‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

‎ ‎🧨 Maneno Ya Kuuza vs Maneno Ya Kawaida Jifunze LUGHA YA MAUZO.

 ‎

Rafiki Yangu,

‎🛑 Acha tuanze na swali moja rahisi:

‎Ungependa mtu akusikie...

‎au akusikie na achukue hatua?

‎Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuongea tu, na kuongea hadi mtu avue viatu akimbie kununua kitu chako.

‎Karibu kwenye darasa la mtaa hapa unajifunza maneno ya kuuza, si maneno ya kupoteza muda.

‎🔥 1. Watu Wengi Wanakosea Hapa Hawajui Kuzungumza  LUGHA YA MTEJA

‎Wanauza kama wanaelezea.

‎Wanashawishi kama wanahubiri.

‎Wanatumia maneno ya kawaida kwenye kazi ya kuuza.

‎Mfano:

‎“Hii ni bidhaa bora sana.”

‎“Tuna huduma nzuri.”

‎“Karibu tukuhudumie.”

‎Yaani mtu anasikia, lakini hashtuki. Hakuna msisimko. Hakuna kichwa kumruka.

‎Matokeo yake? Wanapitwa tu na wanaojua kuchagua maneno sahihi.

‎💣 2. INAKERA! Unajua Kitu Chako Ni Kizuri, Lakini Watu HAWANUNUI!

‎Unajituma.

‎Unajua bidhaa yako ni ya maana.

‎Lakini ukiweka tangazo, ni kama umeandika barua ya maombi.

‎Ni kama vile unawaomba wanunue, badala ya kuwafanya watamani hadi wasilale.

‎Hapo ndipo penye uchungu.

‎Unalipa matangazo, unachoka kutuma meseji, unajitahidi kutoa ofa... lakini response ni ya kushangaza.

‎👉 Tatizo si bidhaa yako. Tatizo ni lugha unayotumia.

‎🧠 3. SOMA HAPA Maneno Ya Mauzo Hayafanani Na Maneno Ya Kawaida....

‎Kuna maneno yanagusa hisia.

‎Yanazima hofu.

‎Yanachochea tamaa.

‎Yanasisimua akili.

‎Mfano halisi:

‎Badala ya kusema: "Hii ni kozi ya ujasiriamali," sema:

‎"Hii ni silaha ya kutoka kwenye presha ya kukopa kila mwisho wa mwezi."

‎Badala ya kusema: "Hii ni ofa ya bei nafuu," sema:

‎"Kabla bei haijapanda kamata nafasi yako leo!"

‎Maneno ya kuuza hayazungumzii tu faida yanasisitiza maumivu, yanavuruga utulivu, yanatonesha kidonda.

‎✅ 4. SULUHISHO: Jifunze Lugha Ya Kuuza Sio Kuuza Kama UNAOMBA

‎Kama unataka kuuza lazima uzungumze kama unaelewa maumivu ya mteja.

‎Sio lazima uwe na Kiswahili kigumu.

‎Sio lazima uwe na Kiingereza cha Oxford.

‎Unachohitaji ni maneno yanayogusa moyo, sio akili.

‎Na unajua nini?

‎Hii ni kitu unachoweza kujifunza.

‎Hatua kwa hatua.

‎Sentensi kwa sentensi.

‎🪬 5. Hii Ndio Stori Yangu Nilipoacha Kuandika Kama MWALIMU Na Kuanza Kuandika Kama Mteja...

‎Miaka kadhaa nyuma, nilikuwa nashangaa.

‎Ninaandika matangazo, post kali, caption nzuri... lakini kimya.

‎Siku moja nikakutana na fundi mmoja wa matangazo akanionyesha kitu kidogo tu:

‎“Acha kuandika kama mtoa taarifa. Anza kuandika kama mtu aliyewahi kuumia.”

‎Nilianza kubadilika.

‎Nikatumia maneno yanayouma.

‎Nikaanza kusimulia stori.

‎Nikawachokoza watu kwa hisia, sio taarifa.

‎📈 Ndani ya wiki mbili niliuza mara tatu zaidi ya kawaida.

‎Leo hii, nafundisha wengine kufanya hivyo.

‎Kama bado unatumia maneno ya kawaida kujaribu kuuza usishangae kama biashara yako inaendelea kuwa ya kawaida.

‎Badilisha lugha.

‎Zungumza kama mtu anayejali.

‎Gusa maumivu yao.

‎Chochea tamaa zao.

‎Sambaza matumaini yao.

‎Ndipo utaona tofauti ya kweli.

‎Kujifunza zaidi, wasiliana na 0750376891.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.



https://forms.gle/W4acPufZXjFRYjUt7

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?