‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

Unapuuza Silaha Inayoweza Kukutoa Kwenye Umasikini, Kila Siku Bila Kujua!...

 ‎



‎Rafiki Yangu Mpendwa,

‎Wewe unateseka.

‎Kila siku unakimbizana kutafuta hela.

‎Lakini maisha yako bado ni yaleyale.

‎Unajua kwanini?

‎Kwa sababu unapuuza silaha moja rahisi sana: KITABU.

‎Ndiyo, kile kitu unachokiona kama vya wasomi pekee.

‎Kile unachosema “Mimi si mtu wa kusoma.”

‎Hicho ndicho kinachokuweka hapo ulipo.

‎Vitabu ni Siri ya Mafanikio.

‎Zimebeba akili za matajiri, wabunifu, na watu waliokwishapitia ulichonacho.

‎Lakini wewe unapita navyo kama takataka.

‎Hebu jiulize...

‎Kila siku unatumia masaa 4 kwenye TikTok, Insta, na kuangalia video za utani.

‎Lakini dakika 15 kusoma kitabu?

‎Huipati!

‎Halafu unataka utajiri...

‎Unataka biashara izae...

‎Unataka maisha ya mamilionea...

‎Lakini hutaki kujenga ubongo wa kimamilionea!

‎Huwezi kuwa tajiri kwa akili ya kupenda starehe na uvivu wa maarifa.

‎Wewe ndiye unajizuia mwenyewe!

‎Wengi wanasema, “Aaah vitabu havisaidii.”

‎Huo ni uongo uliopakiwa kwa ujinga.

‎Vitabu vimewabadilisha watu:

‎Waliokuwa maskini kabisa leo ni mabilionea.

‎Waliokuwa hawajui hata kuandika leo wanatoa mihadhara duniani.

‎Hutahitaji kusoma kila ukurasa wa kila kitabu.

‎Dakika 15 tu kila siku… zinatosha kukuingiza kwenye dunia ya tofauti.

‎Kwa hiyo ukisema vitabu havisaidii,

‎unajikata miguu mwenyewe.

‎Sasa sikiliza:

‎Anza leo.

‎Chagua kitabu kimoja tu cha maarifa – hata iwe “Nguvu Ya Buku.”

‎Kaa kimya.

‎Soma dakika 15 kila siku.

‎Andika pointi tatu kila siku.

‎Kisha, fuata unachojifunza.

‎Miezi 3 tu utashangaa:

‎Fikra zako zitakuwa zimebadilika,

‎na mafanikio yataanza kusogea.

‎Vitabu sio tu maneno, ni silaha.

‎Silaha ya akili.

‎Silaha ya kupasua umasikini.

‎Silaha ya kutoka utumwa wa madeni.

‎Kuna kijana mmoja mtaani kwetu alikuwa analala kwa bibi yake.

‎Maskini hadi viatu havina mguu.

‎Siku moja akapewa kitabu:

‎"Think and Grow Rich" – Tafsiri ya Kiswahili."

‎Akasema, “Ah, ngoja nisome tu kuona.”

‎Alichofanya?

‎Kila siku dakika 15.

‎Akaanza kuandika ndoto zake.

‎Akaanza kuuza vitu vidogo vidogo.

‎Leo?

‎Ana kampuni yake ya online.

‎Anasaidia vijana wengine kusoma vitabu.

‎Na kila wiki anakumbusha watu:

‎“Sikufika hapa kwa connections, nilianza na kitabu.”

‎Unakaa kulalamika maisha magumu,

‎wakati silaha iko mezani mwako!

‎Usiipuuze.

‎Usicheze na vitabu.

‎Usicheze na maarifa.

‎Anza leo,

‎soma dakika 15 tu kila siku.

‎Utaona tofauti ndani ya miezi michache.

‎ “Watu wanaofanikiwa si wa ajabu ni watu waliotumia silaha unayoipuuza kila siku: KITABU.”

‎Unataka kubadilisha maisha yako?

‎Anza na kurasa moja tu leo.

‎Anyway, Kama Unataka Vitabu Vizuri,

‎Wasiliana Na 0750376891.

‎Karibu.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

‎0750376891.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?