‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

Je, Vitabu Vinaweza Kuondoa Msongo wa Mawazo?....

 ‎Rafiki Yangu,


‎Bado namkumbuka....

‎Alikuwa Hana Kitu. Sio Hela. Sio Mtaji. Sio Tumaini.

‎Jina lake ni Salma. Msichana wa kawaida kabisa kutoka familia ya kipato cha chini maeneo ya Mbagala. 

‎Baada ya kumaliza chuo kwa tabu, alipambana kutafuta kazi kwa miaka miwili bila mafanikio. 

‎Polepole, akaanza kupoteza matumaini.

‎Kila siku aliamka akiwa na hofu, akilala na mawazo. Alianza kujitenga na watu, hakupokea simu, na hata chakula kilimchosha. 

‎Msongo wa mawazo ukaanza kula akili yake taratibu.

‎Kila Kitu Kilibadilika Siku Aliyoangukia kwenye Kitabu.

‎Siku moja akiwa kwenye daladala, alimsikia mama mmoja akimsimulia rafiki yake kuhusu kitabu kinachoitwa Nguvu Ya Vitabu. 

‎Salma alijikuta akipata hamu ya kukisoma. Ingawa hakuwa na pesa, aliamua kuuza hereni zake ili kukinunua.

‎Kurasa za kwanza tu, zilianza kumbembeleza polepole kutoka kwenye giza la mawazo. 

‎Alianza kujifunza jinsi akili ya binadamu inavyoweza kubadilika kupitia maarifa. Kitabu kile kilimfundisha mbinu rahisi za kujituliza, kujenga nidhamu, na kujiamini upya.

‎Alianza Taratibu... Lakini Akaendelea.

‎Siku ya kwanza, aliamka mapema na kusoma kurasa chache. Siku ya pili, akaanza kuandika malengo yake. Siku ya tatu, akaamua kuandika blogu kuhusu maisha na afya ya akili.

‎Ndani ya miezi mitatu, watu walianza kumfuata kwenye mtandao. Waliguswa na namna alivyoeleza safari yake ya kutoka kwenye msongo hadi matumaini.

‎Alifungua ukurasa wa Instagram, akaanza kutoa ushauri mdogo kwa vijana waliopitia kile alichopitia.

‎Ilikuwa Rahisi? La.

‎Kulikuwepo siku ambazo alitamani kurudi kitandani na kulia tu. Kulikuwepo maneno ya watu waliomcheka na kumwita "msomi aliyeishiwa.

‎Lakini alikumbuka maneno ya kitabu kile:

‎ *Mawazo mazuri ni kama mbegu. Ukizipanda, utavuna maisha mapya.*

‎Leo Salma ni Taa kwa Wengine.

‎Anaongoza kampeni mitandaoni ya kusaidia vijana wanaokabiliana na msongo wa mawazo. 

‎Ameandika kijitabu chake cha kwanza. Amewasaidia zaidi ya vijana 5,000 kujifunza namna ya kujenga maisha mapya kwa kutumia vitabu.

‎Na bado anasema, "Yote yalianza na kurasa chache tu… na moyo wa kujaribu."

‎Je, Wewe Umeshaanza Safari Yako?

‎Msongo wa mawazo si mwisho wa dunia.

‎Wakati mwingine, unahitaji tu kitabu sahihi…

‎Kuanza tu, kidogo kidogo.

‎Kama Salma, unaweza kuamka tena.

‎📘 Pata nakala ya kitabu ‘Nguvu Ya Vitabu’ leo.

‎Inaweza kuwa mwanzo mpya wa maisha yako.

‎Anyway, kama bado hujapata Kitabu hiki Piga Simu Kwenda 0750376891.

‎Karibu.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir,

‎Kakaa Wa Vitabu.

‎0750376891

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?