Kwa Nini Watu Maskini Hawapendi Kusoma Vitabu
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Kaka/Dada,
Huu Ni Ukweli Unaoumiza Lakini Utakusaidia.
Maskini wengi hawapendi kusoma vitabu.
Umeshawahi kujiuliza kwa nini?
Yaani mtu anaishi maisha magumu…
Lakini ukimpatia kitabu cha bure chenye maarifa ya kutoka hapo alipo anakudharau.
Akiwa online, anaweza kucheka video 20 za utani…
Lakini video moja tu ya mafanikio, ya dakika mbili ataisema:
“Hayo mambo ya matajiri.”
Hapo ndipo utagundua:
Umaskini hauanzi mfukoni… unaanzia kichwani.
Tatizo Halipo Tu Kwenye Pesa
Watu wengi waliokata tamaa si kwamba hawana pesa...
Ni kwamba hawana maarifa.
Wanajua mpira, wanajua drama za mastaa, wanajua nani kapigana na nani...
Lakini hawajui jinsi ya kuongea vizuri ili wapewe kazi.
Hawajui njia rahisi ya kuweka akiba kidogo kila wiki.
Hawajui hata kusoma CV yao vizuri.
Sababu?
Hawajawahi kupewa nafasi ya kuamini kuwa vitabu vinaweza kuwasaidia.
Kuna Uongo Umekaa Kama Ukweli
“Mimi si mtu wa vitabu.”
“Mimi shule ilinichosha.”
“Sina muda wa kusoma.”
Huo ni uongo ulioota mizizi.
Leo hii mtu ana muda wa kuchat usiku kucha, kuangalia movies na memes…
Lakini hana dakika 10 tu za kusoma eBook ya ukurasa 10.
Na ajabu ni hii:
Maarifa ni yale yale yanayotumiwa na matajiri kuendelea kutajirika.
Ukijifunza Peke Yako, Unakuwa Na Nguvu.
Hujaenda chuo?
Huna cheti?
Hakuna shida.
Soma.
Jifunze marketing.
Jifunze psychology.
Jifunze kuandika vizuri.
Vitabu, podcasts, na mafunzo ya eBook ni njia rahisi ya kuanzisha safari ya mabadiliko.
Usikae ukisubiri serikali au wafadhili.
Maisha yako ni jukumu lako.
Hadithi Yangu Halisi – Ramadhani Amiri
Mimi nilikuwa sina chochote.
Familia ya kawaida. Hakuna connection. Hakuna hela.
Nilianza kusoma vitabu nikiwa na simu ya tochi.
Nilikaa cyber, nikasoma eBooks za mafanikio.
Nikagundua ndoto zangu hazitegemei hali yangu ya sasa.
Zinategemea maarifa ninayoyaweka kichwani.
Nikaanzisha kampeni ya Nguvu ya Vitabu.
Leo hii, watu wamenitumia ujumbe:
“Buku moja imenifanya niamini tena ndoto yangu.”
Na hapo ndipo nikaanzisha Akili Kwanza Consultants kampuni inayofundisha watu kufikiri kisomi bila kungoja cheti.
Unataka Kubadilika? Fanya Hivi Leo:
1. Chagua eBook moja tu rahisi.
2. Soma kurasa tano kila siku.
3. Maliza kitabu kimoja kila mwezi.
4. Fanya hivyo kwa miezi 12 maisha yako yatabadilika.
Vitabu vitakufunulia:
Njia za kuongeza kipato
Mbinu za kuacha matumizi ya ovyo
Mikakati ya kuanza bila mtaji
Siri za kuongea na watu wenye nafasi
Anza Sasa Kabla Mwaka Haujaisha.
Weka oda ya eBook ya Nguvu ya Buku hapa, 👇
0750376891
Au niandikie Nguvu Ya Vitabu,
Kwenda 0785376891
Nitakutumia vitabu vya kuanzia.
Usikubali kubaki nyuma kwa sababu ya uvivu wa kusoma.
Mkufunzi Ramadhan
0785376891.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni