‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

Kuna Tofauti Gani Kati ya Kusoma Vitabu Halisi na Audiobooks?

 ‎📘 Sauti Iliongea Nami… Ndipo Nikagundua Nguvu Halisi ya Kusoma

‎Mimi nilikuwa msomaji wa kawaida sana.

‎Nilipenda vitabu… lakini muda wa kusoma? Hakuna!

‎Kazi nyingi, kichwa kiliniuma jioni, mara simu, mara familia.

‎Vitabu vinanivutia lakini kuvisoma ni kama kujilazimisha.

‎Nikaanza kujisikia kama nimechoka kuwa na ndoto zisizoendelezwa.

‎Siku moja rafiki yangu akaniambia:

‎"Kama kusoma kunakuchosha, kwanini usijaribu audiobook?"

‎Nilicheka tu.

‎"Kusikiliza si sawa na kusoma!" Nikasema kwa kejeli.

‎Nilihisi kama nikisikiliza kitabu, nitakuwa mvivu.

‎"Hakuna mtu aliyefanikiwa kwa kusikiliza tu... ni kama kudesa!"

‎Niliendelea kung’ang’ania vitabu vya karatasi, lakini vingi vikasalia na vumbi kabatini.

‎Siku moja nikiwa YouTube, nikamuona mtu mashuhuri akisema:

‎"Audiobooks zimenisaidia kusoma zaidi ya vitabu 50 kwa mwaka."

‎Nikaguswa. Nikasema:

‎"Subiri kidogo… Huyu amefanikiwa, na anasikiliza vitabu? Labda kuna jambo hapa."

‎Nikaamua kujaribu.

‎Nikapakua audiobook ya “The Magic of Thinking Big.”

‎Nikaisikiliza nikiwa kwenye foleni, jikoni, hata bafuni.

‎Kwa mara ya kwanza, nilihisi kitabu kinasimuliwa moja kwa moja ndani ya moyo wangu.

‎Wengine walinicheka:

‎"Eti unasoma kwa sikio? Hujui kusoma au?"

‎Lakini mimi niliendelea.

‎Nikawa na marafiki wa Telegram na WhatsApp wanaosikiliza pia.

‎Tukaanza kushirikiana vipengele vilivyotugusa.

‎Nilijaribu kurudi kwenye vitabu vya kawaida, lakini nikashindwa kuvimaliza.

‎Nilihisi hatia.

‎Je, hii ni dalili kwamba naachana na vitabu halisi?

‎Lakini moyoni nikajiuliza: “Hii ni vita kati ya njia na lengo, sio maadili.”

‎Nikagundua si njia unayosoma, bali kile unachopata.

‎Nilianza kuelewa tofauti:

‎Vitabu vya karatasi vinanifaa nikitaka kuandika, ku-highlight na kufikiri kwa kina.

‎Audiobooks zinanifaa kusikiliza kila sehemu, kujifunza haraka, na kupata msukumo.

‎Zote ni muhimu, ila kwa wakati tofauti.

‎Nimeanza kushauri watu:

‎"Usilazimishe njia. Tafuta njia inayokufaa kwa kipindi chako cha maisha."

‎Mmoja akanijibu: “Sikuwahi kumaliza kitabu hata kimoja, lakini sasa nimesikiliza vitabu vitano. Asante!”

‎Mimi sasa ni msomaji huru.

‎Sioni aibu kusoma kwa sikio wala kwa macho.

‎Najua ninachotafuta ni mabadiliko ya ndani si kujionyesha kwamba nimesoma.

‎Leo, nakuambia wewe msomaji wangu:

‎Sio njia unayotumia kusoma, bali ni jinsi unavyobadilika kwa kile ulichosoma.

‎Ikiwa vitabu vya karatasi havikubebi kwa sasa, usijilaumu jaribu audiobook.

‎Kilicho muhimu ni kujifunza, si kuonekana unajifunza.

‎Niandikie Hapo Kwenye Comment Unataka Kitabu Gani,

‎Au Tuwasiliane Kwa Namba 0750376891.

‎Useme Unataka Kitabu Gani.

‎Karibu.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Ramadhan Amir

‎Mwandishi Wa Vitabu| Mkufunzi Wa Mauzo Yenye Matokeo | Kocha Wa Mafanikio Ya Mauzo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?