Kwanini Wanaosoma Vitabu Huonekana Wasomi Zaidi? Siri Ambayo Wengi Hawajui!
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Hii Ndio Sababu Halisi Wengi Hawaijui!
Rafiki Yangu,
Unakutana na mtu hajavaa suti. Hana lafudhi ya kizungu.
Lakini ukiongea naye, anakuvutia. Anakuonesha dunia kwa maneno.
Unajiuliza, “Huyu kazitoa wapi hizi akili?”
Jibu ni rahisi anasoma vitabu.
Vitabu sio tu karatasi na maneno. Ni bunduki ya akili.
Ukivisoma, unajifunza kuongea kama mtaalam.
Unajua kuandika vizuri, kufikiri kwa undani, na kuelewa haraka mambo ambayo wengine bado wanashangaa.
Sasa angalia watu ambao hawasomi.
Wanaongea kama watu wa mitandaoni.
Wanaishi kwa maneno ya "nilisikia", "walisema", na "inavyoonekana".
Hawana msimamo.
Hawajui kwa nini wanafanya wanachofanya.
Wanadanganywa kirahisi.
Kila kitu kwao ni “trend”, si truth.
Na ukikaa nao, unahisi unarudi nyuma kimaendeleo.
Unadhani kusoma ni kazi ya shule?
Ama ni kwa watu waliopata division one?
Umeambiwa uache vitabu usije ukaonekana "unaringa"?
Huo ni uongo mkubwa kuliko ahadi za wanasiasa.
Mtu anaposoma vitabu, anachonga akili yake.
Anapata maneno ya kusema, hekima ya kutenda, na moyo wa kuelewa.
Sio lazima uende chuo.
Lakini ukisoma vitabu vizuri, unaweza kumfunza hata Profesa.
Anza kusoma vitabu.
Si lazima viwe vya kiingereza kigumu kama cha Shakespeare.
Anza na vitabu vya maisha, biashara, pesa, mahusiano.
Kila siku soma kurasa 5 tu.
Baada ya miezi 3, utagundua maneno yako yamebadilika.
Mtazamo wako umeinuka.
Hata watu wataanza kukuuliza, “Wewe ni msomi wa chuo gani?”
Hapo nyuma....
Nimekutana na kijana mmoja Kariakoo.
Anaitwa Jumanne, alikuwa anauza socks.
Kila muda wa mapumziko, alikuwa anasoma kitabu cha "Think and Grow Rich".
Nilimwambia, Hii kitu itakusaidia kweli
Aliniambia, “Mzee, akili haibebwi na elimu, inabebwa na maarifa.”
Miaka miwili baadae, nikamkuta anauza bidhaa mtandaoni.
Amesajili kampuni. Ana timu ya vijana 5.
Ameniambia, “Mkufunzi Ramadhani, kilichonitoa kwenye stendi sio hela ni vitabu.”
Niliinama nikamwambia, “Wewe sasa ni msomi halisi.”
Unataka kuonekana msomi kweli?
Si lazima usome vitabu kumi kwa siku.
Anza na kimoja.
Jifunze. Badilika. Ishi kwa maarifa.
Ukitaka vitabu vya kukuchochea kwa lugha rahisi na ya maisha niambie.
Nitakutumia mapendekezo.
Tuwasiliane NAMBA Ni 0750376891.
Maisha ni mafupi sana kuishi bila maarifa! 🧠🔥
Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,
Mkufunzi Ramadhan,
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni