‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

Hivi Umeshawahi Kukuta Mtu Anasoma Kitabu Alafu Anakula Pesa? 😳

 

‎Rafiki Yangu,

‎Watu wengi wanasoma vitabu.

‎Wanaandika mistari.

‎Wanaweka nukuu kwenye status.

‎Wanafanya kama wameelewa.

‎Lakini bado broke. 😥

‎Bado wanahangaika.

‎Bado hawajui hela inaingiaje.

‎Kwa nini?

‎Kwa sababu hawajui kusoma kwa akili ya biashara.

‎Hawajui kuchuja hela kwenye kurasa.

‎Hawajui kugeuza maarifa kuwa mpunga.

‎Wanasoma kwa ajili ya kufurahia tu.

‎Sio kutengeneza thamani.

‎Sio kutatua matatizo ya watu.

‎Na ndio maana unaona:

‎Wamesoma sana...

‎Lakini bado wanaomba airtime.

‎Wanaomba lift ya kwenda kazini.

‎Wanapiga status za “Siku moja nitafanikiwa.” 😩

‎Wamesoma vitabu vya Robert Kiyosaki,

‎Lakini mpaka leo hawajui difference ya asset na liability kwa vitendo.

‎Wamepitia Think and Grow Rich,

‎Lakini bado wanathink tu — hawagrow wala hawarichi!

‎Kibaya zaidi?

‎Wanasema: “Mimi ni msomi…”

‎Lakini hela yao ni ya kushika wiki mbili tu.

‎Kusoma vitabu ni kama kuchimba kisima.

‎Lakini kama huna ndoo ya kuchotea,

‎Kuna faida gani?

‎Unabaki na kiu tu. 😓

‎Hii ndio siri:

‎Maarifa bila matumizi ni kama chakula kisichoingia tumboni.

‎Utaona, utavutiwa, lakini hautashiba.

‎Vitabu si vya kukumbuka tu.

‎Ni vya kubadili tabia.

‎Ni vya kutafuta njia ya kusaidia wengine — halafu kulipwa kwa hiyo msaada. 💰

‎Kama unataka kugeuza maarifa kuwa pesa:

‎1. Soma kwa lengo.

‎Uliza: “Nani ana shida hii?”

‎“Naweza kuwasaidiaje kwa haya ninayojifunza?”

‎2. Chuja maarifa ya biashara.

‎Tafuta pointi zinazoweza kugeuzwa kuwa bidhaa, huduma, au mafunzo.

‎3. Anza kidogo.

‎Tumia kile ulichosoma leo kusaidia mtu mmoja.

‎Iwapo atafaidika anaweza kukuamini.

‎Anaweza kukulipa.

‎Hapo ndipo hela inaanza kutiririka.

‎Mwaka 2019, kulikuwa na kijana mmoja aliitwa Mussa.

‎Alikuwa anakaa Mwanza.

‎Maskini lakini mjanja.

‎Aliokota kitabu kilichokuwa kimechakaa — Rich Dad Poor Dad.

‎Akakisoma.

‎Akaandika pointi 10 muhimu.

‎Akaanza kuzielezea kwa watu kwenye WhatsApp group.

‎Watu wakaanza kumuuliza: “Unaweza kutufundisha?”

‎Hakukataa.

‎Akaandaa session ya Zoom.

‎Watu 3 walihudhuria.

‎Baada ya wiki 2, akawa na watu 20.

‎Leo, Mussa ana kampuni yake ya kutoa mafunzo ya fedha.

‎Anaingiza pesa ya maana.

‎Na yote ilianza na maarifa kutoka kwenye kitabu kimoja.

‎Soma ili kusaidia.

‎Saidia ili ulipwe.

‎Ukilipwa basi vitabu vyako vimekuza biashara ya maisha yako.

‎Hapo ndo kusoma kunalipa.

‎Unataka kujua mbinu zaidi za kugeuza vitabu kuwa biashara?

‎🔥 Tafuta kitabu chetu: “NGUVU YA VITABu” kinapatikana sasa hivi kwa ofa ya bure wiki hii!

‎Kukipata wasiliana na 0750376891.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?