Siri Za Hadithi Za Mauzo...

 *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Rafiki Yangu, Wauzaji wengi wanahangaika kuandika matangazo yanayouza. Wanaandika, lakini hakuna anayeona, hakuna anayeuliza, hakuna anaye nunua. Ni maumivu makali kuona mtu mwingine anauza bidhaa kama yako, Lakini wewe unabaki unalalamika *soko ni gumu.* Kitabu *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Kinakuonyesha namna ya kuandika hadithi zinazogusa mioyo, zinazoeleza, zinasisimua, na hatimaye zinauza. Utajifunza kuandika maandiko yanayovutia macho, yanayobeba hisia, na yanayobadilisha wasomaji kuwa wanunuzi. Pata nakala yako leo. Kwa kuwasiliana na 0755376891. PS; Anza kuandika hadithi zinazouza badala ya maneno yasiyoleta matokeo.

Kwanini Wanaosoma Vitabu Huonekana Wasomi Zaidi? Siri Ambayo Wengi Hawajui! ‎

Hii Ndio Sababu Halisi Wengi Hawaijui!

‎Rafiki Yangu,

‎Unakutana na mtu hajavaa suti. Hana lafudhi ya kizungu.

‎Lakini ukiongea naye, anakuvutia. Anakuonesha dunia kwa maneno.

‎Unajiuliza, “Huyu kazitoa wapi hizi akili?”

‎Jibu ni rahisi anasoma vitabu.

‎Vitabu sio tu karatasi na maneno. Ni bunduki ya akili.

‎Ukivisoma, unajifunza kuongea kama mtaalam.

‎Unajua kuandika vizuri, kufikiri kwa undani, na kuelewa haraka mambo ambayo wengine bado wanashangaa.

‎Sasa angalia watu ambao hawasomi.

‎Wanaongea kama watu wa mitandaoni.

‎Wanaishi kwa maneno ya "nilisikia", "walisema", na "inavyoonekana".

‎Hawana msimamo.

‎Hawajui kwa nini wanafanya wanachofanya.

‎Wanadanganywa kirahisi.

‎Kila kitu kwao ni “trend”, si truth.

‎Na ukikaa nao, unahisi unarudi nyuma kimaendeleo.

‎Unadhani kusoma ni kazi ya shule?

‎Ama ni kwa watu waliopata division one?

‎Umeambiwa uache vitabu usije ukaonekana "unaringa"?

‎Huo ni uongo mkubwa kuliko ahadi za wanasiasa.

‎Mtu anaposoma vitabu, anachonga akili yake.

‎Anapata maneno ya kusema, hekima ya kutenda, na moyo wa kuelewa.

‎Sio lazima uende chuo.

‎Lakini ukisoma vitabu vizuri, unaweza kumfunza hata Profesa.

‎Anza kusoma vitabu.

‎Si lazima viwe vya kiingereza kigumu kama cha Shakespeare.

‎Anza na vitabu vya maisha, biashara, pesa, mahusiano.

‎Kila siku soma kurasa 5 tu.

‎Baada ya miezi 3, utagundua maneno yako yamebadilika.

‎Mtazamo wako umeinuka.

‎Hata watu wataanza kukuuliza, “Wewe ni msomi wa chuo gani?”

‎Hapo nyuma....

‎Nimekutana na kijana mmoja Kariakoo.

‎Anaitwa Jumanne, alikuwa anauza socks.

‎Kila muda wa mapumziko, alikuwa anasoma kitabu cha "Think and Grow Rich".

‎Nilimwambia, Hii kitu itakusaidia kweli

‎Aliniambia, “Mzee, akili haibebwi na elimu, inabebwa na maarifa.”

‎Miaka miwili baadae, nikamkuta anauza bidhaa mtandaoni.

‎Amesajili kampuni. Ana timu ya vijana 5.

‎Ameniambia, “Mkufunzi Ramadhani, kilichonitoa kwenye stendi sio hela  ni vitabu.”

‎Niliinama nikamwambia, “Wewe sasa ni msomi halisi.”

‎Unataka kuonekana msomi kweli?

‎Si lazima usome vitabu kumi kwa siku.

‎Anza na kimoja.

‎Jifunze. Badilika. Ishi kwa maarifa.

‎Ukitaka vitabu vya kukuchochea kwa lugha rahisi na ya maisha niambie.

‎ Nitakutumia mapendekezo.

‎Tuwasiliane NAMBA Ni 0750376891.

‎Maisha ni mafupi sana kuishi bila maarifa! 🧠🔥

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan,

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Mbinu 7 Za Kukumbuka Unachosoma Katika Vitabu Bila KUSAHAU TENA... ‎

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection