‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu? ...

 ‎ Hii hapa safari ya kugusa moyo wako. ‎ ‎Nawezaje Kuwa Mwanafunzi wa Maisha Kupitia Kusoma Vitabu?.... ‎ ‎Nilikuwa nimehitimu shule. ‎ ‎Nikiwa na cheti mkononi na ndoto kubwa kichwani. ‎ ‎Lakini maisha yakaniambia: “Karibu kwenye darasa halisi.” ‎ ‎Sikupata kazi niliyoitegemea. ‎ ‎Nikawa najiuliza: "Kwani elimu yangu haikutosha?" ‎ ‎Nilikuwa nimefundishwa mambo ya darasani lakini si maisha. ‎ ‎Siku moja nikakutana na nukuu: ‎ ‎“Don’t let school interfere with your education.” — Mark Twain ‎ ‎Nikaanza kujiuliza: ‎ ‎"Je, kuna elimu nyingine zaidi ya vyeti? Elimu ya maisha?" ‎ ‎Nikapuuzia. ‎ ‎Nikajua vitabu vya darasani tu ndivyo vya maana. ‎ ‎Niliona vitabu vingine kama vya watu walioshindwa. ‎ ‎Mbona havifundishwi shuleni? ‎ ‎Mbona havijasheheni nadharia na mitihani? ‎ ‎Mtu mmoja akanishika begani na kuniambia: ‎ ‎"Unapokoma kuwa mwanafunzi, ndipo unapokoma kukua." ‎ ‎Akanipa kitabu cha “Rich Dad Poor Dad.” ‎ ‎Akaniongeza na kingine:  ‎ ‎“The 7 Habits of ...

‎🔴 Wateja Wana Sababu 5 Tu Za Kukataa Kununua....

‎Na Kama Huzizimi Mapema, Utauza Ndoto Zako Tu!

‎Wewe ni muuzaji, MJASIRIAMALI au mfanyabiashara?


‎Huu ndio mfumo wa kukusaidia kuwauzia hata wateja wagumu kuliko wote.

‎Kumbuka, kazi yako si kuuza tu ni kuzima visingizio kabla havijaota meno.


‎Unahangaika na wateja.

‎Unawashawishi kwa nguvu.

‎Wanakuambia, "Ngoja nifikirie."

‎Au, "Nitaludi baadaye."

‎Na hakuna kinacholudi.

‎Tatizo si bei yako.

‎Tatizo si bidhaa yako.

‎Tatizo ni pingamizi ambazo hukuzizima mapema.

‎"Sina pesa sasa hivi."

‎"Nimewahi kununua kitu kama hiki, hakikufanya kazi."

‎"Nitamuuliza mke/mume wangu kwanza."

‎"Ngoja nifikirie kwanza."

‎"Si muda mzuri kwangu kwa sasa."

‎Hizo ni objections tano kuu.

‎Na kila objection ni bomba la kuzuia hela zako zishuke mfukoni.

‎Ukikaa kimya, imekula kwako.

‎Ukijitetea vibaya, wanakosa imani.

‎Ukizizima mapema... unashinda mapema.

‎Wauzaji wa kawaida hukimbia objections.

‎Wauzaji waliobobea huzizima kabla hazijasemwa.

‎Na hapa ndipo unahitaji kujua hizi tano:

‎Objection #1: Sina Pesa

‎✅ Zima mapema kwa kuuliza:

‎“Unaposema huna pesa, unamaanisha huna kabisa au una vipaumbele vingine kwa sasa?”

‎Objection #2: Nahitaji Kufikiria

‎✅ Zima mapema kwa kusema:

‎“Kama huna swali lolote sasa, kuna uwezekano unafikiri nini hasa kabla ya kusema ndiyo?”

‎Objection #3: Nitamuuliza Mwenza

‎✅ Zima kwa kuuliza:

‎“Je, tukimuita apate maelezo hapa hapa, itakuwa rahisi kufanya maamuzi pamoja?”

‎Objection #4: Si Muda Mzuri

‎✅ Zima kwa kusema:

‎“Niambie, kama huu ndio muda sahihi, ungetaka kuanza lini? Kwa nini?”

‎Objection #5: Sitaki Kufanya Makosa Tena

‎✅ Zima kwa kuwapa uthibitisho hai:

‎“Wengi waliokuwa na hofu kama yako, leo wanashangaa kwa nini walichelewa sana.”

‎ Tumia Mfumo wa Kuzizima Mapema

‎👉 Kila unapoanza kuwasilisha ofa, sema objections kabla hawajasema.

‎Unawashangaza.

‎Unawaamini.

‎Unawapunguza uoga.

‎Hii inaitwa: “Pre-framing objections.”

‎Ni kama kusafisha njia kabla hujapita.

‎Na matokeo yake?

‎Unafunga dili mapema. Bila kubembeleza.

‎. 📚 Hadithi ya Ukweli: Dili Langu la Milioni 5 Lilikimbia kwa Sababu Moja Tu...

‎Nilikuwa na client mmoja mkubwa.

‎Nikampelekea ofa ya huduma zangu — branding, copywriting, full funnel.

‎Akafurahi.

‎Akasema, “Hii kazi ni nzuri sana. Tutaongea na mke wangu halafu tukujulishe.”

‎Nikakosea.

‎Nikakubali kusubiri.

‎Siku mbili baadaye, sipokei simu.

‎Wiki ikapita, nikamuona ana-run campaign na jamaa mwingine.

‎Kilichotokea?

‎Sikuzima objection mapema.

‎Ningeuliza, “Je, mkeo ana nafasi ya kuongea leo tukajibu maswali yake moja kwa moja?” — hiyo milioni 5 ingekuwa yangu.

‎Tangu hapo, najua:

‎Objection ikishinda, unashindwa.

‎🔚 Mwisho wa Siku...

‎Wateja hawakatai kwa sababu hawapendi bidhaa yako.

‎Wanakataa kwa sababu wana maswali ambayo hujajibu mapema.

‎Na kazi yako sio kusubiri waulize

‎Ni kuwatuliza kabla hawajawa na wasiwasi.

‎📢 Ukijifunza kuzizima objections hizi tano,

‎utaanza kufunga dili hata kwa wale waliowahi kukukataa!

‎JIULIZE:

‎Leo umepoteza dili ngapi kwa sababu hukuzungumzia objections mapema?

‎Je, unataka mfumo huu kwa kina?

‎Jiunge na Kozi Ya Copywriting utajifunza kuwauzia hadi watu wagumu kama chuma!

‎Kujiunga Tuma Meseji "NIUNGE"

‎Kwenda 0750376891.

‎Karibu.

‎Rafiki Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan Amir.

‎0750376891.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

‎Jinsi Ya Kutumia Vitabu Kujenga Maisha Na Biashara Bila Mtaji Mkubwa...

‎Hatua 7 Rahisi Za Kuanzisha Ndoto Yako Bila Mtaji Mkubwa- Hata Kama Huna Connection

Vitabu Gani Vilibadilisha Maisha Yangu?