‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

Kurasa 10 Tu… Ndipo Nilipotaka Kukitupa Kitabu Dirishani....

Kuna Kipindi.....


‎Nilijua kabisa kuwa watu waliofanikiwa wanasoma vitabu.


‎Nikajipa changamoto: “Nitasoma kitabu kimoja kila mwezi.”


‎Nikaanza na motisha kali, nikakaa vizuri, nikaweka daftari la dondoo.


‎Lakini… kilichotokea kiliniumiza moyo.


‎Kurasa kumi za mwanzo nilisoma kwa kasi ya roketi.


‎Ilikuwa kama ndoa ya mapema yote ni furaha na matumaini.


‎Lakini ghafla… nikaanza kuchoka.


‎Nilikuwa nimesoma lakini sikumbuki nilichosoma.


‎Nikaanza kuchek WhatsApp katikati ya kurasa.


‎Halafu nikasema: “Labda kitabu chenyewe hakivutii.”


‎Nikaanza kulaumu kila kitu:

‎📌 Lugha ni ngumu

‎📌 Mistari ni mingi

‎📌 Sina muda

‎📌 Mbona ni boring?


‎Nikahifadhi kitabu kwenye droo.


‎Na changamoto yangu ya mwezi? Ilikufa siku ya pili.


‎Nikamkuta kijana mmoja kwenye YouTube, anasema:


‎"Tatizo si wewe. Tatizo ni mfumo wa kusoma uliorithishwa.


‎Vitabu vinahitaji mbinu, si nguvu za mabega."


‎Nikamsikiliza hadi mwisho.


‎Akasema: "Watu huchoka baada ya kurasa 10 kwa sababu hawajasoma kwa malengo, hawajaandaliwa kiakili wala kihisia."


‎Nikachukua kitabu kingine, lakini sasa kwa njia mpya:


‎✅ Nikaandika kwa nini nakisoma

‎✅ Nikagawanya kusoma kwa dakika 10 tu

‎✅ Nikawa nasoma sehemu yenye utulivu

‎✅ Nikaanza na sura ya kuvutia kwanza (sio mstari wa kwanza tu wa mwanzo)


‎Na ghafla… nikagundua siri.



‎Wengine waliniambia: “Kama huchangamki mwanzo, acha tu.”


‎Lakini mimi niliendelea.


‎Nikakutana na wasomaji Telegram na WhatsApp, tukawa tunasoma pamoja.


‎Kila mtu alikiri: “Kurasa 10 za mwanzo huwa ngumu kwa kila mtu!”


‎Sio wewe peke yako.


‎Siku moja niliamua kusoma kitabu kigumu kinachojadili fedha.


‎Kilikuwa na maneno magumu, namba, na historia nyingi.


‎Nilitaka kukiacha.


‎Lakini nikajiambia: "Nitasoma kurasa 5 tu leo, 5 kesho."


‎Mwishoni, nilikimaliza.


‎Na matokeo? Yalinibadilisha!


‎Nikagundua kuwa:

‎📌 Kusoma ni mazoezi ya akili.

‎📌 Sio kila kitabu ni cha kusoma mwanzo hadi mwisho.

‎📌 Hakuna ubaya kusoma sehemu tu ya kitabu.

‎📌 Mbinu bora hufanya kusoma kuwa safari ya kufurahisha.


‎Niliamua kusaidia wengine wanaohisi kama mimi.


‎Nikaandika post: “Kurasa 10 Si Kiama. Ni Geresha Tu Ya Mwanzo.”


‎Watu wakaanza kuniandikia:


‎"Asante. Umeniondolea hatia ya kujiona mvivu.”



‎Mimi sasa ni msomaji wa mbinu, si nguvu.


‎Nikisoma, najua kwa nini nasoma, najua lini niachie, na najua lini nitafakari.


‎Situmii tena kusoma kama adhabu ni safari ya maarifa.


‎Nikuambie ukweli mmoja tu:


‎Kama unachoka baada ya kurasa 10, hauko peke yako lakini pia hujachelewa kubadilika.


‎Kuna njia, kuna mbinu, kuna mwanga.


‎Na ikibidi… usianze na kitabu kizima anza na ukurasa mmoja tu kwa moyo wote.


‎Kujifunza zaidi na kuungana na wenzako makini waliodhamiria kuleta mapinduzi Makubwa,



‎Kupitia usomaji wa vitabu,


‎Basi tuwasiliane kwa simu namba 0750376891.



‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,


‎Kocha Ramadhan Amir,


‎Mwandishi | Mkufunzi Wa Mauzo Yenye MAFANIKIO| Kocha Wa MAFANIKIO Ya Mauzo.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?