Hivi Ndivyo Nilivyopata Mteja Wangu Wa Kwanza Kwa Kalamu Tu!...
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Kakaa/Dadaa yangu…
Hivii ushawahi kukaa na njaa hadi unaandika mawazo kwenye daftari badala ya kula?
Mimi nilishawahi.
Nilikuwa na ndoto ya kuwa copywriter.
Lakini sikujua nianzie wapi.
Zero network.
Zero pesa.
Na mbaya zaidi…
Watu hawakuamini kitu kama *kuandika matangazo* ni kazi.
Walinicheka.
Hawakuziamini ndoto zangu.
Wengine walinambia:
"We kaa tu uandike mashairi yako huko!"
Nilihisi kama naota ndoto ambayo haipo kwenye Google.
Lakini moyo haukukubali niachane nayo.
Ilikuwa Kama Ndoto Mbaya
Kila siku nilikuwa ninaamka asubuhi na kuchora matangazo kwenye daftari la zamani.
Hapo....
Sina laptop.
Sina printer.
Nina tu kalamu ya cello na daftari la kasuku.
Nilijifunza kuandika matangazo yenye hisia.
Yale ya kumgusa mtu mpaka ashindwe kulala bila kukutafuta.
Lakini bado…
Hakuna mtu aliyekuwa anajua kuwa mimi ni copywriter.
Nilikuwa kivuli.
Hapo Ndo Nikapiga Stop
Nikajikumbusha ile kauli niliyoambiwaga na mentor wangu:
*Bro, kama huwezi kuingia kwa milango ya mbele, pita dirishani.*
Nikaanza kuandika tangazo kali kama sample.
Kalamu tu na karatasi.
Nikakaa chini, nikamtengenezea tangazo jamaa mmoja niliyemfahamu kwenye Instagram.
Anauza viatu.
Sikutuma DM.
Sikutuma email.
Nilipiga print hiyo kazi kwa shilingi 50 TU stationary.
Nikafungasha vizuri.
Nikaenda kwao kama mteja wa kawaida.
Baada ya kuongea kidogo nikamwambia:
"Bro, kuna kitu nimeandika… Naamini kitakusaidia kuuza viatu vyako faster."
Alisoma.
Akatulia.
Akatabasamu.
Akanitazama machoni.
Akasema:
"Bana, hii kitu ni moto wa kuotea mbali!"
Ndiyo hivyo…
Mteja wa kwanza nilivyompata.
Na aliingia kwa sababu ya kalamu tu.
Ndio Nikajifunza Siri Hii
Watu hawataamini unachoweza…
Mpaka uwaonyeshe kwa vitendo.
Sio kuomba.
Sio kusubiri.
Onyesha tu kazi yako hata kama ni bure mara ya kwanza.
Na kama unaamini kuwa huwezi kuanza sababu hauna tools…
Ngoja nikwambie ukweli mchungu:
Huna njaa ya kweli.
Mwenye njaa ya kweli, hata kalamu inamtosha kabisa.
Leo hii…
Ninavyoandika hivi, nina wateja kutoka ndani na nje ya nchi.
Lakini nilianza na karatasi na kalamu tu.
Hakuna shortcut.
Ni damu, jasho na mistari ya kugusa moyo.
Kama Wewe Ni Kama Mimi...
Kama unahisi upo peke yako.
Kama unaandika lakini hakuna anayekuamini.
Kama watu wanakudharau kwa vile kazi yako *haionekani*…
Jua kwamba kuna mtu mmoja tu unayemhitaji akuamini.
Na huyo mtu ni wewe mwenyewe.
Tulia.
Andika.
Sambaza kazi yako.
Usiombe nafasi.
Itengeneze.
Kalamu ndiyo silaha yangu.
Na kama mimi niliweza,
basi hata wewe unaweza.
Kama unataka mwongozo kamili ulionifikisha hapa.
Bonyeza Hapa 👇
*https://wa.link/pz47ru*
Karibu
0750376891.
Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan Amir.
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni
Chapisha Maoni