‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

‎Soma Dakika 15 Kila Siku: Njia Rahisi Ya Kuvunja Umasikini Na Kujenga Utajiri...

 ‎Rafiki Yangu...

‎Unalala na simu mkononi.

‎Unamka na WhatsApp, Insta, na bet.

‎Hujawahi kukaa chini usome dakika 15 hata siku moja.

‎Na bado unajiuliza, “Mbona maisha hayaendi?”

‎Sasa sikia…

‎Watu wengi wanadhani utajiri unatokana na bahati.

‎Au kuwa na baba tajiri.

‎Au kufungua biashara kubwa ghafla.

‎Hawajui siri moja ya ajabu:

‎Dakika 15 tu za kusoma kila siku zinaweza kubadili kila kitu.

‎Sio lazima usome vitabu vigumu kama vya sayansi.

‎La hasha.

‎Unaweza kusoma kuhusu pesa, biashara, akili, au tabia za mafanikio.

‎Ni kama kuchoma mafuta polepole lakini mwisho gari linafika mbali sana.

‎Lakini unajua kinachoumiza zaidi?

‎Watu wanaosema “mimi sibadiliki kwa kusoma!”

‎Wanasema hivyo wakiwa broke.

‎Wakiwa wamechoka na maisha.

‎Wakilia usiku, wakicheka mchana.

‎Wanataka pesa, heshima, uhuru…

‎Lakini hawako tayari kusoma hata ukurasa mmoja kwa siku.

‎Wanakataa kusoma lakini wanakubali kuumia.

‎Wanachoka kusubiri neema ya ghafla, wakati wenyewe wamekata neema ya maarifa.

‎Kuna uongo mkubwa sana unaenezwa mtaani:

‎Eti “vitabu havisaidii tena.”

‎Huu ni mtego.

‎Unaangusha wengi.

‎Kwa sababu ukweli ni huu:

‎Watu matajiri wanajifunza kila siku.

‎Wanasoma.

‎Wanasikiliza.

‎Wanatafuta maarifa mpya kila siku.

‎Wewe unapoacha kusoma, unachagua kubaki nyuma.

‎Kwenye giza la umasikini, la kutegemea wengine, la kupotea.

‎Sasa sikia suluhisho la kweli:

‎Soma dakika 15 kila siku.

‎Ndiyo. Sio saa nzima.

‎Sio kitabu kizima.

‎Dakika 15 tu.

‎Soma kuhusu:

‎Jinsi ya kutengeneza kipato

‎Namna ya kudhibiti matumizi

‎Tabia za watu waliowahi kufanikiwa

‎Kwa mwezi mmoja, utashangaa akili yako inavyobadilika.

‎Kwa miezi sita, utashangaa wallet yako.

‎Kwa mwaka mmoja, watu watakuuliza “ulilogwa na nani?”

‎Nimkumbushe Mwanafunzi mmoja anaitwa Mussa.

‎Alikuwa anauza vocha Kariakoo.

‎Kila siku, jua kali, kazi nyingi, pesa ndogo.

‎Akanunua kitabu cha Nguvu Ya Buku.

‎Akaamua kusoma dakika 15 kila siku.

‎Akajifunza kuhusu kuweka akiba, kuwekeza buku, na kufungua biashara.

‎Miaka miwili baadaye, ana duka lake mwenyewe.

‎Anauza vocha kwa jumla.

‎Na analipia dada yake chuo.

‎Wakati wenzake walikuwa busy na michezo ya simu,

‎Yeye alikuwa busy kuongeza maarifa kichwani.

‎Leo?

‎Anasema hivi:

‎“Siri ni dakika 15 tu za kusoma. Zilinigusa zaidi ya pesa ya bahati nasibu.”

‎Sasa Ni Zamu Yako…

‎Utasema nini miaka mitatu ijayo?

‎"Nilijaribu kusoma na maisha yangu yakabadilika?"

‎Au

‎"Nilikuwa busy na Tiktok, sasa nalia mtaani?"

‎Chagua leo.

‎Soma dakika 15 kila siku.

‎Anza na vitabu kama Nguvu Ya Buku, Siri Za Mafanikio, au Jinsi Ya Kudhibiti Matumizi.

‎Dakika 15 tu.

‎Zinaweza kuwa tiketi yako ya kutoka kwenye umasikini.

‎Kama Unataka Vitabu Vizuri,

‎Tuwasiliane Kwa Kupiga Simu Au Kutuma Ujumbe Kwenda 0750376891.

‎Karibu.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

‎#NguvuYaMaarifa

‎#Dakika15InawezaKubadiliKilaKitu

‎#NguvuYaBukuToto

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?