Siri Za Hadithi Za Mauzo...

 *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Rafiki Yangu, Wauzaji wengi wanahangaika kuandika matangazo yanayouza. Wanaandika, lakini hakuna anayeona, hakuna anayeuliza, hakuna anaye nunua. Ni maumivu makali kuona mtu mwingine anauza bidhaa kama yako, Lakini wewe unabaki unalalamika *soko ni gumu.* Kitabu *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Kinakuonyesha namna ya kuandika hadithi zinazogusa mioyo, zinazoeleza, zinasisimua, na hatimaye zinauza. Utajifunza kuandika maandiko yanayovutia macho, yanayobeba hisia, na yanayobadilisha wasomaji kuwa wanunuzi. Pata nakala yako leo. Kwa kuwasiliana na 0755376891. PS; Anza kuandika hadithi zinazouza badala ya maneno yasiyoleta matokeo.

‎Mbinu Rahisi Za Kusoma, Kuandika Na Kushirikisha Maarifa Uliyojifunza....

 ‎


‎Kakaa/Dadaa Yangu.

‎Watu kibao wanasoma vitabu, wanaangalia video kali za maarifa, wanahudhuria semina kali…

‎Lakini baada ya siku tatu tu, hakuna kitu wamekumbuka.

‎Maarifa yote yamepotea kama upepo.

‎Halafu wakikutana na mtu anayetaka kusaidiwa, wanajikuta wamekauka kama jangwa.

‎Wewe pia umewahi kujiskia hivo? Kama unaelewa hiyo hali… hii makala ni yako.

‎Unasoma hadi macho yanachoka.

‎Unanunua vitabu, unaandika notes, unawasha YouTube hadi bundle zinaisha.

‎Lakini ukiwaulizwa ulichojifunza… kimya!

‎Unaanza kurukwa na kujiuliza, “Iko faida gani kusoma kama siwezi kutumia haya maarifa?”

‎Unajikuta unaacha kabisa. 

‎Unakata tamaa.

‎Unaanza kuamini kwamba, “Labda mimi sio wa kusoma. 

‎Hii mambo ya maarifa sio yangu.”

‎Lakini ukweli ni huu:

‎Tatizo sio wewe.

‎Tatizo ni mfumo wa kusoma.

‎Watu wengi wanasoma kama wanapiga mswaki haraka haraka tu.

‎Hawakumbuki, hawajaandika, hawajashirikisha.

‎Unasoma tu, alafu unaiweka kando.

‎ Unatarajia kumbukumbu itafanya kazi yenyewe.

‎Hii ni mbinu mbovu. Inakuteka akili kimakosa.

‎Sasa sikia mbinu rahisi, lakini kali ajabu:

‎SOMA - ANDIKA - SHIRIKISHA.

‎Kwanza, soma kwa lengo usiwe tu unasoma ilimradi usome.

‎Andika pointi tatu au tano ambazo zimekugusa.

‎Halafu, shirikisha mtu mwingine andika post, tuma voice note, ama ongea tu na mtu.

‎Utakaposhirikisha, akili yako inaweka maarifa hayo kwenye kumbukumbu ya kudumu.

‎Inakuwa mali yako ya kweli.

‎Unakuwa sio msomaji tu, bali mtumiaji wa maarifa.

‎Mimi mwenyewe nilikuwa hivi.

‎Nilikuwa nasoma vitabu vya mamilionea, mafanikio, ubongo… lakini sikumbuki hata sentensi moja.

‎Nilisoma kitabu kimoja cha watu mashuhuri, siku tatu baadaye nikawa hata sijui nilichojifunza ni nini.

‎Nikakata tamaa.

‎Lakini baada ya kuanza kuandika yale niliyojifunza kwenye status, kwenye daftari, na kuwaelezea marafiki…

‎Boom! Maarifa yakaanza kubaki kichwani.

‎Nikaanza kuyatumia kwenye biashara.

‎ Nikaanza kuwasaidia watu.

‎Nikaanza kuaminika.

‎Sasa hivi, kila kitu ninachosoma kinaleta matokeo.

‎Kwa sababu nakisoma kwa akili, nakiandika kwa mkono, na nakishirikisha kwa moyo.

‎Kwahiyo,

‎Ukitaka maarifa yakusaidie soma kwa lengo, andika kwa uhakika, na shirikisha kwa moyo.

‎Usisome tu ili uonekane msomi.

‎Soma ili uishi kile ulichosoma.

‎Na kumbuka…

‎Maarifa yasiyotumika, ni mzigo tu wa akili.

‎Ukiona hii makala imekugusa, usiache shirikisha mtu mwingine leo.

‎Maana… maarifa tunayoshirikishana ndiyo yanayobadilisha maisha yetu.

‎Kama Bado Hujajiunga Na Jumuia Ya Wasomaji Wa Vitabu,

‎Basi Bonyeza Hapa 👇 

‎*https://wa.link/nt2nd8*

‎Karibu Tuendelee Kuwa Pamoja.

‎0750376891.

‎Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan Amir.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Mbinu 7 Za Kukumbuka Unachosoma Katika Vitabu Bila KUSAHAU TENA... ‎

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection