‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

‎🔥 Story: Nilipochoka Kuishi Maisha Duni...

Safari Ya Kujiokoa Kwa Vitabu

‎Nakumbuka Miaka 9 iliyopita nilikuwa mtu wa "tutasonga tu."

‎Nilikuwa na maisha ya kawaida, kazi ya kawaida, ndoto za kawaida na hata mawazo ya kawaida.

‎Lakini moyoni…

‎Nilihisi kuna kitu nakikosa.

‎Nilikuwa hai, lakini si mzima.

‎Nilicheka, lakini ni kwa Kujilazimisha.

‎Niliamka kila siku, lakini bila msisimko.

‎Ilikuwa kama maisha yananipita tu na mimi nikiangalia kama mgeni.

‎Siku moja, nilikutana na rafiki mmoja wa zamani alikuwa tofauti.

‎Anang'ara. Anaongea kwa uthabiti. Ana maono.

‎Nikamwambia:

‎“Bro, umebadilika sana. Ulifanya nini?”

‎Akaniambia kwa upole,

‎“Niliamua kuanza kusoma vitabu sahihi. Ndipo maisha yangu yakaanza kubadilika polepole.”

‎Nikacheka kwa kejeli:

‎“Vitabu tu?”

‎Akaniambia,

‎“Ndiyo. Lakini si vitabu vyovyote. Vitabu vya kujijenga. Vitabu vya kuamka tena. Vitabu vya kujikomboa.”

‎Nilirudi nyumbani nikiwa na changamoto kichwani.

‎Mimi? Kusoma vitabu? Mimi si mtu wa vitabu.

‎Niliona kama hiyo ni kwa watu ‘serious.’ Mimi nilizoea TikTok, WhatsApp, Fb, Instagram, YouTube na Netflix.

‎Nilijidanganya:

‎“Mimi najua maisha kwa vitendo, si kwa kusoma.”

‎Lakini moyoni, nilijua nimeshikika.

‎Siku kadhaa baadaye, nilimpigia tena yule rafiki.

‎Nikamuuliza,

‎“Ni vitabu gani hasa ulianza navyo? Nataka tu nijaribu. kimoja tu.”

‎Akacheka, akasema,

‎“Niko tayari kukuongoza. Ila usisome kwa haraka soma kwa kuokoka.”

‎Akanitumia listi ya vitabu 5 vya kuanza upya:

‎📚 Vitabu Vya Kuanza Upya Maisha Yako:

‎1. “The Power of Now” – Eckhart Tolle

‎Unajifunza kuachilia yaliyopita na kuishi sasa. Hapa ndipo safari ya ndani huanza.

‎2. “Atomic Habits” – James Clear

‎> Unaanza kujenga maisha mapya kwa tabia ndogo ndogo kila siku.

‎3. “Awaken the Giant Within” – Tony Robbins

‎Unagundua nguvu kubwa iliyo ndani yako ambayo haijawahi kutumika.

‎4. “The Four Agreements” – Don Miguel Ruiz

‎Unajifunza kuachilia mitazamo ya jamii na kuishi kwa uhuru wa kweli wa akili.

‎5. “The Alchemist” – Paulo Coelho (Riwaya ya Kiroho)

‎Unajifunza kuwa kila mtu ana “hazina” yake safari yako ni ya kipekee.

‎Nilinunua vitabu viwili vya mwanzo.

‎Nikaamua: “Nitavisoma mpaka mwisho,

‎Hata kama ni ukurasa mmoja kwa siku.”

‎Kila ukurasa ulinifungua.

‎Kila sentensi ilikuwa kama dawa.

‎Nilianza kuona mwanga mdogo mbele ya handaki.

‎Wakati mwingine nilichoka. Marafiki wakanicheka:

‎“Eti unataka kubadilisha maisha kwa kusoma vitabu? Hahaha!”

‎Lakini kila nilipohisi kuvunjika moyo, ukurasa mmoja wa kitabu changu ulinikumbusha:

‎“Mabadiliko huanza ndani. Si kwa kelele, bali kwa utulivu.”

‎Nakumbuka usiku mmoja nilijikuta nikilia peke yangu.

‎Nikakumbuka maneno ya Tolle:

‎ “Suffering is necessary… until you realize it’s not.”

‎Hapo ndipo nilipoamka kwa mara ya kwanza si kwa macho, bali kwa roho.

‎Miezi sita baadaye…

‎Nilikuwa mtu mpya.

‎Nilianza biashara ndogo.

‎Niliacha ulevi.

‎Nilianza kujiamini.

‎Watu wakaanza kuniuliza:

‎“Wewe umetumia dawa gani?”

‎Nikawaambia kwa utulivu,

‎“Nilianza kusoma vitabu vinavyobadilisha maisha.”

‎Sasa najua si lazima uzaliwe tajiri.

‎Si lazima uwe na bahati.

‎Si lazima uwe chawa.

‎Unachohitaji ni kuamua kuanza upya, kwa kitabu kimoja tu.

‎Mimi ni yuleyule kwa jina.

‎Lakini ndani yangu, mimi ni mtu tofauti kabisa.

‎Mimi ni kiongozi wa maisha yangu.

‎Na kila siku huanza na kurasa kadhaa za kunionyesha njia.

‎Na sasa nimekuja kukuambia wewe pia:

‎"Ukichoka kuishi maisha duni, soma vitabu visivyo vya kawaida. Ndipo utakapoishi maisha yasiyo ya kawaida."

‎Unataka kuanza upya maisha yako?

‎Usianze na pesa. Usianze na watu.

‎Anza na ukurasa mmoja.

‎Anza na kitabu kimoja.

‎📚 Na uanze leo.

‎Tuwasiliane Kwa Namba 0750376891.

‎Nikupe Hivo Vitabu.

‎Karibu.

‎Rafiki Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?