‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

‎🔥 Nilikuwa Sina Dira... Mpaka Kitabu Kimoja Kilivyonibadilisha...

 ‎Siku zote nilikuwa mtu wa kawaida tu.

‎Ninaamka asubuhi, nakwenda kazini, narudi jioni nikiwa nimechoka.


‎Mishahara ni ileile, ndoto zipo tu kichwani lakini hakuna kinachoenda mbele.


‎Nilihisi maisha hayaendi… lakini pia sikuamini sana mambo ya vitabu.


‎Nikajipa moyo: “Hivi kweli mtu anaweza kufanikiwa kwa kusoma tu?”


‎Siku moja nikiwa kwenye daladala, nikasikia kijana mmoja akimwambia mwenzake:


‎"Mimi sikuchaguliwa chuoni, lakini kitabu kimoja kilinifunulia njia.


‎Sasa nauza online na nimefungua biashara yangu."


‎Maneno yale yalinigusa kama mshale.


‎Je, nami naweza kubadilika kupitia kusoma?


‎Nilijitetea:

‎"Aah! Mbona wengi wanasoma hawafanikiwi? Wengine wanamaliza PhD lakini bado ni masikini."


‎Nikajifariji kwa kisingizio cha muda na pesa.

‎Lakini moyoni nilihisi sauti ikiniambia: "Jaribu. Hata kama ni mara moja."



‎Nikamfuata rafiki yangu mmoja, ambaye nilimjua ana maendeleo makubwa.


‎Alinitazama na kuniambia kwa sauti ya upole:

‎"Mafanikio huanza kichwani. Ukikitunza kichwa chako, maisha yatakusikiliza.


‎Anza na kitabu kimoja tu."

‎Akanipa kitabu cha “Think and Grow Rich.”

‎Nikaanza kusoma taratibu... bila shinikizo.



‎Nilipoanza kusoma, sikuamini macho yangu.

‎Nilianza kufikiria kwa njia tofauti.

‎Nikaanza kuandika ndoto zangu.

‎Nikaanza kutunza muda wangu.


‎Nikagundua, kumbe matatizo yangu mengi yalianzia kwenye namna ninavyofikiri.


‎Wengine walinizomea: "Eti unasoma vitabu? Si vitasaidia nini Tanzania hii?"


‎Wengine wakaniita ‘mjuaji’ au ‘philosopher’ wa mtaa.

‎Lakini nilivumilia.


‎Nikaanza kutafuta vitabu vingine.

‎Nikakutana na watu wenye mawazo chanya.

‎Tukaanzisha group la kujifunza pamoja.



‎Wakati mmoja nilivunjika moyo.

‎Baada ya kusoma na kujifunza sana, bado maisha yalikuwa magumu.


‎Nikaanza kujiuliza: "Je, hivi vitabu ni hadithi nzuri tu zisizo na faida halisi?"


‎Lakini nikakumbuka nukuu moja niliyoisoma:


‎"Watu huacha mita moja kabla ya dhahabu."


‎Nikaamua kuendelea.


‎Miaka miwili baadaye, nilianza biashara ndogo mtandaoni kwa kutumia maarifa niliyojifunza kutoka kwenye vitabu.


‎Nikaanza kupata faida.

‎Nikaanza kusaidia familia.

‎Nikaanza kufundisha wengine.


‎Nilirudi kwa wale waliokuwa wakinibeza.

‎Sikumsema yeyote.

‎Niliamua kuandika blogi, kushiriki video, na kusaidia vijana walio kama mimi wa zamani.

‎Nilitaka kuwapa zawadi ile ile niliyopata: Maarifa.


‎Leo, mimi si yule mtu wa zamani.

‎Sina tena hofu ya kesho.

‎Sina mashaka na ndoto zangu.

‎Nimejifunza kuwa vitabu si hadithi tu ni ramani ya maisha.


‎Mafanikio huanza kichwani, na vitabu ndio ufunguo wa kufungua kichwa.


‎Leo naandika hadithi hii kwa ajili yako.

‎Kama uko pale nilipokuwa mimi, usipuuze vitabu.


‎Usipuuze kujifunza.

‎Soma.

‎Jifunze.

‎Tumia.

‎Kama vilinibadilisha mimi, vinaweza kukubadilisha wewe pia.


‎Karibu tuungane Pamoja,

‎Tuwasiliane Kwa Namba 0750376891.


‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,


‎Mkufunzi Ramadhan Amir



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?