Copywriting Ni Silaha Ya Siri Ya Wafanyabiashara Matajiri Wewe Unaijua?
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Rafiki Yangu,
Umeshawahi kujiuliza kwanini bidhaa ya mtu mwingine inanunuliwa sana, ilhali yako haivutii hata mbu?
Wateja wanapita tu. Wanakudharau.
Lakini yule jamaa wa duka la pembeni, kila siku anaweka “sold out” kwenye bango.
Unadhani ni bahati?
Hapana ndugu yangu!
Anaijua sanaa moja ya kichawi… Copywriting!
Leo nitakuonyesha:
Copywriting ni nini, inavyofanya kazi kimyakimya kwenye akili za watu, na kwanini wewe kama mfanyabiashara, unahitaji kuimasta kabla biashara yako haijafa bila msiba.
3. PICTURE — (Fumba Macho, Tazama Maisha Yako Baada Ya Ujuzi Huu)
Hebu tafakari...
Unapost tu chapisho moja WhatsApp au Instagram…
Dakika tano tu, simu yako inaanza kulia.
Mpaka unachoka kupokea order.
Wateja wanakuomba kuwahudumia, siyo wewe kuwabembeleza!
Hii si hadithi ya kufikirika. Ni hali halisi ya wale waliobobea kwenye Copywriting.
Mwaka 2022, kuna kijana mmoja aliandika maneno 12 tu kwenye status ya WhatsApp…
Aliuza vitabu 267 ndani ya siku 1.
Hakuwa na website. Hakuwa na ofisi. Hakutumia hela ya matangazo.
Alitumia maneno yenye mvuto Copywriting.
Sasa sikia,
Copywriting ni nini?
Ni sanaa ya kuandika maneno yanayobeba mvuto, hisia, na msukumo wa mtu kuchukua hatua, iwe ni kununua, kujiunga, au kuulizia zaidi.
Ni kama uchawi wa maneno.
Mfano Rahisi:
Badala ya kusema:
*Nunua bidhaa hii*
Copywriter anasema:
*Usikubali tena kulala njaa, wakati suluhisho liko hapa mkononi.*
Unaona tofauti?
Ni maneno, lakini yamebeba hamasa ya mtu kutaka kuchukua hatua, hapo hapo.
Kwa Nini Hii Ni Muhimu Kwako?
✔️ Unapopost mitandaoni – Copywriting.
✔️ Unapoongea na mteja – Copywriting.
✔️ Unapotangaza bidhaa – Copywriting.
✔️ Unapojieleza ili upate fursa – Copywriting.
Hii ni silaha ya karne hii. Bila hiyo, unapoteza hela kila siku bila kujua.
Usisubiri hadi biashara yako ipotee ndipo uje kusema “Laiti ningeijua hii mapema.”
Watu wanapiga hela kwa maneno tu, tena ya kawaida kabisa.
Chukua hatua.
Jifunze Copywriting leo.
Tafuta kozi, kitabu au mentor anayekuelewa, Anza sasa hivi kabla wateja hawajakusahau kabisa!
Biashara Bila Copywriting Ni Kama Duka Bila Mlango ,Wateja Wanapita Tu Hawaingii.
Jiulize:
Je, utaendelea kujiuza kwa bei ya huruma, au utajifunza kuuza kwa heshima?
Uamuzi ni wako.
Lakini kumbuka: Wanaoandika vizuri, ndiyo wanaishi vizuri.
Ukitaka makala kama hii kwa bidhaa yako, niche au kozi yako, niambie.
Nikuandikie maneno yatakayokuletea hela kabla jua halijazama kesho.
Kama ni ndiyo, Tuma Meseji "NATAKA COPYWRITING" Kwenda 0750376891.
Karibu.
Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,
Mkufunzi Ramadhan Amir
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni