetea:

‎“Mbona kusoma kitabu mara moja tu inatosha? 

‎Sina muda wa kurudia! Kuna vitabu vingapi bado sijavifungua?

‎Niliona kurudia kitabu kama kurudia darasa uliokwisha kufaulu.

‎Lakini ndani kabisa, nilihisi kuna kitu kinakosekana.

‎Nikamkuta mjasiriamali mmoja aliyenukuliwa kwenye podcast:

‎.Mimi husoma vitabu vichache lakini kila mwaka narudia vitabu vitatu muhimu.

‎Kila mara nagundua hazina mpya.

‎Akanitajia kitabu alichokisoma mara tano, na jinsi kila usomaji ulivyomletea mafanikio mapya.

‎Nilitulia. Nikasema:

‎"Na mimi nitajaribu."

‎Nikachukua kitabu nilichokisoma miezi 6 iliyopita: “Atomic Habits.”

‎Nikaanza kusoma tena lakini safari hii kwa utulivu.

‎Kila ukurasa uligusa maeneo ya maisha yangu niliyokuwa sikuyazingatia hapo awali.

‎Nikagundua kwamba usomaji wa mara ya pili… ndio ulikuwa wa kwanza wa kweli.

‎Wengine walinishangaa:

‎"Umerudia tu hicho kitabu? Kwani hakuna kingine?"

‎Lakini mimi niliona tofauti.

‎Nikaanza kuandika journal.

‎Nikatekeleza hatua moja moja.

‎Nikaanza kuona mabadiliko halisi maishani.

‎Nilipoanza kutekeleza aliyosema mwandishi, nikakutana na vikwazo.

‎Nikaona ugumu wa kubadili tabia.

‎Nikashawishika kusema:  *Haya yote si rahisi kama alivyoandika.*

‎Lakini nikakumbuka:

‎*Mwandishi alishasema mazoea huhitaji uvumilivu.*

‎Niliendelea.

‎Wiki chache baadaye, maisha yangu yalibadilika:

‎📌 Nikaacha kurudia makosa yaleyale.

‎📌 Nikaweka ratiba za kweli.

‎📌 Nikaanza kuona matokeo.

‎📌 Nikaanza kuishi kile nilichokisoma.

‎Nikaanza kuhamasisha wengine:

‎"Usiwe na haraka ya kukusanya vitabu. Kusanya tabia."

‎Nikaanza kozi ya kusoma kwa kina si kwa haraka.

‎Watu wakaanza kuniambia:

‎"Kwa mara ya kwanza nimesikia mtu akisema tusome kitabu kimoja mara nyingi kuliko vitabu vingi mara moja."

‎Sasa mimi ni msomaji tofauti.

‎Ninapoona kitabu kizuri, siwezi kukiacha kwa usomaji mmoja tu.

‎Naona kina vipindi tofauti vya maisha yangu.

‎Kila usomaji mpya unaniambia kitu tofauti.

‎Sina haraka.

‎Ninapenda kina.

‎Nimekuja kukwambia hivi rafiki:

‎Kitabu kizuri si cha kusomwa mara moja ni cha kuishiwa nacho mara nyingi.

‎Kama kuna kitabu kilikugusa, kirudie tena.

‎Kila safari ya kurudia inakuletea zawadi mpya.

‎Usiwe msomaji wa haraka kuwa msomaji wa mabadiliko.

‎Kujiunga Na Wasomaji Makini Wa Vitabu,

‎Nipigie au Nitumie ujumbe kwenda 0750376891.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Kocha Ramadhan Amir, 

‎Mwandishi | Mkufunzi Wa Mauzo Ya MAFANIKIO | Kocha Wa MAFANIKIO Ya Mauzo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?