‎🔥Siri Za Hadithi Zinazouza Kama Kichaa , Mfumo Wa The Hero’s Journey!🔥 ‎

Kakaa/Dadaa Yangu.... Wewe unajua kwanini hadithi zingine zinaburudisha mpaka unashindwa kutoka kwenye screen? ‎ ‎Unajua kwa nini mtu anakusimulia story mpaka unajikuta unaitikia, *Duh! Alafu ikawaje?* ‎ ‎Basi sikia hii... ‎ ‎Wauzaji wengi wanaandika hadithi ambazo hazigusi hisia. ‎Ni kama kuangalia movie ya kuchosha kwenye slow motion. ‎Wateja hawajali. Wanaskip. Wanapotea. ‎ ‎Lakini... ‎Kuna mfumo mmoja wa KISANII, wakisanii mbaya, ambao ukishaujua, utawakamata watu kama sumaku. ‎ ‎Unaitwa: Hero’s Journey. ‎ ‎Ni mfumo wa hadithi ya shujaa. ‎Yaani mtu wa kawaida, anakutana na changamoto, anapambana, anakata tamaa, anasimama tena, na mwisho anashinda. ‎ ‎Kama Simba kwenye Lion King. ‎Kama Neo kwenye Matrix. ‎Kama wewe kwenye maisha yako. ‎ ‎Sasa tatizo ni hili... ‎Watu wanajaribu kuuza bila kuleta safari ya kihisia. ‎Wanataka kuuza bidhaa kama vile ni maharage sokoni. ‎Wanakosa story. ‎Na bila story,hakuna connection. ‎ ‎Unasema bidhaa yako ni bora? So what? ‎Wateja wanataka kujihisi w...

‎Hivi Ndivyo Nilivyopata Mteja Wangu Wa Kwanza Kwa Kalamu Tu!...

 


‎Kakaa/Dadaa yangu…

‎Hivii ushawahi kukaa na njaa hadi unaandika mawazo kwenye daftari badala ya kula?

‎Mimi nilishawahi.

‎Nilikuwa na ndoto ya kuwa copywriter.

‎Lakini sikujua nianzie wapi.

‎Zero network.

‎Zero pesa.

‎Na mbaya zaidi…

‎Watu hawakuamini kitu kama *kuandika matangazo* ni kazi.

‎Walinicheka.

‎Hawakuziamini ndoto zangu.

‎Wengine walinambia:

‎"We kaa tu uandike mashairi yako huko!"

‎Nilihisi kama naota ndoto ambayo haipo kwenye Google.

‎Lakini moyo haukukubali niachane nayo.

‎Ilikuwa Kama Ndoto Mbaya

‎Kila siku nilikuwa ninaamka asubuhi na kuchora matangazo kwenye daftari la zamani.

‎Hapo....

‎Sina laptop.

‎Sina printer.

‎Nina tu kalamu ya cello na daftari la kasuku.

‎Nilijifunza kuandika matangazo yenye hisia.

‎Yale ya kumgusa mtu mpaka ashindwe kulala bila kukutafuta.

‎Lakini bado…

‎Hakuna mtu aliyekuwa anajua kuwa mimi ni copywriter.

‎Nilikuwa kivuli.

‎Hapo Ndo Nikapiga Stop

‎Nikajikumbusha ile kauli niliyoambiwaga na mentor wangu:

‎*Bro, kama huwezi kuingia kwa milango ya mbele, pita dirishani.*

‎Nikaanza kuandika tangazo kali kama sample.

‎Kalamu tu na karatasi.

‎Nikakaa chini, nikamtengenezea tangazo jamaa mmoja niliyemfahamu kwenye Instagram.

‎Anauza viatu.

‎Sikutuma DM.

‎Sikutuma email.

‎Nilipiga print hiyo kazi kwa shilingi 50 TU stationary.

‎Nikafungasha vizuri.

‎Nikaenda kwao kama mteja wa kawaida.

‎Baada ya kuongea kidogo nikamwambia:

‎"Bro, kuna kitu nimeandika… Naamini kitakusaidia kuuza viatu vyako faster."

‎Alisoma.

‎Akatulia.

‎Akatabasamu.

‎Akanitazama machoni.

‎Akasema:

‎"Bana, hii kitu ni moto wa kuotea mbali!"

‎Ndiyo hivyo…

‎Mteja wa kwanza nilivyompata.

‎Na aliingia kwa sababu ya kalamu tu.

‎Ndio Nikajifunza Siri Hii

‎Watu hawataamini unachoweza…

‎Mpaka uwaonyeshe kwa vitendo.

‎Sio kuomba.

‎Sio kusubiri.

‎Onyesha tu kazi yako hata kama ni bure mara ya kwanza.

‎Na kama unaamini kuwa huwezi kuanza sababu hauna tools…

‎Ngoja nikwambie ukweli mchungu:

‎Huna njaa ya kweli.

‎Mwenye njaa ya kweli, hata kalamu inamtosha kabisa.

‎Leo hii…

‎Ninavyoandika hivi, nina wateja kutoka ndani na nje ya nchi.

‎Lakini nilianza na karatasi na kalamu tu.

‎Hakuna shortcut.

‎Ni damu, jasho na mistari ya kugusa moyo.

‎Kama Wewe Ni Kama Mimi...

‎Kama unahisi upo peke yako.

‎Kama unaandika lakini hakuna anayekuamini.

‎Kama watu wanakudharau kwa vile kazi yako *haionekani*…

‎Jua kwamba kuna mtu mmoja tu unayemhitaji akuamini.

‎Na huyo mtu ni wewe mwenyewe.

‎Tulia.

‎Andika.

‎Sambaza kazi yako.

‎Usiombe nafasi.

‎Itengeneze.

‎Kalamu ndiyo silaha yangu.

‎Na kama mimi niliweza,

‎basi hata wewe unaweza.

‎Kama unataka mwongozo kamili ulionifikisha hapa.

‎Bonyeza Hapa 👇 

‎*https://wa.link/pz47ru*

‎Karibu

‎0750376891.

‎Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan Amir.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?