‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

‎🔥 Mambo 7 Unayojifunza Kwenye Vitabu Ambavyo Hukufundishwa SHULENI 🔥...

 

‎Alizaliwa na Kuishi Maisha ya Kawaida Sana…

‎Anaitwa Jumanne. Mtoto wa pili kwenye familia ya watoto saba. Baba mchomeaji vyuma, mama muuza maandazi. 

‎Aliishi maisha ya kujisitiri, hakuwa na nguo za bei, wala viatu vya kuvutia.

‎ Alipomaliza kidato cha nne, hakupata nafasi ya kuendelea na masomo si kwa sababu hakufaulu, bali kwa sababu hakukuwa na ada.

‎Akiwa nyumbani, kila siku ilimchoma moyo kuona wenzake wakisonga mbele. Hakukuwa na ajira, wala mtu wa kumshika mkono. 

‎Ndoto zake zilianza kuzama polepole. Alianza kuamini pengine maisha haya ni ya waliozaliwa na bahati.

‎Lakini Mambo Yalianza Kubadilika Siku Aliyopewa Kitabu Kimoja.

‎Siku moja, jirani yake alimpa kitabu kiitwacho NGUVU YA VITABU.

‎“Jaribu kusoma hiki Kitabu,” alisema yule jirani, “Hata kama huendi shule, akili yako bado inaweza kuelimika.”

‎Kwa mashaka na shingo upande, Jumanne alianza kusoma. Kurasa za kwanza zilimkumbusha thamani ya muda, nguvu ya kujifunza, na umuhimu wa nidhamu binafsi. 

‎Aligundua kuwa kuna mambo ambayo shule haifundishi, kama vile:

‎1. Namna ya kujiongoza bila kusukumwa.

‎2. Jinsi ya kujiamini hata unapokataliwa.

‎3. Mbinu za kutafuta maarifa nje ya darasa.

‎4. Kujenga nidhamu ya kufanya vitu hata kama huna motisha.

‎5. Jinsi ya kushughulika na fedha ndogo.

‎6. Nguvu ya kuanza na kilicho mkononi.

‎7. Namna ya kuvumilia hadi mafanikio yatokee.

‎‎Akaanza Maisha Mapya Kwa Kuanza Kidogo Sana.

‎Alianza kuuza maji baridi kwenye stendi ya daladala. Watu walimcheka, lakini kila siku alisoma kurasa chache kabla ya kutoka. 

‎Alitumia maarifa yale kujiendesha kibiashara. Alijifunza jinsi ya kutunza pesa, kuwahudumia wateja, na kufikiri kama mtu anayejenga biashara.

‎Mambo Hayakuwa Rahisi.

‎Mara kadhaa alikatishwa tamaa. Aliibiwa, alifukuzwa kwenye maeneo ya kuuza, hata wazazi wake walimwambia "anza kutafuta kazi ya mshahara mdogo tu uoe ukae." 

‎Lakini moyoni mwake, alikuwa tayari ameshaamka. Alikuwa na maarifa ambayo hakuwahi kufundishwa na mwalimu yeyote, bali kitabu.

‎Leo Hii, Jumanne ni Mfanyabiashara Mdogo Mwenye Dira Kubwa.

‎Anamiliki duka la vifaa vya ujenzi na kiosk ya chakula. 

‎Anajitolea kuwasaidia vijana wasio na mtaji kwa kuwapa mafunzo ya kujitegemea. Mara kwa mara huwatembelea wanafunzi mashuleni na kuwaambia:

‎"Shule ni muhimu… lakini vitabu vinaweza kukufundisha maisha ambayo darasa halijawahi kuyagusa."

‎Na Wewe Unaweza Kuanzia Hapo Ulipo.

‎Usingoje mwalimu au ajira. Anza kusoma. Anza leo.

‎Kwa sababu, kama alivyogundua Jumanne:

‎“Maarifa yakiingia kichwani, maisha huanza kubadilika.”

‎📘 Pata nakala ya vitabu vyenye maarifa ya maisha.

‎Usome. Ubadilike. Ushinde.

‎Kupata Kitabu Hiki Na Vitabu Vingine Mzuri,

‎Piga Simu au Tuma Meseji Kwenda 0750376891.

‎Karibu.

‎Kutoka Kwa Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

‎0756694090.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?