‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

‎Jinsi Ya Kugusa Hisia Za Msomaji Kwa Sentensi Ya Kwanza....

 



Kakaa/Dadaa Yangu....

‎Kuna waandishi kibao mitandaoni.

‎Wanaandika vizuri.

‎Lakini makala zao hazisomwi.

‎Unajua kwanini?

‎Sentensi ya kwanza haina mvuto!

‎Haimgusi msomaji popote.

‎Yaani ni kama unamwambia, "Usisome hii makala."

‎Hebu fikiria...

‎Umechukua muda kuandika.

‎Umetafakari kichwa cha habari.

‎Umetafuta picha kali.

‎Lakini msomaji anaishia tu hapo mwanzo.

‎Hajui kilicho ndani.

‎Hasogei kabisa.

‎Unabaki unaumia kimoyomoyo.

‎“Mbona hawasomi makala zangu?”

‎Ni kama kupika pilau halafu mtu anakataa hata kuonja.

‎Wengi hufikiria kuwa sentensi ya kwanza inapaswa kuwa ya kitaalamu sana.

‎Au iwe na maneno ya Kiswahili kigumu.

‎Au iwe ndefu kama maelezo ya mtihani wa Form Four.

‎HAPANA!

‎Sentensi ya kwanza inapaswa kuwa na kitu kimoja tu HISIA.

‎Ipasue moyo.

‎Iguse akili.

‎Ichokoze curiosity.

‎Ikamate macho.

‎Na iseme, “Usiende popote.”

‎Ukitaka kuandika sentensi ya kwanza inayogusa hisia:

‎Gusa maumivu.

‎Gusa ndoto.

‎Gusa wasiwasi.

‎Gusa ndani ya moyo wake.

‎Mfano?

‎"Unajua uchungu wa kuamka kila siku kwenda kazini, lakini mshahara haukutoshi hata kununua sabuni?"

‎Boom!

‎Msomaji anashtuka.

‎Anajiona humo humo.

‎Anataka kujua zaidi.

‎Anabaki hapo hadi mwisho.

‎Namkumbuka jamaa mmoja aliyenifuata DM.

‎Alikuwa ameandika makala 12.

‎Zote hazina engagement.

‎Alikuwa tayari kukata tamaa.

‎Nikamuuliza, "Sentensi ya kwanza inasema nini?"

‎Akaninukuu:

‎"Katika ulimwengu wa sasa wa kidijitali, maudhui bora yana nafasi kubwa katika kukuza biashara."

‎Nikamuambia ukweli mchungu:

‎"Bro, hiyo sentensi haina roho."

‎Nikampatia mbinu moja tu:

‎Anze kwa kugusa uchungu wa msomaji.

‎Akaandika tena.

‎Makala yake ikaanza:

‎"Unaweza kuwa na biashara nzuri, lakini kama hakuna anayejua ipo... utaishia kulia kimya kimya."

‎Matokeo?

‎Makala iliwaka moto.

‎Likes, comments, shares zikaongezeka kama mvua ya masika.

‎Ukweli ni huu:

‎Sentensi ya kwanza si sentensi tu.

‎Ni mlango wa hisia.

‎Ni kama kofi la upole usoni  linakufanya usimame na kusema, “Ngoja nisome.”

‎Usichezee mwanzo wa makala yako.

‎Hapo ndipo msomaji anaamua:

‎“Nisome au niache.”

‎Sasa nikuulize...

‎Sentensi yako ya kwanza inafanya kazi hiyo?

‎Au inapita tu kama upepo wa usiku?

‎Kama unataka kujifunza zaidi kuhusu ujuzi huu adimu ambao haufundishi shuleni,

‎Basi tuma ujumbe *NIFUNDISHE UJUZI ADIMU*

‎Kwenda 0750376891.

‎Karibu.

‎Makala Hii Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan Amir.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?