‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎

Hii hapa safari ya kugusa moyo wako.

‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?....

‎Nilikuwa nimehitimu shule.

‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani.

‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.”

‎Sikupata kazi niliyoitegemea.

‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?"

‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha.

‎Siku moja nikakutana na nukuu:

‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain

‎Nikaanza kujiuliza:

‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?"

‎Nikapuuzia.

‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana.

‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa.

‎Mbona havifundishwi shuleni?

‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani?

‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia:

‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua."

‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.”

‎Akaniongeza na kingine: 

‎“The 7 Habits of Highly Effective People.”

‎Nikaanza kusoma lakini si kama mwanafunzi wa shule, bali mwanafunzi wa maisha.

‎Siku moja, nilisoma mstari mmoja tu ambao ulibadilisha maisha yangu:

‎“Mtu maskini hufanya kazi kwa pesa, mtu tajiri hufanya pesa imfanyie kazi.”

‎Nikahisi kama akili yangu imeunganishwa tena kwa mara ya pili.

‎Nilianza kufungua macho ya maisha kwa mara ya kwanza kwa hiari yangu.

‎Wengine waliniona kama nimepotea:

‎Unaacha kusaka kazi na kusoma vitabu vya mabepari?

‎Lakini mimi niliendelea.

‎Nikaanza kuandika mafunzo.

‎Nikaanza kuchukua hatua ndogo.

‎Nilipokutana na changamoto za maisha, nilikuwa na silaha maarifa.

‎Nilipoanzisha biashara yangu ya kwanza, nikapata hasara.

‎Nilikuwa na kila sababu ya kukata tamaa.

‎Lakini nikakumbuka nilichosoma:

‎"Failure is part of learning. Keep moving."

‎Nikanyanyuka, nikasahihisha kosa, na safari ikaendelea.

‎Leo nimejifunza:

‎📌 Kusoma vitabu ni kama kuongea na wakubwa bila kuwa na miadi.

‎📌 Kila kitabu bora ni darasa jipya.

‎📌 Maisha hayana mitaala, bali yamejaa mitihani ya ghafla.

‎📌 Vitabu vina majibu ambayo shule haikuwahi kunipa.

‎Sasa naandika kila kitabu ninachosoma,

‎Ninafundisha wengine,

‎Na nimejenga tabia ya kuwa mwanafunzi kila siku sio kwa ajili ya daraja, bali kwa ajili ya maisha.

‎Mimi si mtu yule wa mwanzo.

‎Nimekuwa mwanafunzi wa maisha.

‎Kila siku ni somo.

‎Kila changamoto ni mtihani.

‎Na kila kitabu ni mwalimu mpya.

‎Rafiki, kama unaishi kama vile umeshahitimu kila kitu umeshaanza kushindwa.

‎Maisha huwatunuku wanafunzi wa kweli.

‎Soma. Tafakari. Tumia.

‎Usome kwa ajili ya mabadiliko, si kwa ajili ya kujisifu.

‎Kitabu kimoja kinaweza kuwa kozi ya maisha yako.

‎Piga simu au tuma meseji, Kwenda 0750376891.

‎Upate vitabu vya Kiingereza na Vya kiswahili Na Vilivyotafsiriwa Kwa Lugha Rahisi Kabisa.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali,

‎Kocha Ramadhan Amir

‎Mwandishi| Mkufunzi Wa Mauzo Ya MAFANIKIO | Kocha Wa Mafanikio Ya Mauzo| 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?