Siri Za Hadithi Za Mauzo...

 *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Rafiki Yangu, Wauzaji wengi wanahangaika kuandika matangazo yanayouza. Wanaandika, lakini hakuna anayeona, hakuna anayeuliza, hakuna anaye nunua. Ni maumivu makali kuona mtu mwingine anauza bidhaa kama yako, Lakini wewe unabaki unalalamika *soko ni gumu.* Kitabu *Siri Za Hadithi Za Mauzo* Kinakuonyesha namna ya kuandika hadithi zinazogusa mioyo, zinazoeleza, zinasisimua, na hatimaye zinauza. Utajifunza kuandika maandiko yanayovutia macho, yanayobeba hisia, na yanayobadilisha wasomaji kuwa wanunuzi. Pata nakala yako leo. Kwa kuwasiliana na 0755376891. PS; Anza kuandika hadithi zinazouza badala ya maneno yasiyoleta matokeo.

‎🔴 Wateja Wana Sababu 5 Tu Za Kukataa Kununua....

‎Na Kama Huzizimi Mapema, Utauza Ndoto Zako Tu!

‎Wewe ni muuzaji, MJASIRIAMALI au mfanyabiashara?


‎Huu ndio mfumo wa kukusaidia kuwauzia hata wateja wagumu kuliko wote.

‎Kumbuka, kazi yako si kuuza tu ni kuzima visingizio kabla havijaota meno.


‎Unahangaika na wateja.

‎Unawashawishi kwa nguvu.

‎Wanakuambia, "Ngoja nifikirie."

‎Au, "Nitaludi baadaye."

‎Na hakuna kinacholudi.

‎Tatizo si bei yako.

‎Tatizo si bidhaa yako.

‎Tatizo ni pingamizi ambazo hukuzizima mapema.

‎"Sina pesa sasa hivi."

‎"Nimewahi kununua kitu kama hiki, hakikufanya kazi."

‎"Nitamuuliza mke/mume wangu kwanza."

‎"Ngoja nifikirie kwanza."

‎"Si muda mzuri kwangu kwa sasa."

‎Hizo ni objections tano kuu.

‎Na kila objection ni bomba la kuzuia hela zako zishuke mfukoni.

‎Ukikaa kimya, imekula kwako.

‎Ukijitetea vibaya, wanakosa imani.

‎Ukizizima mapema... unashinda mapema.

‎Wauzaji wa kawaida hukimbia objections.

‎Wauzaji waliobobea huzizima kabla hazijasemwa.

‎Na hapa ndipo unahitaji kujua hizi tano:

‎Objection #1: Sina Pesa

‎✅ Zima mapema kwa kuuliza:

‎“Unaposema huna pesa, unamaanisha huna kabisa au una vipaumbele vingine kwa sasa?”

‎Objection #2: Nahitaji Kufikiria

‎✅ Zima mapema kwa kusema:

‎“Kama huna swali lolote sasa, kuna uwezekano unafikiri nini hasa kabla ya kusema ndiyo?”

‎Objection #3: Nitamuuliza Mwenza

‎✅ Zima kwa kuuliza:

‎“Je, tukimuita apate maelezo hapa hapa, itakuwa rahisi kufanya maamuzi pamoja?”

‎Objection #4: Si Muda Mzuri

‎✅ Zima kwa kusema:

‎“Niambie, kama huu ndio muda sahihi, ungetaka kuanza lini? Kwa nini?”

‎Objection #5: Sitaki Kufanya Makosa Tena

‎✅ Zima kwa kuwapa uthibitisho hai:

‎“Wengi waliokuwa na hofu kama yako, leo wanashangaa kwa nini walichelewa sana.”

‎ Tumia Mfumo wa Kuzizima Mapema

‎👉 Kila unapoanza kuwasilisha ofa, sema objections kabla hawajasema.

‎Unawashangaza.

‎Unawaamini.

‎Unawapunguza uoga.

‎Hii inaitwa: “Pre-framing objections.”

‎Ni kama kusafisha njia kabla hujapita.

‎Na matokeo yake?

‎Unafunga dili mapema. Bila kubembeleza.

‎. 📚 Hadithi ya Ukweli: Dili Langu la Milioni 5 Lilikimbia kwa Sababu Moja Tu...

‎Nilikuwa na client mmoja mkubwa.

‎Nikampelekea ofa ya huduma zangu — branding, copywriting, full funnel.

‎Akafurahi.

‎Akasema, “Hii kazi ni nzuri sana. Tutaongea na mke wangu halafu tukujulishe.”

‎Nikakosea.

‎Nikakubali kusubiri.

‎Siku mbili baadaye, sipokei simu.

‎Wiki ikapita, nikamuona ana-run campaign na jamaa mwingine.

‎Kilichotokea?

‎Sikuzima objection mapema.

‎Ningeuliza, “Je, mkeo ana nafasi ya kuongea leo tukajibu maswali yake moja kwa moja?” — hiyo milioni 5 ingekuwa yangu.

‎Tangu hapo, najua:

‎Objection ikishinda, unashindwa.

‎🔚 Mwisho wa Siku...

‎Wateja hawakatai kwa sababu hawapendi bidhaa yako.

‎Wanakataa kwa sababu wana maswali ambayo hujajibu mapema.

‎Na kazi yako sio kusubiri waulize

‎Ni kuwatuliza kabla hawajawa na wasiwasi.

‎📢 Ukijifunza kuzizima objections hizi tano,

‎utaanza kufunga dili hata kwa wale waliowahi kukukataa!

‎JIULIZE:

‎Leo umepoteza dili ngapi kwa sababu hukuzungumzia objections mapema?

‎Je, unataka mfumo huu kwa kina?

‎Jiunge na Kozi Ya Copywriting utajifunza kuwauzia hadi watu wagumu kama chuma!

‎Kujiunga Tuma Meseji "NIUNGE"

‎Kwenda 0750376891.

‎Karibu.

‎Rafiki Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

‎0750376891.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Mbinu 7 Za Kukumbuka Unachosoma Katika Vitabu Bila KUSAHAU TENA... ‎

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection