‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

Kwa Nini Watu Wanakosa Pesa Ingawa Wanajituma?



‎Kakaa/Dadaa…
‎Umeshawahi kulala ukiwa umechoka sana,
‎Lakini bado huna hata shilingi mfukoni?
‎Umeamka mapema,
‎Ukapambana jua hadi linazama,
‎Ukavumilia kelele za mabosi,
‎Ukavumilia njaa kwa matumaini.
‎Lakini mwisho wa mwezi,
‎unahesabu senti.
‎Unaambiwa: *Jitume zaidi.*
‎Lakini unaumia moyoni,
‎kwa sababu umeshajituma mpaka unaungua ndani.
‎Kama hii ni hali yako,
‎najua uchungu unaoupitia.
‎Ni kama mbio zisizo na mwisho.
‎Unakimbia, lakini huoni mbele.
‎Unapiga hatua, lakini ni kama umerudi nyuma.
‎Wengine wanakucheka.
‎Wanasema huna akili ya pesa.
‎Lakini hawajui mateso yako.
‎Sasa sikiliza kwa makini...
‎Kazi ngumu pekee haitoshi.
‎Inauma kusema, lakini ni kweli.
‎Watu wengi wanaishia kuishi maisha ya mateso,
‎si kwa sababu hawajitumi,
‎bali kwa sababu hawajui cha kufanya na wanachopata.
‎Wanatumia kila walichonacho.
‎Hakuna mpango.
‎Hakuna akiba.
‎Hakuna uwekezaji.
‎Hakuna ndoto inayoelekea kutimia.
‎Na hapo ndipo ndoto nyingi hufia.
‎Ndipo ndoto nyingi hulia kwa ukimya.
‎Lakini bado kuna tumaini...
‎Siku utakapoamua kufikiri tofauti kuhusu pesa,
‎Ndipo utakapogeuza mwelekeo wa maisha yako.
‎Pesa si adui.
‎Pesa si ya kuikimbiza bila kuelewa.
‎Pesa ni mti unaoota pale unapopanda mbegu sahihi.
‎Anza kuipangilia.
‎Anza kuwekeza.
‎Anza kuiona kama njia ya kutimiza ndoto zako.
‎Nakupa mfano...
‎Kuna kijana mmoja, Ali.
‎Kila siku alikuwa kwenye jua, kwenye vumbi, kwenye jasho.
‎Lakini maisha yake yalikuwa yale yale. 
‎Migongoni mwa daladala,
‎maskani ya huzuni.
‎Mpaka siku rafiki yake alivyomfundisha kitu kimoja,
‎Kuiheshimu pesa.
‎Kuipangilia.
‎Kuwekeza hata kidogo.
‎Ali akachukua hatua ndogo.
‎Na hatua hiyo iligeuka kuwa maisha mapya.
‎Miaka michache baadaye akamiliki nyumba,
‎Ana biashara yake mwenyewe.
‎Si kwa sababu alikuwa na bahati.
‎Ni kwa sababu alijifunza kutumia pesa kwa akili.
‎Na wewe pia unaweza.
‎Usikubali maisha yako yawe hadithi ya maumivu yasiyoisha.
‎Chukua hatua.
‎Jifunze sasa.
‎Badilisha maisha yako.
‎Piga Simu: 0750376891
‎Nitakusaidia.
‎Tutapambana pamoja.
‎Mpaka uzishike ndoto zako mkononi.
‎Mkufunzi Ramadhan Amir
‎0750376891

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?